Hivi mizani ya tanroads ina kazi gani hasa?

Haludzedzele

JF-Expert Member
Nov 22, 2012
1,468
528
Nipo safarini kutoka Dar kwenda Mbeya na basi la Majinjah Special tumevuka mizani ya Kibaha,Mikese na Mikumi baada ya hapo mikumi stand konda kapakia mizigo ya kutosha tumefika Ipogolo Iringa wamepakia mizigo na watu kibao kituko sasa Mzani wa Tanangozi tumepima mara ya kwanza gari limezd mara ya pili umezid mara ya 3 tena mara ya nne tena pamoja na kupunguza abiria mara ya 5 konda akaomba abiria wote tushuke wakashuka wote nikabaki mwenyewe na dereva likapima ikaonekana lipo safi wamepanda abiria tumeruhusiwa sasa ivi. Swali kwa yeyote anaefaham kwan gar likizid inatakiwaje? Kwa kweli sioni haja ya kuwa na mizani kama watu wanavunja sheria na tanroad waangalizi wenyewe wanaangalia tu
 
Hizo mizani ni kwa manufaa binafsi yakishatokea majanga utasikia uzembe wa dereva kaendesha mwendo kasi!
Inatakiwa Mh Magufuli ulitolee macho hilo.Na sisi abiria ni tamaa ya kufika tuendapo kwa mashaka hapohapo mliposhuka wote mngegoma kupanda tena hadi mmiliki alete basi lingine kwa ajili ya mizigo.
Ombeni Mungu awabebee mizigo yenu mfike Salama!
 
Hizo mizani ni kwa manufaa binafsi yakishatokea majanga utasikia uzembe wa dereva kaendesha mwendo kasi!
Inatakiwa Mh Magufuli ulitolee macho hilo.Na sisi abiria ni tamaa ya kufika tuendapo kwa mashaka hapohapo mliposhuka wote mngegoma kupanda tena hadi mmiliki alete basi lingine kwa ajili ya mizigo.
Ombeni Mungu awabebee mizigo yenu mfike Salama!

kweli mkuu
 
Back
Top Bottom