Mateso aliyoyapitia TAL ni zaidi ya MANDELA; makaburu walimuweka ndani kwa muda mrefu lakini hawakumfanyia unyama kama huu. Nawalinganisha waujaji hawa wa Tanzania kuwa ni zaidi ya makaburu wa Afrika Kusini.Mh. Lissu narudia tena Mungu lazima ajilipize kisasi juu yako, labda km siku hizi aoni aisei..
Sent using Jamii Forums mobile app
Inaumiza sana kwakweli!Imenitoa machozi...TL kama binadamu anaweza kuwa ana mapungufu yake,lakini hakustahili unyama huu.Miaka 20 iliyopita,wakati wengine wakiwa hawajaingia kwenye siasa,TL alikuwa Bulyahulu kuwatetea wananchi walibomolewa nyumba zao na Serikali ili kumpisha muwekezaji,walihamishwa kinyama bila fidia wala chochote.
Wakati akiyafanya haya,serikali ilimuita mchochezi na kumfungulia kesi kibao.Aliwatetea raia wa Nyamongo kando ya Mgodi wa North Mara bila hata kulipwa senti,zaidi ya vijana 200 walikuwa wamefungwa jela kwa kesi za kubambikiwa kwa ushirika wa DC wa Tarime na Mgodi wa North Mara.TL alifunga safari toka Dsm mpaka Tarime,aliwatetea bureee na wote wakatoka.Huyu hakustahili adhabu hii ambayo watesi wake wamemchagulia.
Wakati TL akiwa peke yake,akipambana kwa vifungu vya sheria za nchi na za kimataifa dhidi ya ubabe na uonevu wa wananchi kutoka kwa wawekezaji wa Migodi,hao wanaomuita "msaliti" walikuwa busy bungeni kupitisha sheria ambazo leo wao ndio wanaziona za kinyonyaji.
Mungu atakupa nguvu mnyampaa Tundu Lissu,utarudi tena katika pumzi na uhai wako,kama Mungu alivyomuokoa Daniel katikati la Simba wenye njaa,ndivyo atakavyotenda kwako,katikati ya watesi watakaolipwa hapahap duniani.
Ni kwanini Mungu umeyaruhusu haya kwa TL?Ni wapi alipokosea zaidi ya sisi wengine na kustahili unyama huu?Lakini wewe Mungu mwenye haki ulinena,ya kwamba hautatuacha kamwe,na wala hautaweza kutupa majaribu yashindayo imani zetu.Jaribu hili kwa TL,linaonyesha uimara na imani yake kubwa kwako.Tenda Mungu,tenda ewe mwenye haki,tenda sawasawa na fadhila zako
Upone haraka TL
Ni position ya miguu tu!! Inawezekana wa kulia alinyoosha wa kushoto kakunja!! Pale wa kulia ulipokuwa ndipo risasi nyingi zikamiminikia hapo. Au vice versa lakini kikubwa miguu inaonekana haikukaa sawa, aliipishanisha na ulipokuwa wa kulia ndipo palishambuliwa zaidi!!
Kumbe kubenea yupo sahihi kuliko ndugai?
Kumbe sio risasi tano tu!
Yule "Chizi" wa Dodoma analazimisha ziwe tano tuu,kiasi cha kutaka kumsulubu Kubenea kwa kusema risasi zilikuws nyingi zaidi ya hizo tano zake
KWA HYO KUBENEA KAONGEA UKWELI KUWA NI RISAS ZAID YA 38. NGUGAI KADANGANYA BUNGE
GET WELL SOON TUNDU LISSU
32 + 8= 40
Nduguai Vs Kubenea, ngoma mbichi ila mshindi ni dhahiri.
Kama haujashuhudia kitu ni bora ukanyamaza ndugu, hali iliyopo ni mbaya sana na kiuhalisia mguu wake mmoja umesagika na inawezekana hata kuunga ikawa ni kazi ngumu sana, hivyo usiandike kwa kuwa tu umeonyeshwa kufurahia kwa kilichofanyika. Tambua siku zote Mungu ulipa hapa hapa na inawezekana hata wewe unayeshabikia ujinga huu ukapata hukumu stahiki kwa unyama huu uliofanyika.Risasi mbili zivunje mguu zaidi ya mara 5 basi Ana matatz ya mifupa.. dogo alopogwa risasi faya ya mguu na police kavunjika mara moja na ile risasi ni ya smg pia..
au wanaongeza chumvi watoa taarifa maana mfupa ni tafauti na kioo jamn
Ni kweli; tena yuko kwenye kiti anazunguka na kunywa juisi akiona nge tu anakimbia kuogopa kuumwa na kufa lakini yeye amesababisha binadamu mwenzake kumiminiwa risasi ili afe.Kuna watu wameamua kuchagua kukaa upande wa shetani na kujiondolea hofu ya Mungu mioyoni mwao, madaraka yamewalevya wapo tayari kumwaga damu kisa hawataki kukosolewa.
Eee Mwenyezi Mungu mpiganie Mpendwa wetu Lissu na pigana juu ya watesi wake.