Hivi ndivyo majasusi ya Kirusi yalivyokuwa yakidukua mazungumzo ya ubalozi wa Marekani kwa ufundi wa hali ya juu

Konzo Ikweta

JF-Expert Member
Oct 3, 2013
735
1,464
Mnamo mwaka 1946, kundi dogo la wanafunzi watoto wa shule wa nchini Urusi kutoka katika kikundi kidogo kilichojulikana kama "Vladimir Lenin All-Union Pioneer Organization (wapo kama vijana flani hivi wa skauti wa hapa Bongo) walimpatia zawadi ya nembo ya taifa la marekani (kama huku kwetu Tanzania ni ile nembo yetu ya bibi na bwana) ndugu Avarell Harriman, aliyepata kuwa balozi wa Marekani nchini Urusi (USSR)

Ile zawadi, kama ishara ya urafiki mwema wa urusi kwa marekani ambaye alikuwa ni mshirika wake mkuu katika vita ya pili ya dunia, ilikuja kuning'inizwa katika eneo maalum la makazi ya balozi huyo yaliyokuwapo katika jiji kuu la Moscow.

Nembo ile ya taifa la marekani iliendelea kuning'inia pale ukutani kwa kwenye makazi ya balozi kwa muda wa miaka saba (7), mpaka kwa bahati mbaya wataalam kutoka wizara ya mambo ya nje (bila shaka ni maofisa wa CIA) walipokuja kugundua kumbe ile zawadi ilikuwa ni zaidi ya urembo wa ukutani.

Mara paaaaaap, kumbe ilikuwa ni kifaa cha kunasia mazungumzo (bugging device)........!!!!!.


Warusi waliunda kifaa cha kusikilizia mazungumzo kwa siri sana (bug), ambacho makachero wa kupambana na wapelelezi wa nchi hasimu (counterintelligence unit) wa Marekani walikitunga jina na kukiita (The Thing).

Kifaa kile kilifichwa kwa usiri sana ndani ya nembo ya taifa la Marekani na kimekuwa kikisikiliza mazungumzo ya balozi Harriman pamoja na mabalozi wote waliomfuata kwa kipindi chote ambacho kifaa kile kilikuwa kinaning'inia mule ndani.

Balozi yule alikiri kwa kusema ya kuwa Ilidhihirisha siku ile kumbe USSR ilikuwa na wataalam wa kutisha sana wa masuala ya electronics.

Balozi alisema ya kuwa sasa ninaamini ya kwamba kwa ugunduzi huu utaalam mzima wa serikali kusikilizana siri umefikia viwango vya hali ya juu sana vya technology.

Wanadiplomasia pamoja na wamarekani wengine waliokuwa wakifanya kazi katika ubalozi wao pale USSR walikwisha amini zamani hata kabla ya kuwa kuta zote zilizopo jiji la Moscow "zina masikio"

Aliyewahi kuwa rais wa marekani kwa miaka ya zamani sana bwana James Buchanan aliwahi kisema ya kwamba mara zote wanadiplomasia wetu huzungukwa na mashushushu wenye taaluma zote kubwa na ndogo, na ni mara chache sana tunaweza kukodisha ama kuajiri mtumishi wa ndani ambaye sio informer wa polisi.

Mwanzoni mwa karne ya 20, ujasusi kwa njia za kibinadamu pamoja na usikilizaji wa mazungumzo ulijawa na technology mpya ya nyaja pamoja na vifaa vidogo vya kusikilizia na kurekodia mazungumzo.

Wageni wote waliokuwa wakiingia katika nyumba ya makazi ya balozi walikuwa wakipewa kadi punde tu wanapowasili wakitahadharishwa ya kuwa nyumba vyote pamoja na bustani ndani ya eneo lile vilikuwa vinapelelezwa kwa ukaribu sana na makachero wa KGB.


Hiki kifaa kiliundwa na bwana Termen, ambaye alipata kuishi nchini Marekani kwa kipindi kirefu kidogo kisha akaja kurudi Urusi kabla ya vita ya pili ya dunia.

Baada ya kuwasili Russia, bwana theremin alipelekwa moja kwa moja katika chuo cha siri chenye maabara kisha kupewa jukumu la kuunda na kuja na njia ya kitaalam ya namna na kusikilizia mazungumzo ya nyumbani kwa balozi wa Marekani nchini Russia.

Kifaa alichofanikiwa kuunda mtaalamu huyo kilikuwa na antenna pamoja na cylinder pamoja na waya mdogo sana uliotumika kama microphone. Majasusi wa KGB waliokuwa wanazurura maeneo ya mtaa huo ambapo kuna makazi ya balozi wa marekani, walikuwa na uwezo wa kuwasha hicho kifaa kwa remote maalum inayotumia mawimbi ya radio.

Sasa pale ambapo balozi ama mtu mwingine yeyote aliyepo chumbani akiongea, yale mawimbi ya sauti yalikuwa nayawaendea moja kwa moja vijana wa KGB na kuweza kusikiliza mazungumzo mazima.

Maajabu ya hicho kifaa ni katika udogo wake. Kilikuwa ni kidogo mno. Tena saaaanaa aiseee. Kilikuwa hakitumii chanzo chochote cha umeme wali betri, hakukuwa na nyaya ambazo zingeweza kugundulika wala betri za kubadilisha na kiliweza kifanya kazi pindi tu KGB wakikiwasha kwa remote inayotumia mawimbi ya redio. Laa sivyo kinazimika kiasi kwamba wakaguzi wa CIA wasingeweza kukigundua.

Wizara ya mambo ya nje ya marekani kupitia wataalam wake wa kufagia vifaa vya kunasia sauti (bug sweepers) walipatwa na mashaka kwamba KGB waliunda kifaa cha namna hii pale ambapo wataalam wa mawimbi ya radio kutoka jeshi la marekani pamoja na uingereza waliokuwa wanachungua mawasiliano ya USSR bila kutarajia wakajikuta wanakamata mawasiliano ya sauti ya wanadiplomasia wao kwa kutumia vifaa vyao wenyewe.

Matukio ya namna hiyo pamoja na kitendo cha marekani kuruhusu wafanyakazi wa urusi kufanyia marekebisho nyumba ya balozi wao kabla ya kuhamia mwaka 1952, ambapo ndio ili nafasi nzuri kwa KGB kupandikiza vifaa vya kusikilizia, ilipelekea CIA kutuma wataalam wake kupitia wizara ya mambo ya nje kwenda kufagia nyumba nzima (bug sweeping) bila mafanikio.

Walitoka kapa mpaka wakaanza kushuku labda KGB wamebadili mbinu zao za kupandiliza vifaa ama taaluma ya CIA ya kugundua vifaa hivyo ndio imepitwa na wakati.....!!!!!

Baada ya kuona hali si hali, wizara ikaamua kutuma tena wataalam wawili, Ford pamoja na Bezjian, mpaka Moscow kufanya zoezi upya tena kwa kina na umakini zaidi. Bezjian akahisi labda KGB waliondoa kifaa chao kabla zoezi jipya la ukaguzi halijaanza na kisha kupachika tena hali ilipokuwa shwari.

Ili kuwakamata vizuri KGB, akaamua kujifanya kama tu ni mgeni wa balozi Kennan. Vifaa vyake vya kazi vilikuwa vipo tayari na vimefichwa vizuri kabisa hata kabla hajafika na kisha kukaa pale kwa balozi kwa siku kadhaa huku akicheza karata na kuwaangalia kwa umakini wafanyakazi wa nyumba ya balozi wakati huo anatumia muda wa usiku kutafuta kifaa hicho cha kunasia sauti. Lakini safari hii wakachemka tena. Hola. Wakatoka patupu.

Sasa jioni moja wakati balozi yupo kwenye chumba chake hicho akiwa anasoma kwa sauti ya chini kidogo baadhi ya nyaraka zake za siri wakati wataalam wa CIA bwana Ford na Bezjian wakiwa wanazunguka nje ya nyumba wakiwa na vifaa vyao vya detection, ghafla Bezjian akafanikiwa kukamata sauti ya bwana Kennan kwenye receiver yake na kisha taratiiibu kabisa akaamua kuifuatilia ile signal mpaka chanzo chake inapotokea.

Bezjian akaenda katika chumba cha kusomea na kumwambia Kennan kwa ishara kwa aendelee kusoma kwa sauti zaidi kwa maana kuna signal ameikamata. Ile signal iliyokuwa na sauti ya Kennan ilionekana inatokea katika kuta nyuma ya ile "zawadi aliyopewa balozi.

Bezjian akaondoa ile zawadi kutoka ukutani kisha kwa kutumia nyundo akaanza kupasua ukuta ambapo ile zawadi ilikuwa imetundikwa. Wakati anabomoa ukuta signal ikapotea ghafla.

Bezjian ndipo machale yakamcheza kuwa kile kifaa cha sauti hakikuwa katika ukuta, bali kilikuwa ndani ya ile zawadi ya balozi na kisha kuamua kuvunja ile zawadi kwa kutumia nyundo ile ile.

Ndani ya dakika chache zoezi likakamilika na yule mtaalam wa CIA akakuta ndani ya ile zawadi kulikuwa na kifaa kidogo sana kinachoweza kulingana na penseli.

Kwa usiku wote ule, ofisa wa CIA bwana Bezjian akaamua kulala na kifaa kile chini ya mto wake ili kwamba KGB wasije kukiiba. Kesho yake kifaa kikapelekwa kwenda marekani chaaaaap ili kisomwe na kitengenezwa mbadala wake na idara za usalama za marekani jambo ambalo likawa kama vile ndio chanzo cha mashindano ya silaha baina ya USSR na USA katika kuunda vifaa vya kunasa mawasiliano vya hali ya juu zaidi ili kila mmoja amchunguze mwenzake zaidi.

Kwa miaka mingi sana hii zawadi ya mtego ilining'inizwa juu ya kuta za nyumba ya balozi wa marekani iliyokuwa busy sana na wageni wa aina tofauti tofauti mpaka wale wa levels za juu sana kama General wa jeshi Eisenhower, watumishi wa ikulu ya marekani pamoja na wabunge wengi sana, wakibadilishana taarifa mbali mbali kuhusiana na hali ya usalama na ustawi wa nchi yao.

Mmoja wa watumishi wa KGB ambaye alikuwa anasimamia kifaa kile akaja kukiri baadaye ya kuwa kile kifaa kiliwawezesha kupata taarifa muhimu zilizowezesha USSR kuweza kuwazidi kete wamarekani katika siasa za dunia wakati wa kipindi kigumu cha vita baridi.
 
Pongezi kwako mtoa mada kwa mada nzuri. Kila siku huwa nawahabarisha watu kuwa kiteknolojia achana na Mrusi wao wanasema Mmarekani. Ila iko siku watamjua Mrusi ni nani.
 
Ndio kusema Nape January Mzee Kinana Mzee Makamba Membe walishindwana kbs kujilinda na ili...
 
Back
Top Bottom