Hivi Mnajua Kocha wa Zambia Herve Renard aliomba Kuifundisha Taifa Stars - TFF Wakamkataa!!!

Wachezaji ndiyo wa kulaumiwa na siyo kocha. Tujiulize mara ya mwisho kushiriki AFCON hadi leo ni makocha wangapi tumekuwa nao na hakuna lolote la maana, je wote hao hawana mbinu za ufundishaji? Ni muda muafaka kuiweka hii timu ya wazee pembeni na kuishirikisha timu ya chipukizi.
 
Usimba na uyanga unachangia sana kuua soka la tz

Ulipaswa kusema Usimba na Uyanga ndio kiini cha mpira wetu kudidimia. Hizi timu zote hushinda kwa kubebwa (kama magamba wanavyobebwa na "tume ya uchaguzi").
Usipokubali fair competition na ukategemea kubebwa utapata "mafanikio" ya ndani lakini ujinga wako utajidhihirisha wazi siku utashindanishwa na mwingine anaetoka mazingira tofauti na kubebwa. Yanga na Simba zisimamishwe kushiriki ligi angalau kwa miaka 3 ili mentality ya Usimba na Uyanga uishe!
 
nadhani tatizo letu sio kocha ni wachezaji wenye vipaji ni wachache au ni wale wale hawana jipya,hakuna ushindani wa kuchezea TAIFA STARS, Wacheza wana motisha ndogo,washabiki pia tunamatatizo tunacheza mpira majukwani hatuna uhalisia!timu zetu hazifanyi vizuri kimataifa!hata kocha mzuri kiasi gani apewe Taifa Stars tusitegemea suluhisho la ushindi!tubadilishe mfumo wetu wa mpira!wadhamini wajitokeze,mpira uchezwe mikoani,ligi ziwe za ushindani,waamuzi watende haki na makocha wawe professionals
 
Tanzania hatuwezi fika mbali kisoka sababu 10% na undungunaizeshe wa TFF, tulikuwa na kikosi kizuri kile cha copa coca cola kile kikosi kisingevunjwa tungekuwa zaidi ya chipolopolo.

Pili tujue ni jinsigani ya kuiandaa timu ya taifa, kipindi kile 1993 baada ya wachezaji wote kupoteza maisha wakati huo KK aliunda timu ya vijana akawapeleka brazili, akajitoa kwenye mashindano yote ya kimataifa akaisuka timu taratibu bila haraka ndipo wakapata hiki kikosi walianza kufundishwa zamani wakiwa bado kinda sasa wamekomaa kazi yao imeonekana wazi.

Tukitaka kufika walipo Zambia inabidi tutafute makinda tuwape mafunzo ya uhakika taratibu bila haraka nasi tutafikia walipo Zambia ama hata zaidi ya Zambia, tuache ubabaishaji na undugunaizesheni, ushkaji na mambo ya 10% tutafika mbali.

BT................ naomba nikuweke sawa. ...................

hapo kwenye red, wakati ule kulikuwa na FC na sio KK ikulu ya zambia..................

kwenye blue, ............... hawakujitoa mashindano ya kimataifa ila waliomba kama wiki mbili hivi kuteua timu nyingine na baada ya kuiteua timu mpya............ ilicheza mechi zote zilizokuwa zimebaki kikamilifu na kufaniukiwa kufuzu kucheza fainali za AFCON mwaka 1994 ................ na huko kwenye fainali, .............iliweza kuingia fainali na bafanabafana ............. wakati faianali hizo zilizofanyika kwa mara ya kwanza south africa................ ikishuhudiwa na madiba nwenyewe live.................
 
Hata tungemchukua morinyo au ancellot......bado tusingepata mafanikio...tatizo waswahili hatuelewi..kocha si sababu
 
Wachezaji ndiyo wa kulaumiwa na siyo kocha. Tujiulize mara ya mwisho kushiriki AFCON hadi leo ni makocha wangapi tumekuwa nao na hakuna lolote la maana, je wote hao hawana mbinu za ufundishaji? Ni muda muafaka kuiweka hii timu ya wazee pembeni na kuishirikisha timu ya chipukizi.

uko sahihi. Hakuna kitu ambacho tuko serious nacho hata kimoja. Wazembe wavivu na si mpira tu. Hata maofisini.
 
Tatizo la Tanzania wanadhani kuwa kocha kuwa mzungu ndio kufanikiwa....ona sasa wenzetu Zambia wamechukua kombe sisi bado tunauza sura nahuyu mzungu.
 
Hapo umemchukulia Herve Renard kama ndio siri pekee ya mafanikio ya Zambia, kwamba angepewa kikosi chochote hata kama dhaifu kama hiki chetu basi angeweza tu kushinda CAN 2012! Si kweli bana...uwepo wa wachezaji wenye kiwango kikubwa ni moja ya sababu ilizoifanya Zambia ishinde, hatuna sisi wachezaje kama wale wa Zambia. Labda Paulsen angekuwa na mafanikio zaidi ya Renard kama angepata kikosi kama cha Zambia...nobody knows!

Ahsante sana Dr, kiwango cha Wachezaji wetu wa sasa huwezi kabisa kukilinganinisha na enzi za akina Maulid Dilunga, King Kibaden, Kitwana Manara, Omar Kapera, Hassan Gobbos, Willy Mwaijibe au akina Sunday Manara, Mohamed Salim, Mohamed Chuma na wengineo wengi. Hata tupate kocha mzuri kiasi gani hatuwezi kufika kokote kwa sababu kiwango cha wachezaji wetu kwa sasa ni kidogo mno ukilinganisha na miaka ya nyuma.
 
Wachezaji wa Tanzania hawana malengo, wanalewa sifa za kijinga, wanasahau kinachofanya wawe pale, ni mambumbumbu.
Viongozi wa soka Tanzania, hawana vision, hawashauriki, wapo pale kwa interest zao

Ni ndto tanzania kushiriki mashindano yoyote ya kimataifa, hata tukienda ni ndoto kufika hata robo final achilia mbali kuchukua kombe

Inshu zima ni malipo, kama smart guy anayeweza kuziona zile vectors za speed kati ya upepo na mpira akisikia wanalipwa vizuri na mfumo unashawishi vizuri kuachana na madude mengine, kwa nini asifanye bidii kupiga soka? Na kwa nini wazazi wasimruhusu mtoto wao mwenye kipaji cha soka kufanya vitu vya mpira na si kukomaa naye na udaktari au uhandisi au uanasheria?

kwa hiyo hapa ni inshu nzima za malipo, mfumo wetu wa kubebana bebana bila kujali uwezo nawatu kutoamini kuwa kama watoto wao watawaruhusu kucheza mpira, wanadhani wataharibikiwa. kwa hiyo bado kuna mentality za hivyo!!!
 
Katika kumtafuta mrithi wa Marcio Maximo Kocha wa Zambia Herve Renard aliomba kuifundisha Taifa Stars lakini TFF wakasema hakidhi vigezo (hana qualification), ikabidi wamuajiri Poulsen. Tujiulize, je huyu Poulsen katufikisha wapi na huyu Herve Renard "the chosen one" au Mourinho wa Africa amewafikisha wapi Chipolopolo? Nawasilisha.
Chibingo, tatizo la Watanzania wanaoongoza soka katika TFF na katika vilabu vyetu wengi wao huwa ni wanasiasa tuu. Hugombania nafasi hizo ili wajulikane na baadaye utawasikia wanagombea UBUNGE.
 
Tatizo laTanzania sio kocha bali mfumo tulio nao sio wakutengeneza teaminayoweza kuleta ushindani kokote mfumo wetu unaruhusu wahuni kuingia katika team kubwa na hatimae taifa sasa leo Bongo hata akija Mourinho bado tutakuwa kichwa cha mwendawazimu

Na huo mfumo wa TFF unaakisi mfumo mbovu uliopo Serikalini.
 
Back
Top Bottom