Haludzedzele
JF-Expert Member
- Nov 22, 2012
- 1,468
- 528
Nipo safarini kutoka Dar kwenda Mbeya na basi la Majinjah Special tumevuka mizani ya Kibaha,Mikese na Mikumi baada ya hapo mikumi stand konda kapakia mizigo ya kutosha tumefika Ipogolo Iringa wamepakia mizigo na watu kibao kituko sasa Mzani wa Tanangozi tumepima mara ya kwanza gari limezd mara ya pili umezid mara ya 3 tena mara ya nne tena pamoja na kupunguza abiria mara ya 5 konda akaomba abiria wote tushuke wakashuka wote nikabaki mwenyewe na dereva likapima ikaonekana lipo safi wamepanda abiria tumeruhusiwa sasa ivi. Swali kwa yeyote anaefaham kwan gar likizid inatakiwaje? Kwa kweli sioni haja ya kuwa na mizani kama watu wanavunja sheria na tanroad waangalizi wenyewe wanaangalia tu