barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,726
- 32,818
Hivi ndivyo mmiliki wa Slipway Hotel na kampuni zake nyingine ikiwemo kampuni ya ndege ya Coastal Aviation ndugu Nicola Colangelo alivyoagwa na wafanyakazi wake.
Toka Hotel ya Slipway mpaka viunga vya Ras Kutani-Kigamboni,Camps za Watalii katika pori la Selous na Hotel zake kule visiwa vya Mafia ilikuwa ni majonzi matupu.
Mtoni Marine Zanzibar mpaka CSI na maeneo yote alipokuwa amewekeza,ilikuwa ni vilio na kwikwi za huzuni.Wafanyakazi wake wote katika maeneo yote aliyowekeza,walitenga muda wa kukaa kimya na kufuatilia habari za mazishi yake huko kwao Italia.
Ilikuwa ni siku ya huzuni,katika picha wapo wazee walioanza kufanya kazi na Nicola akiwa hana utajili mkubwa.Hakuwahi kuwaacha eti kwa sababu amejenga hoteli kubwa ya kitalii na wao hawakuwa na elimu kubwa ya kuhudumia utalii,Nicola alienda nao,na leo ametangulia mbele za haki na wao wamebaki.
Kuna wapishi wake walioanza kumpikia chakula binafsi toka miaka ya 1970's wakiwa mabinti wadogo,mpaka leo ni wabibi lakini alikuwa nao pamoja.
Picha hizi ni muunganiko wa matukio,katika hotel ya Slipway,Uwanja wa ndege wa JNIA eneo la Terminal One zilipo ndege zake,Mafia na Selous.
Hivi ndivyo,Nicola alivyoagwa,mtu wa watu na mlowezi aliyewekeza kwa wazawa kwa moyo mmoja.
Pumzika kwa Amani Nicola.