Uchaguzi 2020 Hivi ni haki kweli kwa akina Robert Amsterdam kuingilia uchaguzi mkuu wa nchi yetu? Je, tunaweza kuwashitaki kwenye mahakama za kimataifa?

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,952
4,326
Ni kweli kama walivyosema kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni wa kihistoria.Haijawahi kutokea huko nyuma, kwa uchaguzi mkuu wa nchi yetu kuingiliwa ki wazi wazi na watu wa nchi za nje wa aina ya akina Robert Amsterdam!

Sijui ingalikuwaje kama kila mgombea wa urais katika uchaguzi huu angalikuwa na Amsterdam wake kutoka mataifa yenye nguvu duniani; yakimprotect mgombea wao na kutishia kuwafikisha kwenye mahakama ya ICC wale wote watakaoonekana kuwa tishio la mgombea wao kupata ushindi.

Fikiria kama Benard Membe naye angalikuwa na Amstedam wake, kwa dhoruba alilolipata, Seif na Zitto wangalikuwa wanasubiri kufikishwa ICC!! Fikiria dhoruba wanayoipata akina Hashim Rungwe kwa kuzuiliwa kutoa ubwabwa kwenye kampeni zao, idadi ya watu wangaliofikishwa mahakama ya ICC wangalikuwa kiasi gani? Fikiria dhoruba wanayoipata akina Lipumba na kadhalika kwa kukosa mafuriko kwenye mikutano yao na kadhalika.

Huko kwa akina Amsterdam nchi nyingine hata kuhisiwa tu kama ilishiriki kuingilia uchaguzi wa nchi yao huwa ni jambo lisilokubalika. Tulishuhudia kasheshe iliyotokea kwa China na Urusi kuhisiwa kusaidia ushindi wa Trump katika uchaguzi mkuu wa Marekani wa mwaka 2016. Kasheshe hii hadi sasa haijaisha na wala Trump mambo ya ICC hayamuhusu.

Sasa jee tunaweza kuwashitaki kwenye mahakama za kimataifa hawa akina Robert Amsterdam ambao wazi wazi kabisa wameingilia uchaguzi mkuu wetu? Au sheria za kimataifa zinasema nini juu ya watu kama hawa?
 
Wameingiliaje uchaguzi?

Kuzungumzia ukweli ni kuingilia uchaguzi? Siku hizi hakuna uchaguzi wa peke yako, upeke yako unabaki katika kutiki tuu karatasi ya kura lakini mengine yanawahusu wote was ulinwengu huu.

Kama uliusoma ujumbe wa Balozi wa Marekani nadhani utakuwa umeelewa vizuri alimaanisha nini umuhimu wa uchaguzi wa TZ na mataifa yote ya East and Central.

Kukubali kunyamazia ujinga wa jirani kisha yale ya Rwanda au Burundi yanatokea kisha ndio wanajitokeza utakuwa upuuzi wa hali ya juu
 
Amsterdam ni tapeli mpiga debe tu, wala usiwe na wasiwasi naye kabisa. Ubaya kwake ni kuwa anapambana na mtu mwenye msimamo. Wewe focus kwenye uchaguzi tu usihangaike na Amsterdam hata siku moja; atalala usingizi muda wowote kuanzia sasa.
 
Tendeni haki...tume iwe huru...Malawi wagombea walisaidiwa kujaza fomu na tume ya uchaguzi...HAKI
Hapa duniani kuna sheria tu, haki iko mbinguni kwa Mwenyezi Mungu. Hivyo kwetu hapa duniani haki ni zile sheria tulizojitungia wenyewe kwenye bunge letu na haki za aina hiyo hupatikana mahakamani tu kama unaona au kuhisi hujatendewa haki.

Tume yetu iko huru kwa mjibu wa sheria zetu na katiba yetu. Kama unahisi haiko huru nenda kaidai mahakamani, vinginevyo utakuwa unataka kuleta vurugu na kuvunja amani yetu.
 
Wameingiliaje uchaguzi?
Kuzungumzia ukweli ni kuingilia uchaguzi? Siku hizi hakuna uchaguzi wa peke yako, upeke yako unabaki katika kutiki tuu karatasi ya kura lakini mengine yanawahusu wote was ulinwengu huu.
Kama uliusoma ujumbe wa Balozi wa Marekani nadhani utakuwa umeelewa vizuri alimaanisha nini umuhimu wa uchaguzi wa TZ na mataifa yote ya East and Central.
Kukubali kunyamazia ujinga wa jirani kisha yale ya Rwanda au Burundi yanatokea kisha ndio wanajitokeza utakuwa upuuzi wa hali ya juu
Haya na wewe nenda Marekani ukafanye kama alivyofanya kwetu Amsterdam! Haitachukua hata sekunde moja utakuwa ahera ukiserebuka!
 
Haya na wewe nenda Marekani ukafanye kama alivyofanya kwetu Amsterdam! Haitachukua hata sekunde moja utakuwa ahera ukiserebuka!
Ziko sababu nyingi ambazo zinanifanya nisiwe huru kuingilia uchaguzi wa Marekani nawe wazifahamu.

Mzazi aweza kumkagua mwanae kama kavaa chupi safi na lisiwe kosa au mjadala, lakini mtoto hawezi muuliza mamaye hata rangi ya chupi.

Ona Burundi tuu, mnachafuana na kuzalisha wakimbizi ambao hata kuwalisha mlo mmoja hamuwezi bado anayewalisha akae kimya?
 
Anza kuwashitaki CCM wanawabambikia kesi wafanyabiashara wakubwa kodi kubwa za TRA kuwapa kesi za uhujumu uchumi kiuonevu, kuwabambikia kesi kesi kuwapiga risasi wapinzani uonevu unyanyasaji uovu mwingi wa CCM kwa wapinzani anza na huo kwanza kisha ufuate wizi wa trilion 1.5 wakamtoa CAG kafara na zile bilion 12 za Ndungai kule india na hata ujenzi wa chato Airport kienyeji pasipo idhini ya bunge, anza kuwashitaki hao ndipo uende kwa Amsterdam
 
Haya na wewe nenda Marekani ukafanye kama alivyofanya kwetu Amsterdam! Haitachukua hata sekunde moja utakuwa ahera ukiserebuka!
Marekani hakuna ujinga ushetani wa kupita bila kupingwa wala NECCCM Polisiccm kuwa chombo binafsi cha chama Tawala , hawana mambo ya hovyo kama yaliyopo kwenye utawala huu wa kisukuma wa Mkoloni mweusi kaburu wa Chato
 
Mithali 34:14
Haki huinua Taifa na dhambi ni aibu ya watu wote.

Hivi ushawahi kujiuliza ni kwanini watawala wetu, wanahimiza sana wananchi wa nchi hii, tudumishe AMANI bila kudumisha utekelezaji wa HAKI kwenye majukumu yao?

Kwa kuwa imenenwa kuwa AMANI NI ZAO LA HAKI
 
Hapa duniani kuna sheria tu, haki iko mbinguni kwa Mwenyezi Mungu. Hivyo kwetu hapa duniani haki ni zile sheria tulizojitungia wenyewe kwenye bunge letu na haki za aina hiyo hupatikana mahakamani tu kama unaona au kuhisi hujatendewa haki. Tume yetu iko huru kwa mjibu wa sheria zetu na katiba yetu. Kama unahisi haiko huru nenda kaidai mahakamani, vinginevyo utakuwa unataka kuleta vurugu na kuvunja amani yetu.
Aende kudai Haki kwenye mahakama ipi? Maana mahakamaccm haipo huru na haitoi HAKI hususani kwa wanachadema au aende kudai haki kwenye mahakama ya Dunia?
 
Hivi utawezaje kudumisha AMANI, wakati nchi imeu-introduce msamiati mpya wa WATU WASIOJULIKANA?

Hivi yuko wapi Bensaanane?

Yuko wapi Azory Gwanda?

Wako wapi waliotaka kumwua Tundu Lissu?

Ni uhayawani kuweza kuhubiri tudumishe AMANI, bila kwanza kuwahimiza watawala wetu watende HAKI katika utendaji wao
 
Ukisikiliza interview ya Lissu leo, barua ya Amsterdam ya jana na threads za kumtangaza mshindi zinazoanzishwa JF.

Utabaini wana ka coordinated move chao uchwara wa kujiandaa kukataa matokeo eti Lissu anadai kwa kile alichoita survey iliyofanywa na CDM (which is opinion poll kwa lugha sahihi, huyu ndio mtu anaekosoa English za wenzake) inaonyesha atashinda kwa asilimia 65-75 kwa ushahidi kwamba ni yeye pekee ndio mikutano yake ilikuwa inajaa na ya Magufuli awezi jilinganisha nae kwakuwa anakusanya wanafunzi tu.

Lissu is something else I am glad idadi ya watanzania inaongezeka mtaani ambao wameanza kukerwa jinsi polisi wanavyocheka nae.

Like I said halipo wasili kutoka Belgium the extent of mental problems za Lissu watu watakuja kuona baada ya uchaguzi.

Busara ni kupata akae nae chini mapema na kumrudisha duniani kutoka lala land halipo aache kujiweka on equal per with Magufuli hilo jambo litamtesa kwa sababu Magufuli week hii inayofuata atashinda tena kwa kishindo.
 
Lisu = Kigogo (chahali)= amsterdam hiyo ni project moja ya mabeberu kujaribu kutu destabilize.
 
Nilisoma barua yake ya wazi kwa JPM na website yake imetrend jina la Tanzania tu,nilichogundua kwa huyu jamaa ni kama mambo yanakuja kwa namna ambavyo hawakutegemea.

tatizo lao kuanzia lissu,amsterdam,chahali wanamtazamo hasi juu ya watanzania wamecheza vita ya kisaikolojia lakini wamejikuta pabaya sana :)
 
Dr. Akili, wewe kweli ni daktari au topasi. Kama ni daktari basi vyeti vyako ni FAKE. Tanzania wamekubali UNIVERSAL DECLARATION ON HUMAN RIGHTS. Masuala ya human rights hayana mipaka na mataifa, katika miaka mitano iliopita wame badilisha katiba za nchi yao kuingiliana na masuala haya.

Kwa hiyo masuala ya human rights hayana mipaka wala siyo masuala ya ndani ya nchi. Sisi wazenji tunajua kuwa tutakuwa wa mwanzo kuuliwa kwa sababu tunaikataa CCM kwa asilimia 90. Wakimtangaza mtalii wao tunaingia barabarani mpaka kieleweke. Haiwezekani kila miaka mitano CCM wanaiba kura na tunanyamaza . Munakaribishwa zenji.
 
Back
Top Bottom