Hivi ni huruma tu ya wanawake au kuna tatizo la ziada?

magode

JF-Expert Member
Oct 2, 2014
2,200
3,317
Wanajamvi,

Heri ya mwaka mpya 2017.

Kuna jambo limekuwa likinisumbua sana akilini mwangu. Kwenye suala la mapenzi na ndoa, kuna hili jambo la fumanizi linapotokea kati ya mwanaume na mwanamke na uamzi unaochukuliwa kwa pande zote mbili.

-Wanawake: Mwanamke anaweza kuwa na mume, mchumba au mpenzi. Katika uhusiano wao anaweza kuwa anashuhudia dalili za kusalitiwa kwa hata 80%, anaweza kukuta sms za wapenzi kwa mwenza wake, au mazingira mengine. Akijaribu kuhoji atapewa uongo wawazi kabisa lakini atauamini na kuendelea na penzi lake.

Anaweza kufumania kabisa mtu wake akiwa kitandani na mtu wake tena kitanda kilekile anacholala yeye anapokuwepo. Atalia hata kuzimia lakini baadae ataanza kujipendekeza na hata kuapa kupigania penzi lake hata kama dalili zote zinaonyesha yeye hatakiwi. Hapa ndo najiuliza huwa kuna nini kichwani mwa wanawake?

-Wanaume: Mwanaume akiwa katika uhusiano na mke, mchumba au mpenzi na ikatokea kafumania hata sms tu ya mwenza wake ikionyesha akijihusisha na mtu mwingine hali huwa ni mbaya sana.

Mwanamke atajitahidi kujieleza lakini kueleweka huwa ni ngumu sana na mara nyingi uhusiano hufikia tamati. Hata ikitokea wakaendelea lakini hilo hubakia tusi kwa mwanamke. Atatukanwa kila aina ya tusi kuonyesha jinsi alivyo malaya.

Wanajamvi kwanini kunakuwa na hii mitizamo isiyolingana? Hivi ni vigumu sana kwa wadada kuwaacha wapenzi wao hata wakiwa na idadi kubwa ya michepuko? Na kwanini wanaume hawana uwezo wa kusamehe wakifumania hata kama na yeye alishafumaniwa akasamehewa?

Nawasilisha.
 
namtakia maisha marefu sana na yenye baraka tele mama yangu na wanawake wote wanaojua ndoa nini
ahsante mkuu kwa maoni yako. Lkn hujamtendea haki pia Baba ambae kwa namna yoyote kwenye ndoa iliyodumu kwa upendo huwa ni mchango wa wahusika 50% kwa 50%.
 
unachoongea ni kweli ila wanawake wenye moyo huo ni wale waliozaliwa kuanzia mwaka 1979 na kurudi nyuma.. ila kuanzia 1980 na kuendelea mbele mmmmh!!! aisee ni wa kutafuta na kurunzi, hata wanaume ambao wana tabia ulizoorodheshe ni wale wa kipindi cha nyuma kwa maana wanaume wengi siku hizi baada ya kushuhudia manyanyaso wanayopata mama zao nao wakaelimika, wengi wamestaaribika, kwa kuwa siku hizi mimi binafsi nashuhudia wanaume wengi sana wananyanyaswa kimapenzi na wapenzi wao kuliko wanawake, kwa hiyo tuseme mchezo umebadilika kwa nyakati hizi.
 
unachoongea ni kweli ila wanawake wenye moyo huo ni wale waliozaliwa kuanzia mwaka 1979 na kurudi nyuma.. ila kuanzia 1980 na kuendelea mbele mmmmh!!! aisee ni wa kutafuta na kurunzi, hata wanaume ambao wana tabia ulizoorodheshe ni wale wa kipindi cha nyuma kwa maana wanaume wengi siku hizi baada ya kushuhudia manyanyaso wanayopata mama zao nao wakaelimika, wengi wamestaaribika, kwa kuwa siku hizi mimi binafsi nashuhudia wanaume wengi sana wananyanyaswa kimapenzi na wapenzi wao kuliko wanawake, kwa hiyo tuseme mchezo umebadilika kwa nyakati hizi.
Mmmmh!!
 
bulletproof-bodyarmor-hq.jpg

If you get shot with a vest on, you replace the vest. You shoot a gun, you re-load and keep them slugs flying.
 
Mwanaume akipata mwanamke mtundu kitandani huwa hana maneno. Hata ajuwe mwanamke wake ana gegedwa basi hubaki kuumia moyoni tu.
Kwa Mwanamke akipata mwanaume mtundu kitandani pia awe na pesa na anampenda. Hawezi kufanya lolote hata akiwa mwanaume wake anatembea na shoga yake. Hubakia kumnunia shoga yake lakini tamaa yake na utamu wa mgegedo ndio vilivyo mponza.
 
Mwanaume akipata mwanamke mtundu kitandani huwa hana maneno. Hata ajuwe mwanamke wake ana gegedwa basi hubaki kuumia moyoni tu.
Kwa Mwanamke akipata mwanaume mtundu kitandani pia awe na pesa na anampenda. Hawezi kufanya lolote hata akiwa mwanaume wake anatembea na shoga yake. Hubakia kumnunia shoga yake lakini tamaa yake na utamu wa mgegedo ndio vilivyo mponza.
Mkuu labda wewe na wengine ila sio mwanaume mimi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom