Hivi Nchi Nyingine Kuna Hii Kitu?

Hans Miki

Member
May 30, 2017
12
28
Kwa hapa nchini ili uweze kugombea uongozi TFF au katika klabu kadhaa za michezo inabidi uwe una angalau elimu ya kidato cha nne. Cha ajabu ili kugombea ubunge inabidi ujue tu kusoma na kuandika! Viongozi wa klabu, kwa mfano, wanasimamia maslahi ya wanachama wachache tu wakati wabunge wana jukumu la kutunga sheria zinazokuwa na athari hata kwa vizazi vijavyo. Hivi kweli sifa ya kusoma na kuandika inafaa katika hilo?
 
TFF NA BUNGE NI VITU VIWILI TOFAUTI KABISA.AFU MKUU UNATAKA KUANZISHA UCHOCHEZI SIO....hahahahaa
 
Kwa hapa nchini ili uweze kugombea uongozi TFF au katika klabu kadhaa za michezo inabidi uwe una angalau elimu ya kidato cha nne. Cha ajabu ili kugombea ubunge inabidi ujue tu kusoma na kuandika! Viongozi wa klabu, kwa mfano, wanasimamia maslahi ya wanachama wachache tu wakati wabunge wana jukumu la kutunga sheria zinazokuwa na athari hata kwa vizazi vijavyo. Hivi kweli sifa ya kusoma na kuandika inafaa katika hilo?
Usifananishe TFF na nanihii... Soka ni imani ya watu (maana kuna watu ikifungwa timu yake unaweza kudhani amefiwa na wengine wanazimia, watu pia wanaishi kwa kucheza kamari za soka) na nanihii ni kijiwe cha porojo na kusinzia (kwa mujibu/sauti ya bashite)...

Utasikia: haya "wanafiki waseme ndiyo" "ndiiiiyoooooooo!"...
 
Muwakilishi wa wananchi, wananchi wanahaki ya kumchagua yoyote wanaedhani ni sahihi...
Mkwawa na kinjekitile ngwale hawakuwahi kupita hata kindergarten....
Vinginevyo tungetenganisha wawakilishi wa wananchi na watunga sheria wakawa wengine wenye at least degree ya sheria
 
Ukiweka degree kama minimum qualification kwa ubunge utapataje kura za ndio katika kupitisha maazimio? BTW hata kupitihsa hii yenyewe ni kwa azimio sasa akina Bulembo, Msukuma , Kessy na Lusinde watalipisha kweli?
 
Mkuu hivi mazingira ya kina Mkwawa na sasa yanashabihiana kweli?
Yako tofauti lkn pia mtu yoyote anaejua kusoma na kuandika kama akiamua anaweza kuwa na maarifa yoyote anayotaka...
Mfano waziri mkuu mmoja Mstaafu wa Australia. Huyo jamaa alifanya economic reform nyingi lkn hakuwahi kupitia formal education.
Tatizo letu sio degree uvivu wa kusoma na kutafuta taarifa sahihi ni ugonjwa wa wote degree holder na hao wanajua kusoma na kuandika...
 
Ndio ni sahihi hasa pale unapoweka wabunge ambao wapiga kura wao wengi wana elimu ndogo ni sawa na kuwanyanyapaa na wao wakitaka hizo nafasi

Nchi nyingine kama ulaya wameendelea na wamewekeza sana kwenye elimu
Lakini je hii ni tamaduni sahihi kwetu?
 
Back
Top Bottom