Mngurimi
JF-Expert Member
- May 27, 2020
- 819
- 789
Wakuu habari zenu..
Huu ni wakati ambao Watanzania wengi wapo macho sana kusikiliza taarifa kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania hasa zinazohusu uchaguzi mkuu unaopangwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu 2020. Kuna wale wenzangu na mimi ambao siasa kidogo na mambo mengine zaidi.
Leo ningependa nikupe mtazamo wangu wa vipindi vitano vya Radio na Tv vyenye ushawishi mkubwa sana wa kusikilizwa au kutazamwa kwenye media za hapa Bongo.
1. Friday Night Live (FNL)
Hiki ni kipindi ambacho huruka kila siku za Ijumaa kuanzia majira ya saa 3:00 usiku hadi saa 5:00 usiku. Kipindi hiki ambacho hurushwa na kituo cha televisheni cha EATV ni kipindi ambacho kinaonekana kuwa na mvuto sana. Ukubwa wa kipindi hiki unatokana na ukweli kwamba wasanii wengi wa Afrika Mashariki wanapohitaji kutambulisha video zao mpya basi hufika hapo kuzitambulisha na hii huvutia watazamaji wengi hasa vijana kukitazama ili waone video mpya iliyotoka/zilizotoka.
2. XXL ya Clouds Fm:
Unaweza kukataa au kukubali lakini mnyonge mnyongeni isipokuwa msimdhulumu haki yake. XXL ni moja kati ya show kali sana ambayo huruka kila siku kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa saa 7:00 mchana hadi saa 10:00 alasiri.
Hiki ni kipindi ambacho kimekuwa kivutio sana kwa vijana ambao wanapenda kupata habari za muziki wa ndani na nje ya Tanzania huku ma-dj wakali wakipamba kipindi.
3. Sitasahau:
Hiki ni kipindi ambacho mwanzoni kilikuwa kikiendeshwa na mtangazaji Roi Maganga ambaye kwa sasa hayupo tena pale RFA. Kipindi hiki kimekuwa kivutio cha wengi sio watoto, wazee na hata vijana na hualika wageni kutoa simulizi za mambo magumu waliyoyapitia kwenye maisha yao. Kipindi hiki huruka kila siku za Jumapili kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 5:00 pale Radio Free Africa.
Clouds Fm walikuja na kipindi cha kufanana na"Sitasahau" na wakakipa jina la "Njia panda" lakini bado ile ladha ya kipekee ya Sitasahau bado ipo juu.
4. Papaso ya TBC Fm:
Kuna watu wanadai kuwa kipindi hiki kimepoteza mvuto lakini nikwambie kitu kimoja kuwa hakuna kipindi chenye wasikilizaji wengi hasa vijijini kama PAPASO. Mtangazaji wa kipindi hiki D'jaro Arungu mbali na kujizolea umaarufu mkubwa lakini ameshinda tunzo kadhaa za kuwa Mtangazaji bora kupitia kipindi chake.
Papaso huruka kila siku za juma isipokuwa Jumamosi na Jumapili kuanzia 19:00 hadi 22:00 Maudhui ya kipindi hiki yapo kwenye burudani, habari, simulizi n.k.
5. ITV Habari:
Japo karibia vituo vyote vya televisheni vinasoma habari lakini bado ITV Habari kinakuwa na kipindi ambacho kina watazamaji wengi sana. Kipindi hiki huruka kila siku saa 2:00 usiku hadi saa 3:00 usiku. Ubora wa kipindi hiki unatokana na kuenea kwa reporters wake wengi nchi nzima na nje ya Tanzania na hutoa habari zenye uhakika na zilizohaririwa kwa kiwango cha juu.
HITIMISHO
Vipindi hivyo hapo juu ni kwa mujibu wa utafiti wangu nilioufanya kwa miaka kadhaa. Mpangilio huu pia hauhusiki na ni media gani yenye wasikilizaji wengi ila nimeegemea kwenye kipindi kama kipindi. Unaweza kuja na maoni yako pia ambayo yanaweza kuwa kinyume na mimi au ukaongeza list.
Naomba kuwasilisha....
Huu ni wakati ambao Watanzania wengi wapo macho sana kusikiliza taarifa kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania hasa zinazohusu uchaguzi mkuu unaopangwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu 2020. Kuna wale wenzangu na mimi ambao siasa kidogo na mambo mengine zaidi.
Leo ningependa nikupe mtazamo wangu wa vipindi vitano vya Radio na Tv vyenye ushawishi mkubwa sana wa kusikilizwa au kutazamwa kwenye media za hapa Bongo.
1. Friday Night Live (FNL)
Hiki ni kipindi ambacho huruka kila siku za Ijumaa kuanzia majira ya saa 3:00 usiku hadi saa 5:00 usiku. Kipindi hiki ambacho hurushwa na kituo cha televisheni cha EATV ni kipindi ambacho kinaonekana kuwa na mvuto sana. Ukubwa wa kipindi hiki unatokana na ukweli kwamba wasanii wengi wa Afrika Mashariki wanapohitaji kutambulisha video zao mpya basi hufika hapo kuzitambulisha na hii huvutia watazamaji wengi hasa vijana kukitazama ili waone video mpya iliyotoka/zilizotoka.
2. XXL ya Clouds Fm:
Unaweza kukataa au kukubali lakini mnyonge mnyongeni isipokuwa msimdhulumu haki yake. XXL ni moja kati ya show kali sana ambayo huruka kila siku kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa saa 7:00 mchana hadi saa 10:00 alasiri.
Hiki ni kipindi ambacho kimekuwa kivutio sana kwa vijana ambao wanapenda kupata habari za muziki wa ndani na nje ya Tanzania huku ma-dj wakali wakipamba kipindi.
3. Sitasahau:
Hiki ni kipindi ambacho mwanzoni kilikuwa kikiendeshwa na mtangazaji Roi Maganga ambaye kwa sasa hayupo tena pale RFA. Kipindi hiki kimekuwa kivutio cha wengi sio watoto, wazee na hata vijana na hualika wageni kutoa simulizi za mambo magumu waliyoyapitia kwenye maisha yao. Kipindi hiki huruka kila siku za Jumapili kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 5:00 pale Radio Free Africa.
Clouds Fm walikuja na kipindi cha kufanana na"Sitasahau" na wakakipa jina la "Njia panda" lakini bado ile ladha ya kipekee ya Sitasahau bado ipo juu.
4. Papaso ya TBC Fm:
Kuna watu wanadai kuwa kipindi hiki kimepoteza mvuto lakini nikwambie kitu kimoja kuwa hakuna kipindi chenye wasikilizaji wengi hasa vijijini kama PAPASO. Mtangazaji wa kipindi hiki D'jaro Arungu mbali na kujizolea umaarufu mkubwa lakini ameshinda tunzo kadhaa za kuwa Mtangazaji bora kupitia kipindi chake.
Papaso huruka kila siku za juma isipokuwa Jumamosi na Jumapili kuanzia 19:00 hadi 22:00 Maudhui ya kipindi hiki yapo kwenye burudani, habari, simulizi n.k.
5. ITV Habari:
Japo karibia vituo vyote vya televisheni vinasoma habari lakini bado ITV Habari kinakuwa na kipindi ambacho kina watazamaji wengi sana. Kipindi hiki huruka kila siku saa 2:00 usiku hadi saa 3:00 usiku. Ubora wa kipindi hiki unatokana na kuenea kwa reporters wake wengi nchi nzima na nje ya Tanzania na hutoa habari zenye uhakika na zilizohaririwa kwa kiwango cha juu.
HITIMISHO
Vipindi hivyo hapo juu ni kwa mujibu wa utafiti wangu nilioufanya kwa miaka kadhaa. Mpangilio huu pia hauhusiki na ni media gani yenye wasikilizaji wengi ila nimeegemea kwenye kipindi kama kipindi. Unaweza kuja na maoni yako pia ambayo yanaweza kuwa kinyume na mimi au ukaongeza list.
Naomba kuwasilisha....