Hivi ndivyo nilivyoelewa kuhusu Richmond na Escrow

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,304
12,965
Wakati wa mjadala mkali wa kashfa ya Richmond bungeni, huku tume iliyochunguza kashfa hiyo ikibanwa kuwa haikutoa nafasi kwa watuhumiwa hasa Lowassa kujitetea, aliibuka mwenyekiti wa tume ile Mh. Mwakyembe na kusema kuwa kama watu hawaridhiki waombe kanuni zitenguliwe ili aweze kuwasilisha upya ripoti yake ili aweze kusema hata siri waliyoificha ili kuikoa serikali isiporomoke yote.


Kwa maneno hayo mimi nilliewa kuwa kumbe tume ile iliwasilisha ukweli nusu na hivyo kumtoa kafara Lowassa na mawaziri wawili ili kumwokoa rais ambaye kwa maneno ya Mwakyembe kama wangeyasema yote, ingesababisha serikali yote kuporomoka. Kwa ufupi nilivyoelewa ni kuwa taarifa ile ilikuwa inamgusa rais moja kwa moja na kwa maana hiyo alipaswa kuondolewa madarakani lakini akaokolewa na tume kwa kuficha siri. Hivyo kilichofanyika ilikuwa ni kukivunja kichwa (Lowassa) kwa kosa lililofanywa na ulimi (rais). Na ndio maana katika kikao kimojawapo cha chama Lowassa alimuhoji mwenyekiti kuwa ni jambo gani ambalo yeye aililifanya ambalo yeye hakujua au kumtuma?


Hivi majuzi kamati ya bunge ya hesabu za serikali iiwasilisha bungeni taarifa kuhusiana na akaunti ya Esrow. Ndani yake ilipendekezwa kuwajibishwa na kushitakiwa kwa viongozi mbali mbali wakiwamo mawaziri na Waziri mkuu. Lakini kamati hii nayo ilifanya kama ile ya Mwakyembe. Wakati wa kuwasilisha taarifa yake, Deo Filikunjombe akiwa anasoma baada ya kumpokea Zitto alinukuu kitabu cha Mwl Nyerere ambapo alisema "… mnaweza kumwondoa waziri mkuu na nchi ikabaki imara lakini hamwezi kumwendoa rais bila nchi kuyumba…" Kwa maelezo yake alisema kama rais akiondolewa nchi itayumba lakini sio waziri mkuu. Hivyo wakapendekeza waziri mkuu naye awe miongoni mwa watakaowajibishwa.


Kwa maelezo hayo ni wazi kamati iligundua uhusika wa ikulu katika sakata zima la Escrow hivyo moja kwa moja kumgusa rais. Ilionesha wazi jinsi ikulu ilivyoshiriki katika mchakato mzima wa kutoa fedha za Escrow na jinsi baadhi ya maofisa wa ikulu walivyopokea mgano wao. Hivyo kwa sisi wengine wenye akili ‘fupi' tulichoelewa kutokana na nukuu ile ni kuwa rais naye alipaswa kuwajibishwa au kuondolewa lakini alikolewa na kamati kupitia maoni ya Mwl Nyerere yaliyonukuliwa na kamati kutoka katika kitabu cha "Uongozi wetu na hatima ya Tanzania" cha baba wa Taifa Mwl Nyerere.


Baada ya kuwasilisha taarifa zao tume zote hutoa mapendekezo ya utekelezaji ambayo serikali kwa maana ya rais ndiye anayepaswa kutekeleza. Kinachotokea ni kuwa mapendekezo yote ya kamati za bunge huwa hayatekelezwi yote au kwa ukamilifu kwakuwa anayepelekewa kutekeza ndiye alipaswa kwanza kuwajibishwa. Hivyo anapelekewa kutekeleza maamuzi ambayo yanamgusa yeye moja kwa moja pamoja na washirika wake ambao anaweza kuwa aliwatuma au wao walimtumia yeye. Na kutokana na hilo ndipo tumeshuhudia utekelezaji wa maazimio ya kashfa ya Richmond mengi kukwamba ingawa yaliwazoa waziri mkuu na mawaziri wawili lakini wahusika wengine waliachwa mpaka wastaafu. Tumeshuhudia pia kutotekelezwa kwa maazimio juu ya katibu mkuu wa wizara ya nishati bwana Jairo wakati ule. Na sasa tunashuhudia kukwama kwa utekelezaji wa maazimio mengi ya bunge katika sakata la Escrow kwa kuwa baadhi ya wahusika walionufaika na pesa hizo wapo ikulu. Kwa sisi wenye akili ‘fupi' tunaweza tukaconclude kuwa wale wa ikulu hawawezi kuadhibiwa kwakua zile walizopata katika mgano hazikuwa zao bali walichukua kwa niaba yake. Tutakuwa tumekosea wapi


Hivyo mitindo inayotumiwa na kamati za uchunguzi zakashfa mbali mbali za kuficha siri za wahusika wakuu au kuogopa kuchukua hatua kutokana na nukuu za Nyerere ndio itakayosababisha nchi iendelee kuwa na kashfa baada ya kashfa kwa kuwa tume zinajitahidi kukata matawi badala ya kung'oa shina na mizizi yake.


Nakumbuka mbunge mmoja alitoa hoja bungeni kuwa bunge limekuwa likitoa maazimio ya utekelezaji lakini mara nyingi yamekuwa hayatekelezwi na akataka bunge litoe msimamo itakuwaje endapo maazimio waliyopendekeza hayatatekelezwa tena kama yale ya Richmond bunge lichukue hatua gani? Hoja hii ilifinyangwa kijanja na spika kwakuwa alijua wanampelekea mtuhumiwa kutekeleza maazimo yanayomgusa moja kwa moja. Maokeo yake tumeyaona. Amesema pesa hazikuwa za umma. Wakati wa EPA alisema pia kuwa hazikuwa za serikali ila zilikuwa zinazagaa zagaa pale benki kuu ndipo wajanja wakazichukua.


Mimi nilivyoelewa kuhusu hiyo akaunti ya Esrow ni kuwa pesa zile ni za Tanesco ambazo ziliwekwa pale ili kusubiri mgogoro baina yakena mdai usuluhishwe ili kama kutakuwa hakuna tatizo ndipo zile pesa zilipwe kwa IPTL. Kwa maana hiyo kwakuwa msuluhishi alikuwa hajaamua mgogoro ule zile pesa zilikuwa ni za Tanesco kwa maana ya kuwa Tanesco hakumlipa mdai wake kwa kuwa mahakama haikusema kuwa zile pesa sasa zilipwe IPTL na kwa maana hiyo Tanesco mpaka sasa hawana risiti ya malipo ya pesa zile kutoka IPTL. Sasa zilitolewaje wakati mgogoro haujamalizwa??!! Pesa zile ni za Tanesco na Tanesco ni shirika la umma hivyo pesa zile ni za umma ambazo kisheria zilikuwa zinasubiri kutatuliwa kwa mgogoro kisha zote zilipwe IPTL au zingine zirudi Tanesco.
 
Jistori reeeeefu, halina kichwa wala miguu.

Umechelewa jamvini karamu imeshaliwa.

Siwezi kuamini kuwa wewe ni mwanamke na kama ni kweli lazima umeshaathirika kisaikolojia, hata kama utakuwa unatetea aidha ajira au maslahi binafsi, ni bora angalau kutumia soft language, haya madhara usishangae ukyaambukiza na kudhuru family yako binafsi,,, am very sorry kama nimekuudhi nisamehe bure, hasa ukiangalia mleta mada na jamii kwa ujumla walivyo nyanyaswa mioyo yao kuhusu swala husika.
 
Tulimumu una hasira za bure kwani unaelewa hizo pesa Tanesco alitakiwa amlipe IPTL kwa kupewa umeme ambao Wananchi wa Tanzania tumeutumia kiuhalali kabisa bila mgawo,
Sasa shida yako na hasira ni ipi?
  • Shareholder wa IPTL /PAP & SIMBA kuchukua chao?
  • Ni nani kaibiwa km Tanesco mwenyewe wanajua ni halali hizo hela walizotoa na bado wanadaiwa na hata leo na kesho wanalipia hiyo Capacity charge (kwani kuna Bodi mpya kwanini usiwaambie wagome kulipa hizo 100megawatt za Tegeta Escrow)
  • Acha hasira tafuta mbadala wa kuzalisha umeme tuachane na IPTL /PAP, ufufue mabwawa yetu
  • Mshauri na peoples power aelewe chanzo cha kuibiwa na wajanja wabunifu wa umeme kwani hakuna madala wa nishati ingine takaachana na hao anaowaita mabwanyeye kwani wamechukua chao halali hata miaka ingepita hiyo hela wangeichukua tu na wanaikamua bado
  • Jiulize wamiliki wa IPTL ni kina nani na kwanini hawataifishiwi mitambo?
Mimi nilivyoelewa kuhusu hiyo akaunti ya Esrow ni kuwa pesa zile ni za Tanesco ambazo ziliwekwa pale ili kusubiri mgogoro baina yakena mdai usuluhishwe ili kama kutakuwa hakuna tatizo ndipo zile pesa zilipwe kwa IPTL. Kwa maana hiyo kwakuwa msuluhishi alikuwa hajaamua mgogoro ule zile pesa zilikuwa ni za Tanesco kwa maana ya kuwa Tanesco hakumlipa mdai wake kwa kuwa mahakama haikusema kuwa zile pesa sasa zilipwe IPTL na kwa maana hiyo Tanesco mpaka sasa hawana risiti ya malipo ya pesa zile kutoka IPTL. Sasa zilitolewaje wakati mgogoro haujamalizwa??!! Pesa zile ni za Tanesco na Tanesco ni shirika la umma hivyo pesa zile ni za umma ambazo kisheria zilikuwa zinasubiri kutatuliwa kwa mgogoro kisha zote zilipwe IPTL au zingine zirudi Tanesco.
 
Last edited by a moderator:
Mimi binafsi katika swala Zima la escrow sijaelewa sehemu moja, kwenye akaunti kulikuwa na fedha za tanesco na iptl, Kuna fedha za tanesco kwa kuwa tanesco wanalipishwa zaidi na inavyostahili, sasa hicho kiasi cha zaidi wanachotozwa tanesco Ni shilingi ngapi? Au tanesco wanakisia shilingi ngapi wanaidai iptl kutokana na kulipishwa zaidi, na kiasi gani kilichobakia Ni cha iptl, kwa kuwa kile kiasi ambacho tanesco walikuwa wanaidai iptl ndicho ambacho Ni fedha za wananchi na ndio tunaweza kusema zimeibiwa, na zilizo za iptl atakuwa amechukua mwenyewe, sasa mbona kwenye taarifa nyingi zinasema fedha zote za kwenye akaunti Ni za tanesco, ikiwa na maana kuwa iptl hana hata shilingi, ikiwa na maana fedha zote zile zaidi ya billion 300 Ni za tanesco, sasa kwenye akaunti hii zilifata nini? Au zililetwa ili ziibiwe.
 
Jistori reeeeefu, halina kichwa wala miguu.

Umechelewa jamvini karamu imeshaliwa.
Uko "sahihi" na hii inawezekana only in Tz because Tanzania is the greatest nation in the world! Every thing is possible!
 
Tulimumu una hasira za bure kwani unaelewa hizo pesa Tanesco alitakiwa amlipe IPTL kwa kupewa umeme ambao Wananchi wa Tanzania tumeutumia kiuhalali kabisa bila mgawo,
Sasa shida yako na hasira ni ipi?
  • Shareholder wa IPTL /PAP & SIMBA kuchukua chao?
  • Ni nani kaibiwa km Tanesco mwenyewe wanajua ni halali hizo hela walizotoa na bado wanadaiwa na hata leo na kesho wanalipia hiyo Capacity charge (kwani kuna Bodi mpya kwanini usiwaambie wagome kulipa hizo 100megawatt za Tegeta Escrow)
  • Acha hasira tafuta mbadala wa kuzalisha umeme tuachane na IPTL /PAP, ufufue mabwawa yetu
  • Mshauri na peoples power aelewe chanzo cha kuibiwa na wajanja wabunifu wa umeme kwani hakuna madala wa nishati ingine takaachana na hao anaowaita mabwanyeye kwani wamechukua chao halali hata miaka ingepita hiyo hela wangeichukua tu na wanaikamua bado
  • Jiulize wamiliki wa IPTL ni kina nani na kwanini hawataifishiwi mitambo?
Nimeeleza mtizamo wangu. Kama kutakuwa na mwananchi atakaye kuwa hachukizwi na hayo yanayotokea kupitia EPA,Richmond, Escrow nk basi huyo lazima awe mmoja wa wanufaika na ufisadi huo
 
Mimi binafsi katika swala Zima la escrow sijaelewa sehemu moja, kwenye akaunti kulikuwa na fedha za tanesco na iptl, Kuna fedha za tanesco kwa kuwa tanesco wanalipishwa zaidi na inavyostahili, sasa hicho kiasi cha zaidi wanachotozwa tanesco Ni shilingi ngapi? Au tanesco wanakisia shilingi ngapi wanaidai iptl kutokana na kulipishwa zaidi, na kiasi gani kilichobakia Ni cha iptl, kwa kuwa kile kiasi ambacho tanesco walikuwa wanaidai iptl ndicho ambacho Ni fedha za wananchi na ndio tunaweza kusema zimeibiwa, na zilizo za iptl atakuwa amechukua mwenyewe, sasa mbona kwenye taarifa nyingi zinasema fedha zote za kwenye akaunti Ni za tanesco, ikiwa na maana kuwa iptl hana hata shilingi, ikiwa na maana fedha zote zile zaidi ya billion 300 Ni za tanesco, sasa kwenye akaunti hii zilifata nini? Au zililetwa ili ziibiwe.

Hilo swali lako wote wamelikwepa, usitegemee majibu.
 
Nimeeleza mtizamo wangu. Kama kutakuwa na mwananchi atakaye kuwa hachukizwi na hayo yanayotokea kupitia EPA,Richmond, Escrow nk basi huyo lazima awe mmoja wa wanufaika na ufisadi huo


Wewe jibu uliyoulizwa, usirukie kutafuta msaada kwa kucheza na akili za misukule. Wengine hatununuliki, si kwa fedha si kwa uongo wa kucheza na emotions zetu.

Mimi nakuuliza jingine, mlitaka umeme wa bure?
 
Wewe jibu uliyoulizwa, usirukie kutafuta msaada kwa kucheza na akili za misukule. Wengine hatununuliki, si kwa fedha si kwa uongo wa kucheza na emotions zetu.
Mimi nakuuliza jingine, mlitaka umeme wa bure?
Nimeeleza mtizamo wangu. Kama kutakuwa na mwananchi atakaye kuwa hachukizwi na hayo yanayotokea kupitia EPA,Richmond, Escrow nk basi huyo lazima awe mmoja wa wanufaika na ufisadi huo
Faiza huyu Tulimumu ana yake yaani analeta hasira na uongo wa kutungwa na kina Zitto na Kafulila uonekane km ukweli kuwa hela zimeibiwa.
mwenye hela ni Tanesco amalipa gharama za umeme na mwenye hela ameshazichukua yeye anataka aingie mifyukoni mwa watu na kuzichunguza.
Mwenye kudaiwa leo mpaka kesho ni Tanesco amenyamaza na anaendelea kulipa tangu 2006 licha ya kushtaki na kulalamika kuwa ghrama ni kubwa , akaambiwe akaziweke hizo hela za huyo IPTL huko ESCROW
sasa mtasemaje ni mali ya serikali
  • km ni Kodi TRA watalipwa na PAP kwani wapo na wanaendelea kuzalisha umeme 100mw toka Tegeta
Ok wasioelewa sasa waksirike tu, na uamuzi wowote chukueni maana majungu yamezidi na Wahisani wamefungulia misaada yao tayari
 
Jistori reeeeefu, halina kichwa wala miguu.

Umechelewa jamvini karamu imeshaliwa.

Siku zote jamii tawala haitakiwi kusahau kuwa chochote wanachomiliki ni mali ya raia wanaofanya kazi kwenye mashamba ya vibwenyenye, migodi ya makaburu, mashuleni, wamachinga, wabwia unga, madaktari manesi na raia wote wasiona ajira za kusemeka. Kundi la watawala wanapotumia hovyo mali za nchi huibua hasira za wanaohangaika kuzisaka mali hizo(wananchi). Iambie serikali yako na wewe mnaamsha hasira za wananchi.

Tanesco ni shirika la umma si mali ya rais wala waziri yeyote kwakuwa yawezekana hachangii lolote kwenye uendeshwaji wa shirika hili. Kodi kwenye Mshahara wa mwalimu hukatwa ili Tanesco na mashirika mengine ya serikali yapate nayo mgao wake. Huwezi tenganisha jasho la mwalimu na pesa za Tanesco hata siku moja, ni dhambi iliyoje kudanganya umma kuwa pesa zile hazina utata hata kidogo. Sidhani kama kuna raia mpumbavu ama mtumba kiasi cha kufikia kusema hilo. Kesi ya mahakamani ni juu ya utata katika kiasi kinacholipwa na Tanesco inayoendeshwa kwa jasho la watanzania. Pesa yeyote ya Tanesco ni mali ya mtumiaji wa umeme anayeilipa Tanesco, ni mali ya mtu aliyeenda dukani na kununua bidhaa iliyokatwa kodi ili tanesco iendelee kutoa huduma, ni pesa ya wale wanaokatwa kodi mishahara yao ili tanesco ilipe mabosi wake Mshahara. Huwezi kusema pesa ambayo tanesco iliilalamikia si ya watanzania.

Ni udhaifu kudai kuna watu wanapandikiza chuki kwa kuongelea jambo hili kwa watanzania wasiojua kuwa tanesco wanayoiendesha ina kesi na mtu anayewanyonya kwa miaka kadhaa sasa na wametumia mabilioni kuendesha kesi hii.

Ifike wakati na nyinyi muelewe lengo la kuwa na raisi katika nchi. Si kutetea ujinga na kuficha uchafu wa chama, yule ni mtumishi wa maskini. Mjie kuwa kila tonge mnalomega kwenye mali ya wananchi ni zao la wamachinga wanaopigwa na mgambo, makonda wa daladala tunaoitwa wahuni......
 
Siku zote jamii tawala haitakiwi kusahau kuwa chochote wanachomiliki ni mali ya raia wanaofanya kazi kwenye mashamba ya vibwenyenye, migodi ya makaburu, mashuleni, wamachinga, wabwia unga, madaktari manesi na raia wote wasiona ajira za kusemeka. Kundi la watawala wanapotumia hovyo mali za nchi huibua hasira za wanaohangaika kuzisaka mali hizo(wananchi). Iambie serikali yako na wewe mnaamsha hasira za wananchi.

Tanesco ni shirika la umma si mali ya rais wala waziri yeyote kwakuwa yawezekana hachangii lolote kwenye uendeshwaji wa shirika hili. Kodi kwenye Mshahara wa mwalimu hukatwa ili Tanesco na mashirika mengine ya serikali yapate nayo mgao wake. Huwezi tenganisha jasho la mwalimu na pesa za Tanesco hata siku moja, ni dhambi iliyoje kudanganya umma kuwa pesa zile hazina utata hata kidogo. Sidhani kama kuna raia mpumbavu ama mtumba kiasi cha kufikia kusema hilo. Kesi ya mahakamani ni juu ya utata katika kiasi kinacholipwa na Tanesco inayoendeshwa kwa jasho la watanzania. Pesa yeyote ya Tanesco ni mali ya mtumiaji wa umeme anayeilipa Tanesco, ni mali ya mtu aliyeenda dukani na kununua bidhaa iliyokatwa kodi ili tanesco iendelee kutoa huduma, ni pesa ya wale wanaokatwa kodi mishahara yao ili tanesco ilipe mabosi wake Mshahara. Huwezi kusema pesa ambayo tanesco iliilalamikia si ya watanzania.

Ni udhaifu kudai kuna watu wanapandikiza chuki kwa kuongelea jambo hili kwa watanzania wasiojua kuwa tanesco wanayoiendesha ina kesi na mtu anayewanyonya kwa miaka kadhaa sasa na wametumia mabilioni kuendesha kesi hii.

Ifike wakati na nyinyi muelewe lengo la kuwa na raisi katika nchi. Si kutetea ujinga na kuficha uchafu wa chama, yule ni mtumishi wa maskini. Mjie kuwa kila tonge mnalomega kwenye mali ya wananchi ni zao la wamachinga wanaopigwa na mgambo, makonda wa daladala tunaoitwa wahuni......

Wewe unaandika miji habari mireeefu, ambayo ungeweza kuielezea kwa sentensi mbili tatu tu. Unanikumbusha Mkandara

Fupisha tukusome vizuri.

Hao woooote uliowataja ndiyo waliowaweka madarakani wanaoongoza nchi kwa sasa kwa kuwapigia kura. Usisahau hilo.
 
Back
Top Bottom