Hivi ni fasheni au nini kuvivalisha vitoto vinguo vya ajabuajabu

EvilSpirit

JF-Expert Member
Jun 15, 2017
8,560
12,676
Povu langu linawahusu nyie wazazi,Ukiwa kwenye sehemu kama sabasaba ni kawaida kuwaona wazazi wakiwa na watoto wao wakiwa wamewavalisha vivazi vya ajabu ajabu watoto wao hasa watoto wa kike.Unamkuta mtoto kavalishwa kisketi kifupi.Ninahisi hata hawa wanaotuvalia nusu nyuchi leo hii watakuwa wametokea huko kwenye kuvalishwa vinguo vya ajabu ajabu wakiwa watoto.

Hata hayo manywele mnaowasuka watoto na yenyewe sio mazuri unamsuka mtoto utafikiri mtu mzima ili iweje.Najua wengine lengo lenu mpate sifa watoto wenu wanapendeza lakini hamjui madhara yake.Watoto unaambiwa utosi unakuwa haujakomaa sasa kwanini umsuke mtoto kwa style ya kuzivuta nywele zake au kumuwekea midawa ya ajabuajabu hapa bila shaka hayo makemikali yanaanza kumla mtoto toka akiwa mdogo


hili la kuwavalisha watoto vimini yataendelea hata watakapokuwa watu wazima .Mtakuja kuwalaumu watoto bure kumbe nyie ndio mmewafanya wawe hivyo watavyokujua kuwa.Kwa upande wa watoto wa kiume wenyewe wanawanyoa minyoo ya kiduku kila mtoto siku hizi unamkuta ana kiduku kama jogoo.Hivi ni fasheni au mnapenda kuigaiga kila mnachokiona.Kuna siku mzazi atamtoboa masikio mtoto wake wa kiume kwa ajili ya kumvalisha heleni na yenyewe mtaanza kuiga
 
Povu langu linawahusu nyie wazazi,Ukiwa kwenye sehemu kama sabasaba ni kawaida kuwaona wazazi wakiwa na watoto wao wakiwa wamewavalisha vivazi vya ajabu ajabu watoto wao hasa watoto wa kike.Unamkuta mtoto kavalishwa kisketi kifupi.Ninahisi hata hawa wanaotuvalia nusu nyuchi leo hii watakuwa wametokea huko kwenye kuvalishwa vinguo vya ajabu ajabu wakiwa watoto.

Hata hayo manywele mnaowasuka watoto na yenyewe sio mazuri unamsuka mtoto utafikiri mtu mzima ili iweje.Najua wengine lengo lenu mpate sifa watoto wenu wanapendeza lakini hamjui madhara yake.Watoto unaambiwa utosi unakuwa haujakomaa sasa kwanini umsuke mtoto kwa style ya kuzivuta nywele zake au kumuwekea midawa ya ajabuajabu hapa bila shaka hayo makemikali yanaanza kumla mtoto toka akiwa mdogo


hili la kuwavalisha watoto vimini yataendelea hata watakapokuwa watu wazima .Mtakuja kuwalaumu watoto bure kumbe nyie ndio mmewafanya wawe hivyo watavyokujua kuwa.Kwa upande wa watoto wa kiume wenyewe wanawanyoa minyoo ya kiduku kila mtoto siku hizi unamkuta ana kiduku kama jogoo.Hivi ni fasheni au mnapenda kuigaiga kila mnachokiona.Kuna siku mzazi atamtoboa masikio mtoto wake wa kiume kwa ajili ya kumvalisha heleni na yenyewe mtaanza kuiga
Ungewauliza hao wazazi huko 77 ulipowaona
 
Povu langu linawahusu nyie wazazi,Ukiwa kwenye sehemu kama sabasaba ni kawaida kuwaona wazazi wakiwa na watoto wao wakiwa wamewavalisha vivazi vya ajabu ajabu watoto wao hasa watoto wa kike.Unamkuta mtoto kavalishwa kisketi kifupi.Ninahisi hata hawa wanaotuvalia nusu nyuchi leo hii watakuwa wametokea huko kwenye kuvalishwa vinguo vya ajabu ajabu wakiwa watoto.
Hao ni watoto wa kidigital...tofauti na sisi tuliozaliwa kuanzia miaka ya 80,70,60,50
 
Back
Top Bottom