Kaduguda
JF-Expert Member
- Aug 1, 2008
- 724
- 641
Watanzania wenzangu, nimekuwa nikjiuliza sana bila majibu ya uhakika. Hivi kwa nini ili nipate kazi ndani ya nchi yangu ambayo tumejihalalishia kwamba Kiswahili ni lugha yetu ya Taifa mpaka niandike barua ya kuomba kazi kwa lugha ya kiingereza? Halafu ukienda kwenye usaili haohao waliokwambia uandike barua bado hata kiingereza chenyewe kinawasumbua na matokeo ni usaili huo kufanyika kwa Kiswahili. Ilikuwa na maana gani basi kuandika hiyo barua kwa kiingereza, kwa nini isiwe Kiswahili tu? Kwani kuandika kiingereza ndo kigezo cha kupat kazi?
Naomba tusaidiane hapa kama kuna umuhimu wa kunganganizana kutumia kiingereza hata kwa kazi ambazo hiyo lugha haitumiki kabisa. Mfano, mimi Afisa wa kutoza kodi chini ya halmashauri fulani, kila siku niko minadani na huko ni Kiswahili na lugha za wenyeji wangu ndo zinatumika kwa sana lakini wakati wa kutafuta kazi naambiwa niandike barua kwa kiingereza sasa huu sio utumwa ndugu zangu? Matokeo yake nilichokiona kwa ndugu zangu wengi ni kila barua kuwa na mfanano wa namna fulani yaani utakuta tofauti ni jina tu lakini asilimia kubwa ya maneno ni yaleyale kwa kila barua ya mwombaji. Tufanye nini ili kuondokana na jinamizi hili la utumwa wa lugha?
Nimeona kwenye nchi za wenzetu, kujua kiingereza sio tija sana. Na hata waombapo kazi hiyo lugha sio ya lazima na haswa kama hiyo kazi haitahusisha mawasiliano ya kimataifa. Kwangu naona kungangania ni kuendeleza utumwa usiokuwa na sababu kwa vijana wetu wa kitanzania.
Nawakilisha!
Naomba tusaidiane hapa kama kuna umuhimu wa kunganganizana kutumia kiingereza hata kwa kazi ambazo hiyo lugha haitumiki kabisa. Mfano, mimi Afisa wa kutoza kodi chini ya halmashauri fulani, kila siku niko minadani na huko ni Kiswahili na lugha za wenyeji wangu ndo zinatumika kwa sana lakini wakati wa kutafuta kazi naambiwa niandike barua kwa kiingereza sasa huu sio utumwa ndugu zangu? Matokeo yake nilichokiona kwa ndugu zangu wengi ni kila barua kuwa na mfanano wa namna fulani yaani utakuta tofauti ni jina tu lakini asilimia kubwa ya maneno ni yaleyale kwa kila barua ya mwombaji. Tufanye nini ili kuondokana na jinamizi hili la utumwa wa lugha?
Nimeona kwenye nchi za wenzetu, kujua kiingereza sio tija sana. Na hata waombapo kazi hiyo lugha sio ya lazima na haswa kama hiyo kazi haitahusisha mawasiliano ya kimataifa. Kwangu naona kungangania ni kuendeleza utumwa usiokuwa na sababu kwa vijana wetu wa kitanzania.
Nawakilisha!