Hivi ni kipi kilipaswa kujengwa kwanza, ni kuinua daraja la Jangwani au kujenga Daraja jipya la Salenda hadi Coco beach?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,477
30,137
Baada ya kuona haya mateso makubwa wanayopata wanabchi kwa kufunga barabara inayounganisha jijini Dar na Magomeni ikijirudia Mara kwa Mara kutokana na mvua kunyesha, nimekuwa nikijiuliza hivi hawa watawala wetu walitumia busara kweli kuamua kujenga daraja la kuunganisha Coco beach na Salenda, badala ya kutoa kipaumbele cha kuliinua daraja la Jangwani?

Imekuwa ni kawaida sana kwa siku za karibuni kila mvua inaponyesha, hata kama ni ndogo, tunaambiwa kuwa barabara ya Morogoro, inayounganisha Magomeni na jijini Dar imefungwa

Hebu tujaribu ku-imagine ni madhara kiasi gani yanayopatikana kiuchumi kila barabara hiyo inapofungwa?

Hebu pia tujaribu ku-imagine ni wakazi wangapi wanapata usumbufu wa kutokwenda kutibiwa kwenye hospitali ya Muhimbili au kwenda waona wapendwa wao waliolazwa katika hospitali hiyo kubwa hapa nchini kutokana na kadhia hiyo?

Lakini kwa kuwa nchi hii hivi sasa tunajua kuwa inaendeshwa kwa "misifa" ya ONE MAN SHOW, kila alitakalo bwana yule ni lazima litekelezwe, bila kwanza kuangalia ni kitu gani cha kutoa kipaumbele kwa muda tulionao

Nina hakika watu maelfu kwa maelfu wanaathirika sana na hii barabara ya Morogoro ya kipande cha daraja la Jangwani kinachounganisha Magomeni na jijini Dar

Pia soma:
1). Magufuli: Tutajenga flyover Salender Bridge
2). Yaliyojiri Uwekaji wa jiwe la msingi Daraja la Selander
3). Wabunge pingeni na kataeni kujengwa kwa Daraja la Juu ya Bahari kutoka Coco Beach to Agakhan

Serikali haikukosea na sipingi ujenzi wa daraja jipya la salenda lenye urefu wa km 1.5 ambalo ni kubwa kuliko lile la nyerere kule kigamboni.
Lakini ujenzi huu umekuja katika wakati ambao kwa maoni yangu sio sahihi ukilinganisha na kero nyingi za wananchi zilizopo kwa Sasa.

Ujenzi huu unagharimu Tsh bil 556.1 huku serikali ikitoa bil 49.5 ikiwa zaidi ya bil 506 zikiwa ni ufadhili kutoka Korea kusini.

Pamoja na kuwa mradi huu umekuja kwa lengo la kupunguza adha ya foleni katika eneo hili lakini kuna maeneo muhimu zaidi katika mkoa wa Dar es salaam ambayo yalitakiwa kupewa nafasi ya kwanza kwenye ujenzi.

1; Daraja la Jangwani.
Daraja hili ni kiuongo muhimu Sana hapa jijini, ikumbukwe kuwa shughuli nyingi za wana dar hutegemea sehemu hii kuunganisha wilaya kinondoni na Ilala kupitia fire na magomeni.
Mara nyingi daraja hili limekuwa likikumbwa na adha ya mafuriko na kufunikwa na maji hivyo kukwamisha shughuli nyingi kwa masaa mengi Sana. Hii ni kero kubwa na niaibu kwa jiji letu hili bora kabisa Afrika mashariki.
Badala ya daraja la salenda serikali ingeanza na hili kwanza.

2; daraja la mto msimbazi katika eneo la kigogo njia panda.
Hapa napo ni sehemu korofi sana lakini ina umuhimu mkubwa kwa wakazi wa jiji la Dar Kama ilivyo kwa eneo la Jangwani hapa napo tatizo ni lile lile, serikali isifumbue macho eneo hili, kila siku Makonda anakuja hapa kujifanya kuangalia athari za mafuriko bila kuchukua hatua yoyote ile, hapana tumechoka Sasa.
Badala kujenga daraja la salenda mngeanza hapa kwanza.

Na sio kujenga daraja tu bali mje na
mpango mkakati wajinsi ya kutanua mto msimbazi kupunguza athari za mafuriko kwa wakazi hawa.

Nasisitiza kusema ujenzi wa daraja la salenda serikali yangu imekurupuka mlitakiwa kuangalia ni eneo gani linagusa watu zaidi Kama kweli hii ni serikali ya wanyonge.

Achaneni na miradi inayolenga tu kupendezesha jiji huku wananchi wanalia.
Mh Rais wangu mpendwa naomba liangalie hili utakuja kuwaambia nini Wana Dar es salaam wakati wa kampeni??
Umejenga mfugale na ubungo ujenzi unaendelea hatupingi kabisa lakini hao watu wanao tokea kimara kupita ubungo kwenye flyover kuja kariakoo watapita wapi wakati Jangwani daraja linajaa maji MH RAIS?

Mh Makonda unayaona haya?
Wananchi wamechoka kukuona unakuja na macamera kupiga picha za daraja kufunikwa na maji watu wanashindwa kuendelea na shughuli za kila siku we kazi unakuja kupiga picha au mnaona kuwa hili ni kivutio cha utalii.???
Tumechoka!!.
 
Ni kweli hupangiwi, lakini unaona mateso makubwa wanayopata wananchi wako kwa kuifunga barabara muhimu sana ya Morogoro, Mara kwa Mara?

Dala la kuunganisha Coco beach wanapita matajiri na ma Beberu wahisani wetu.
Jangwani wanapita machinga na wauza nyanya na njegere Kariakoo.

Hapo utapima mwenye we!

Mbona haujauliza Chato Airport uulize na jangwani kipi kilitakiwa kiwe kipaumbele?
 
Tuna miundo mbinu ya hovyo sana Dar tena miaka yote , yaani hapo Jangwani kumeshindikana mara utasikia feasibility study zinatumia bil 50, mara tunasubiri world bank.

Tatizo kubwa hatuna mipango ya maana ya maendeleo, tukangefanya tafiti ya maeneo korofi yote mfano jangwani ,sewage system modernization ya mji wote Dar, Barabara za mwendo kasi phase 2 & 3, tukazichukulia mkopo mara moja kwa pamoja zikajengwa.

Baada ya hapo kinachobaki inakuwa ni kulipa tu loan, shida iko pale mnakaa miaka mitano mkisubiri pesa mpate huku watu wanatabika, au mnakwenda kuchukua mkopo wa jangwani peke yake ,baada hapo mnakaa kusubiri tena tatizo litokee sehemu Fulani hao mnakimbia huku mara kule, very bad.

Chukueni mara moja mikopo jengeni mmalize yote then kaaeni kukusanya pesa mlipe, ndio maana Africa iko hivi, watu wanahamia sehemu fulani wanazaliana ,population inaongezeka, hawana maji au barabara ndio serikali inatoka usingizini kuanza kuplan wakati huo kumekuwa hakuna jinsi wanaishia kubomolea watu majumba yao.

wakati nchi za nje wanapeleka kwanza maji, barabara zinajengwa, umeme unakuwa huko, shule zinajengwa, hospital halafu wana encourage watu wahamie kule, sisi ni opposite kila kitu ni holela sijui tuna nini kichwani. Mnakumbuka Jangwani tumeimba miaka yote, mwendo kasi kelele nyingi tumeishia phase leo 2020, mitaro ndio hivyo tena mvua ikinyesha, 58 yrs ya uhuru hatujui tufanye nini, wapisheni na wengine wajaribu.
 
Naipenda Dar yangu nilipozaliwa na kukulia.

Aliyejenga au aliyechora barabara ya BRT na lile daraja ni HITMAN na hili la kufunga barabara baada kujaa maji pale litatusumbia daima hadi patakapofumuliwa pale na kujenga kwa usahihi bila kuathiri njia ya maji.

Zamani nyuma ya miaka 10 iliyopita tulikuwa tukipita pale mto upo chini ya daraja na kina unakiona. Baada ya BRT kukamilika mto unauona level moja na daraja. Depo ya kupaki UDART kimejengwa eneo siyo sahihi hii yote ni kutupatia hasara endelevu.

Wataalam wa uhandisi wapitie hiyo michoro na kubaini kama kuna kasoro za kiupangaji zirekebishwe haraka.

Mnapopita pale jangwani siku zote kuna kijiko kinatoa mchanga na taka ili kuongeza kina cha mto. Sishawishiki kuamini kwamba hapakuwepo mchanga na taka hapo zamani bali there is something done inapelekea hii hali ya kufungwa barabara kutokea kila mvua inaponyesha.

Vyombo vya uchunguzi vichunguze kwa undani hili jambo. Inawezekana kuna ushauri ulipuuzwa kwa makusudi. Ikumbukwe kuna siku Rais wa wakati huo alipita eneo hilo wakati depo ya UDART inajengwa akaamrisha ujenzi usimame lakini baadae aliruhusu baada ya kugundua utaratibu ulifuatwa. Najiuliza ni kina nani walipitisha hayo maamuzi na kama walishauriwa kinyume na kupuuzia...

Inavyoelekea tunaanza kuizoea hali hii na kuishi nayo kama hewala.

Copy & Paste Kutoka Whatsapp



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanapenda sifa ndio maana wala hawana mpango na Jangwani. Miradi tunayopenda lazima iwe na hii sifa ......"Daraja la kwa Mtogole ndio Daraja Jembamba zaidi Kusini mwa Afrika"
 
Jamani mabeberu watu wabaya sana wanaleta mvua halafu wanakimbia
IMG_20200116_220427.jpg
IMG_20200116_220435.jpg
 
Dala la kuunganisha Coco beach wanapita matajiri na ma Beberu wahisani wetu.
Jangwani wanapita machinga na wauza nyanya na njegere Kariakoo.
Hapo utapima mwenye we!
Mbona haujauliza Chato Airport uulize na jangwani kipi kilitakiwa kiwe kipaumbele?
Kumbe Mkuu impongo hao tunawaita mabeberu pale tunapowaponda, lakini tunapowanyenyekea na wanapotupa misaada, jina lao linabadilika na kuwa wahisani?
 
Wanapenda sifa ndio maana wala hawana mpango na Jangwani. Miradi tunayopenda lazima iwe na hii sifa ......"Daraja la kwa Mtogole ndio Daraja Jembamba zaidi Kusini mwa Afrika"
mkuu mengine yapo malawi kwenye barabara wanaita lake shore ya mzuzu salima,Nkhokhotha mpaka Baraka then Blantyre or Zomba
 
Back
Top Bottom