Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,562
- 217,903
Wengi tumesikia na kusoma taarifa za Dada Jane Nyamsenda Kuondolewa kwenye Cheo cha Ukuu wa Wilaya, Taarifa hiyo imetolewa na Ikulu ambayo ndio Mamlaka yake ya Uteuzi, na baadaye tukaridhika tu kwamba ndugu Jane Nyamsenda ametumbuliwa, tukaona ni kawaida kama zilivyo kawaida zingine, tukanyamaza!
Bali mimi nikajiongeza kidogo ili kufahamu kiundani, kisa cha dada huyo mrembo kutumbuliwa haraka na ghafla namna hiyo, niliyoyaona yamenistaajabisha na kunichekesha sana!
Siku ya Wanawake ya Dunia, DC aliandaa kama igizo hivi, sijui ni la utayari wa vyombo vya dola au sijui ni kuonyesha uwezo wa Wanawake, haieleweki hasa lengo la jambo lile, basi bhana Wananchi wakiwa wamekusanyika uwanjani msafara wa Mkuu wa Wilaya ambaye bila shaka alikuwa ndio Mgeni Rasmi Ukaingia uwanjani, ukiwa umesheheni askari kibao wenye Mabunduki ya kivita, wakashuka kikakamavu wakaizunguka gari ya DC, mpambe akaja akafungua mlango, DC akatoka akiwa nadhifu huku akitilia kilemba cha kichwa kama kile anachovaa Mh Rais.
Msafara wake ukaanza kusogea kwa miguu akiwa katikati lundo la Maaskari wenye mitutu mizito, sasa baadaye mara askari wake wakaanza kurusha risasi kuelekea mbele yao huku DC akinyakuliwa na kurejeshwa ndani ya gari kwa Style ya kuokoa viongozi dhidi ya maadui na hatimaye gari kuondoka kwa kasi kubwa!
Baada ya kuona jambo hili nimegundua kwamba DC Jane Nyamsenda ni mkuu wa Wilaya wa aina ya Makonda, Sabaya na Jerry Muro, anaonekana anapenda kujimwambafy kupita maelezo! Yaani kwake Ukuu wa Wilaya ni kama Ukuu wa Nchi, Tukio aliloliandaa halikuwa na uhusiano wowote na siku ya Wanawake, Sijui ni nani alimdanganya? Ni Aibu sana kwake, kwa Wazazi wake na kwa waliomteua.
Natoa wito kwa mamlaka ya Uteuzi kwamba, pamoja na ukweli kwamba majukumu ya Mkuu wa Wilaya ya Kufungua Makongamano ya UKIMWI, Kupokea Viongozi wa Kotaifa, Kusimamia Mbio za Mwenge na Kusaidia CCM kwenye Uchaguzi ni mepesi kuliko hata majukumu ya mmachinga au mama lishe, lakini bado kuna haja ya kuteua watu sahihi wanaostahili, haya mambo ya kuokota watu UVCCM, watoto, wajomba, mashemeji wa viongozi, walioshindwa ubunge na Chawa wa viongozi yataliaibisha Taifa, tuwe na mfumo ulio wazi wa kuchagua hawa watu au Tufute hivi vyeo ili kuiheshimisha nchi.
Bali mimi nikajiongeza kidogo ili kufahamu kiundani, kisa cha dada huyo mrembo kutumbuliwa haraka na ghafla namna hiyo, niliyoyaona yamenistaajabisha na kunichekesha sana!
Siku ya Wanawake ya Dunia, DC aliandaa kama igizo hivi, sijui ni la utayari wa vyombo vya dola au sijui ni kuonyesha uwezo wa Wanawake, haieleweki hasa lengo la jambo lile, basi bhana Wananchi wakiwa wamekusanyika uwanjani msafara wa Mkuu wa Wilaya ambaye bila shaka alikuwa ndio Mgeni Rasmi Ukaingia uwanjani, ukiwa umesheheni askari kibao wenye Mabunduki ya kivita, wakashuka kikakamavu wakaizunguka gari ya DC, mpambe akaja akafungua mlango, DC akatoka akiwa nadhifu huku akitilia kilemba cha kichwa kama kile anachovaa Mh Rais.
Msafara wake ukaanza kusogea kwa miguu akiwa katikati lundo la Maaskari wenye mitutu mizito, sasa baadaye mara askari wake wakaanza kurusha risasi kuelekea mbele yao huku DC akinyakuliwa na kurejeshwa ndani ya gari kwa Style ya kuokoa viongozi dhidi ya maadui na hatimaye gari kuondoka kwa kasi kubwa!
Baada ya kuona jambo hili nimegundua kwamba DC Jane Nyamsenda ni mkuu wa Wilaya wa aina ya Makonda, Sabaya na Jerry Muro, anaonekana anapenda kujimwambafy kupita maelezo! Yaani kwake Ukuu wa Wilaya ni kama Ukuu wa Nchi, Tukio aliloliandaa halikuwa na uhusiano wowote na siku ya Wanawake, Sijui ni nani alimdanganya? Ni Aibu sana kwake, kwa Wazazi wake na kwa waliomteua.
Natoa wito kwa mamlaka ya Uteuzi kwamba, pamoja na ukweli kwamba majukumu ya Mkuu wa Wilaya ya Kufungua Makongamano ya UKIMWI, Kupokea Viongozi wa Kotaifa, Kusimamia Mbio za Mwenge na Kusaidia CCM kwenye Uchaguzi ni mepesi kuliko hata majukumu ya mmachinga au mama lishe, lakini bado kuna haja ya kuteua watu sahihi wanaostahili, haya mambo ya kuokota watu UVCCM, watoto, wajomba, mashemeji wa viongozi, walioshindwa ubunge na Chawa wa viongozi yataliaibisha Taifa, tuwe na mfumo ulio wazi wa kuchagua hawa watu au Tufute hivi vyeo ili kuiheshimisha nchi.