Hivi nani competent kati ya Tundu Lissu Vs Peter Kibatala?

Nimetukana wapi?

Wewe si kuna thread Fulani ulidai wewe ni msagaji yaani unafanya mapenzi na wanawake wenzako.

Ndiyo nauliza, ni kwann ukawa msagaji?

mmmnhhh nakumbuka ile thread ulivyonitukana,usinifate fate,hamna thread niliyoleta kuhusu mimi kuwa msagaji,koma!
 
Kweli lisu kichwa,angeshirikishwa masuala ya serikali kuhusu mikataba asaidie,tungwkuwa mbali sana,hata mahakama za nje tulikostakiwa angeenda tuahinde
 
Nitakupa usijali. Nahapo ndipo mbowe alipomtambua lisu kwamara yakwanza nakumpa pick up ili afanye fasta kudeal na kupindua hukumu mahakaman(enzi hizo lisu akiwa Nccr mageuzi. Lakini kule mara alikua katumwa/kaagizwa na Amerika kupitia taasis ya uhifadhi wamazingira TZ.kufatilia nakuandaa ripoti nikweli wananchi wapale wamefukiwa baada ya gvt ya Ben kuwapa wawekezaji ardh ili wachimbe madini(mgodi North mara). Akati vuguvugu linaendelea Wale wapingaji wakiongozwa na chacha wangwe akiwa diwani baadhi walikamatwa pamoja na chacha walifika 40.wakafunguliwa mashitaka ya uhaini. Chacha akagongwa maisha hawa wengine ili 30 kilammoja.. Siku yahukumu chacha alimwambia mbowe (98 alikua Katibu),kwamba kunamtu mwanasheria anaitwa lisu mtafte yupo hapa anakazi maalum atusaidie(kumbuka tayari wameshasomewa),basi kumtafta lisu akampata wakaka nakuongea ila lisu kwambowe aliomba tu msada wa gari kwani ye lisu akiwa kule alikua anatumia baiskeli kwenye maswala yake.kwaufupi ndani ya mwezi mmoja aliwatoa wote chacha nawezake, yote nikwamba lisu aliipindua hukumu ile nawatu kua huru ilikua mahakama kuu kanda yatabora. Rekodi ile haijavunjwa bado.
Naweza kupata hiyo nakala ya kesi uliokua unaelezea tafadhar
 
Mimi ni wakili nimepata fursa ya kufuatilia hawa mawakili wawili kwa karibu sana. Ninachoweza kusema ni kwamba kumlinganisha Tundu Lissu na Peter Kibatala ni sawa na kulinganisha mlima na kichuguu, Lissu ni mlima na Kibatala ni kichuguu. Kibatala is very ordinary lawyer sema tu anajua kujitangaza vizuri sana (good marketing strategies). Kwa wale waliokuwepo mahakama kuu mbele ya majaji 3 kwenye kesi ya Mitaa 200 mwaka 2015 mliona siku jinsi naibu mwanasheria mkuu wa wakati huo Dr. Tulia Akson Mwansasu alivyomtoa jasho Kibatala ambaye alipoteza network kabisa hakawa kama vile hakujiandaa kabisa wakati Dr. Tulia sio legal practitioner bali ni academician lakini alimdhibiti Kibatala kikamilifu. Kibata alishindwa kesi ya Mita 200, Lissu hajawahi kushindwa kesi yoyote ambayo serikali ni mshitaki au mshitakiwa, kila mtu anajua jinsi Lissu alivyoigalagaza Serikali mahakamani kwenye kesi ya ugaidi dhidi ya Lwakatare na Ludovick Rwezaura au kwenye kesi ya uchaguzi ya Lema katika mahakama ya rufaa. Pia kesi Wasira dhidi ya Esther Bulaya kila mtu aliona jinsi Lissu alivyomfanyia kitu kibaya Wasira, Lissu kampiga Wasira mahakama kuu mara mbili na kampiga tena mahakama ya rufaa mpaka Wasira akaamua kustaafu siasa. Tundu Lissu hiyo ni habari nyingine, inaweza kuichukua nchi hii miaka 200 kupata mwanasheria bora kama Lissu. Unaposema top class lawyers wa Tanzania utawataja mawakili kama Lissu, Prof. Kabudi, Prof. Luoga, Magafu, Dr. Kilangi, Masumbuko Lamwai, Dr. Tenga na wengine wachache lakini sio bwana mdogo Peter Kibatala.

Kuna vitu sitaki kuongea kuhusu udhaifu wa Kibatala kwenye tasnia ya sheria maana staki nimvunjie heshima yake.
Mmmm mbona umeharibu tena maoni yako mazuri,kwn lissu hana madhaifu binafsi kisheria? Inaonekana wewe kuna kitu na kibatara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu badilisha headline competent sio neno sahihi kwenye kulinganisha hao wanasheria wawili.
 
Lissu amepigwa risasi zaidi ya 10 na bado yupo hai...kaishinda mahakama ya kifo..
Huyo kibatala akibondwa tu na jiwe moja ataweza kuwa hai kweli..
 
Kuna yule jamaa wa arusha anaitwa albert msando inaonekana naye yupo vizuri sana...
 
Kibatala yupo juu lakini yule jamaa ni mjanja Sana akiona kesi element za kushinda hazipo huwahajihusishi na hiyo kesi angalia mbowe tangu ameruka dhamana kibatala Kawa mpole Sana anajuwa fika mbowe aliharibu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa ni wanasheria nguli wote wanatetea upinzani,

Mi nawapima wanasheria kwa kuangalia yafuatayo
1.Idadi ya kesi alizoshinda
2.Idadi ya maamuzi Tata ya utafasiri wa sheria ambayo kayatatua yakawa mwongozo kwa wengine,
3.Idadi ya wateja reputable aliwatetea kwa crucial cases na kawashinda
4.idadi ya complicated cases ambazo amelegeza kwa kupangua vifungu mpaka zikawa za kawaida

Je kati ya hao wawili nani mkali sana?

Britannica
LISU ni mwasheria aliye egemea siasa na uanaharakati Kibatala is purely practicing lawyer! KIBATALA , sheria is his business yuko juu sana ya Lisu
 
Wote wazur na nafasi zao kama messi na ronaldo


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mimi ni wakili nimepata fursa ya kufuatilia hawa mawakili wawili kwa karibu sana. Ninachoweza kusema ni kwamba kumlinganisha Tundu Lissu na Peter Kibatala ni sawa na kulinganisha mlima na kichuguu, Lissu ni mlima na Kibatala ni kichuguu. Kibatala is very ordinary lawyer sema tu anajua kujitangaza vizuri sana (good marketing strategies). Kwa wale waliokuwepo mahakama kuu mbele ya majaji 3 kwenye kesi ya Mitaa 200 mwaka 2015 mliona siku jinsi naibu mwanasheria mkuu wa wakati huo Dr. Tulia Akson Mwansasu alivyomtoa jasho Kibatala ambaye alipoteza network kabisa hakawa kama vile hakujiandaa kabisa wakati Dr. Tulia sio legal practitioner bali ni academician lakini alimdhibiti Kibatala kikamilifu. Kibata alishindwa kesi ya Mita 200, Lissu hajawahi kushindwa kesi yoyote ambayo serikali ni mshitaki au mshitakiwa, kila mtu anajua jinsi Lissu alivyoigalagaza Serikali mahakamani kwenye kesi ya ugaidi dhidi ya Lwakatare na Ludovick Rwezaura au kwenye kesi ya uchaguzi ya Lema katika mahakama ya rufaa. Pia kesi Wasira dhidi ya Esther Bulaya kila mtu aliona jinsi Lissu alivyomfanyia kitu kibaya Wasira, Lissu kampiga Wasira mahakama kuu mara mbili na kampiga tena mahakama ya rufaa mpaka Wasira akaamua kustaafu siasa. Tundu Lissu hiyo ni habari nyingine, inaweza kuichukua nchi hii miaka 200 kupata mwanasheria bora kama Lissu. Unaposema top class lawyers wa Tanzania utawataja mawakili kama Lissu, Prof. Kabudi, Prof. Luoga, Magafu, Dr. Kilangi, Masumbuko Lamwai, Dr. Tenga na wengine wachache lakini sio bwana mdogo Peter Kibatala.

Kuna vitu sitaki kuongea kuhusu udhaifu wa Kibatala kwenye tasnia ya sheria maana staki nimvunjie heshima yake.
Wakili msomi tafadhali share uzoefu wako kwa mawakili hawa; Majura Magafu, Rugemeleza Nshala, Richard Rweyongeza, Alex Mgongolwa, Prof Shaidi na Dr Ringo Tenga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom