Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Alipokosolewa Mkapa,hakukosolewa kwa sababu hakuwa na zuri alilofanya, alikosolewa kwa sababu ilihitajita afanye zaidi ya aliyoyafanya.Tunafahamu wote wakati wa Awamu ya tatu ya Mzee Mkapa tulikuwa na changamoto kubwa ya vitendo vya Rushwa na ndiyo maana alikosolewa,wakosoaji walilenga kutaka alifanyie kazi tatizo la Rushwa ambalo lilikuwa doa,Ila yapo mazuri aliyoyafanya na hatutamtendea haki tusipoyatambua.
Mbali na mianya ya Rushwa,Awamu ya Mzee Mkapa ilipatwa na changamoto za uendeshaji wa Siasa visiwani Zanzibar,na ndiyo maeneo ambayo Serikali yake ilikosolewa sana,Ila kuna mazuri alifanya na hatuwezi kusema hakufanya kitu,itakuwa hatumtendei haki na ni nadhani aliyafanya kwa sababu yalikuwa ndiyo mahitaji ya kipindi hicho.Hebu ona baadhi ya machache aliyoyafanya......
1.Tanzania inajivunia kuwa na Uwanja mkubwa wa mpira Afrika Mashariki na Kati(Ulijengwa wakati wa Mkapa).
2.Chuo Kikuu Kikubwa Afrika Mashariki(Chuo Kikuu Cha Dodoma),Ni matokeo ya Maamuzi ya Serikali ya Mzee Mkapa na kuja kukamilisha kwa vitendo na Serikali ya Jakaya Kikwete,kumbukumbu kabla ya UDOM watanzania wenye sifa za kusoma Chuo Kikuu walikuwa wanapigana Vikumbo UDSM na SUA kabla ya Ujio wa SAUT.
3.Mtandao wa Barabara za Lami nchi nzima zilianza kutengwa kwa speed kubwa wakati wa Mzee Mkapa,nadhani alilenga kuacha Alama ya kuwa kiongozi ambaye amejenga mtandao wa Lami nchi nzima.
4.Mzee Mkapa aliendeleza pale alipoanzisha Mzee Mwinyi kwa kubadili mfumo wa Uchumi kutoka Uchumi hodhi kwenda Uchumi wa Ubia kati ya Sekta binafsi na Serikali na ndiyo tukaanza kuona kasi kubwa ya uwekezaji katika kila sekta kutoka sekta binafsi,leo tuna Vyuo Vikuu zaidi ya 20 vinavyomilikiwa na sekta binafsi,kwa upande wa Sekta ya Afya zaidi ya asilimia 50 ya vituo vya Afya vinamilikiwa na sekta binafsi Haya Ni matokeo ya maono ya Mzee Mkapa.
5.Mzee Mkapa alianza kutoa mikopo kwa wanafunzi wa Vyuo Vikuu binafsi,kabla ya uamuzi huo ilikuwa ili upate Mkopo ilikuwa lazima usome kati ya UDSM,Muhimbili au SUA hii ilisababisha vijana wengi wenye sifa ya kusoma Chuo Kikuu wakakosa fursa hiyo,leo tujiulize Mkapa asingeamua Haya wangapi wangekosa fursa hii ya kusoma mpaka Chuo Kikuu?Hizi degree zilizotapakaa mpaka Vijijini ni matokeo ya Uongozi wa Mzee Mkapa.
6.Ni wakati wa Mzee Mkapa ndiyo Ajira za Serikali zilirejea rasmi,mwaka 1997,ndiyo Serikali ilirejesha kwa kasi Ajira Serikalini Baada ya kusitishwa kwa muda kwa kile kilichoitwa Kubana matumizi,kabla yake ilikuwa Ni kawaida mtu kumaliza Chuo na kukaa hata miaka 5 bila Ajira kwa sababu kasi ya Serikali kuajiri ilifubaishwa kwa kisingizio cha kubana matumizi.
8.Mzee Mkapa alipokea nchi ikiwa na mzigo wa madeni,binafsi sikuwahi kumsikia akimsema mtangulizi wake kwa kukopa huko,Mzee Mkapa alijua kwa mazingira yeyote Serikali ya Mzee Mwinyi ilikuwa lazima ikope Maana ilichokikuta hazina ilihitaji busara na akili kubwa kuiongoza nchi na ndiyo Maana Mzee Mwinyi alikopa sana,Mzee Mkapa kwa kutambua kazi kubwa aliyofanya Mzee Mwinyi,aliyalipa madeni mpaka kufikia chini ya Trilion 8,alilipa kimya kimya huku akijua Ni wajibu wake.
9.Bunge hili la Kisasa lililopo Dodoma,lilijengwa na Serikali ya Mzee Mkapa.
10.Hata kwenye michezo kila Awamu kulikuwa na mafanikio,Awamu ya kwanza ilishuhudia Tanzania ikicheza kwa Mara ya kwanza fainali za Mataifa Huru barani Afrika,Awamu ya Pili Simba ilicheza faunal za michuano ya kumbe la shirikisho la kabumbu barani Afrika,Awamu ya Tatu Yanga ikafuzu kucheza hatua ya makundi ya kombe la Klabu Bingwa Afrika,awamu ya nne Simba ikacheza hatua hiyo ya makundi ya Klabu bingwa,Awamu ya tano Taifa Stars imecheza fainal za mataifa Afrika huku Simba ikifika hatua za makundi.
Kila kupindi kinamafanikio yake ambayo Ni vyema tukayatambua,Ukosoaji hulenga kuona mafanikio zaidi na zaidi na si ishara ya kubeza.
Shida kubwa nayoiona Ni tafsiri ya Ukosoaji,baadhi hudhani Ukosoaji ni Ubezaji,Hapana Mimi naamini ukosoaji nia yake Ni kumfanya mtu atende vizuri zaidi ya anavyofanya.
Jumapili njema,usiku nitamuelezea Mzee Mwinyi .
Wasalaam
Dotto Bulendu.
Mbali na mianya ya Rushwa,Awamu ya Mzee Mkapa ilipatwa na changamoto za uendeshaji wa Siasa visiwani Zanzibar,na ndiyo maeneo ambayo Serikali yake ilikosolewa sana,Ila kuna mazuri alifanya na hatuwezi kusema hakufanya kitu,itakuwa hatumtendei haki na ni nadhani aliyafanya kwa sababu yalikuwa ndiyo mahitaji ya kipindi hicho.Hebu ona baadhi ya machache aliyoyafanya......
1.Tanzania inajivunia kuwa na Uwanja mkubwa wa mpira Afrika Mashariki na Kati(Ulijengwa wakati wa Mkapa).
2.Chuo Kikuu Kikubwa Afrika Mashariki(Chuo Kikuu Cha Dodoma),Ni matokeo ya Maamuzi ya Serikali ya Mzee Mkapa na kuja kukamilisha kwa vitendo na Serikali ya Jakaya Kikwete,kumbukumbu kabla ya UDOM watanzania wenye sifa za kusoma Chuo Kikuu walikuwa wanapigana Vikumbo UDSM na SUA kabla ya Ujio wa SAUT.
3.Mtandao wa Barabara za Lami nchi nzima zilianza kutengwa kwa speed kubwa wakati wa Mzee Mkapa,nadhani alilenga kuacha Alama ya kuwa kiongozi ambaye amejenga mtandao wa Lami nchi nzima.
4.Mzee Mkapa aliendeleza pale alipoanzisha Mzee Mwinyi kwa kubadili mfumo wa Uchumi kutoka Uchumi hodhi kwenda Uchumi wa Ubia kati ya Sekta binafsi na Serikali na ndiyo tukaanza kuona kasi kubwa ya uwekezaji katika kila sekta kutoka sekta binafsi,leo tuna Vyuo Vikuu zaidi ya 20 vinavyomilikiwa na sekta binafsi,kwa upande wa Sekta ya Afya zaidi ya asilimia 50 ya vituo vya Afya vinamilikiwa na sekta binafsi Haya Ni matokeo ya maono ya Mzee Mkapa.
5.Mzee Mkapa alianza kutoa mikopo kwa wanafunzi wa Vyuo Vikuu binafsi,kabla ya uamuzi huo ilikuwa ili upate Mkopo ilikuwa lazima usome kati ya UDSM,Muhimbili au SUA hii ilisababisha vijana wengi wenye sifa ya kusoma Chuo Kikuu wakakosa fursa hiyo,leo tujiulize Mkapa asingeamua Haya wangapi wangekosa fursa hii ya kusoma mpaka Chuo Kikuu?Hizi degree zilizotapakaa mpaka Vijijini ni matokeo ya Uongozi wa Mzee Mkapa.
6.Ni wakati wa Mzee Mkapa ndiyo Ajira za Serikali zilirejea rasmi,mwaka 1997,ndiyo Serikali ilirejesha kwa kasi Ajira Serikalini Baada ya kusitishwa kwa muda kwa kile kilichoitwa Kubana matumizi,kabla yake ilikuwa Ni kawaida mtu kumaliza Chuo na kukaa hata miaka 5 bila Ajira kwa sababu kasi ya Serikali kuajiri ilifubaishwa kwa kisingizio cha kubana matumizi.
8.Mzee Mkapa alipokea nchi ikiwa na mzigo wa madeni,binafsi sikuwahi kumsikia akimsema mtangulizi wake kwa kukopa huko,Mzee Mkapa alijua kwa mazingira yeyote Serikali ya Mzee Mwinyi ilikuwa lazima ikope Maana ilichokikuta hazina ilihitaji busara na akili kubwa kuiongoza nchi na ndiyo Maana Mzee Mwinyi alikopa sana,Mzee Mkapa kwa kutambua kazi kubwa aliyofanya Mzee Mwinyi,aliyalipa madeni mpaka kufikia chini ya Trilion 8,alilipa kimya kimya huku akijua Ni wajibu wake.
9.Bunge hili la Kisasa lililopo Dodoma,lilijengwa na Serikali ya Mzee Mkapa.
10.Hata kwenye michezo kila Awamu kulikuwa na mafanikio,Awamu ya kwanza ilishuhudia Tanzania ikicheza kwa Mara ya kwanza fainali za Mataifa Huru barani Afrika,Awamu ya Pili Simba ilicheza faunal za michuano ya kumbe la shirikisho la kabumbu barani Afrika,Awamu ya Tatu Yanga ikafuzu kucheza hatua ya makundi ya kombe la Klabu Bingwa Afrika,awamu ya nne Simba ikacheza hatua hiyo ya makundi ya Klabu bingwa,Awamu ya tano Taifa Stars imecheza fainal za mataifa Afrika huku Simba ikifika hatua za makundi.
Kila kupindi kinamafanikio yake ambayo Ni vyema tukayatambua,Ukosoaji hulenga kuona mafanikio zaidi na zaidi na si ishara ya kubeza.
Shida kubwa nayoiona Ni tafsiri ya Ukosoaji,baadhi hudhani Ukosoaji ni Ubezaji,Hapana Mimi naamini ukosoaji nia yake Ni kumfanya mtu atende vizuri zaidi ya anavyofanya.
Jumapili njema,usiku nitamuelezea Mzee Mwinyi .
Wasalaam
Dotto Bulendu.