Hivi mhimili wa mahakama Tanzania haitambui hati ya dharura iliyowekwa na watuhumiwa akina Mbowe?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Tunashuhudia "figisu figisu" nyingi sana zikiendelea katika kesi ya akina Mbowe ikifanyiwa "delaying tactics" huku kiongozi huyo Mkuu wa Chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema, pamoja na mbunge mwenzake Esther Matiko, wakiendelea kusota gerezani Segerea kwa kile kilichoitwa kuidharau mahakama ya Kisutu, tokea mwezi Novemba mwaka Jana, ukiwa huu ni mwezi wa pili wako mahabusu!

Tunafahamu pia kuwa mawakili wa Mbowe walipeleka hati ya dharura mahakama kuu kupinga kufutiwa dhamana kwa wateja wao, baada ya mahakama ya Kisutu kufuta dhamana ya watuhumiwa hao wawili

Tunafahamu kuwa mtu hawezi kupewa adhabu ya kifungo hapa nchini hadi mahakama itakapothibitisha pasipo shaka yoyote kuwa mtu huyo ametenda kosa la jinai

Hivi hiki kitendo cha watuhumiwa hao wawili kukaa gerezani kwa mwezi wa pili sasa tutakiitaje kama siyo kuhukumiwa "indirect" kufungwa gerezani??

Sasa inakuwaje hawa akina Mbowe "wanakomolewa" kwa kukaa mahabusu ikiwa ni mwezi wa pili sasa, wakati mahakama haijawahukumu kuwa wametenda kosa la jinai kwa tuhuma walizofunguliwa nazo mashitaka??

Au tuseme mhimili huo wa mahakama nao "umetekwa" na mhimili wa Executive, kwa kuwa tuliwahi kumsikia Mheshimiwa Rais Magufuli akitoa onyo hadharani kuwa viongozi wa Chadema wataozea jela??

Ni vyema mhimili wa mahakama ukajiosha katika kutenda haki na ukajitoa katika "kufikirika" kuwa unatumika na mhimili wa Executive katika maagizo yake

Kwani ni mhimili huo pekee ndiyo unaotambulika kuwa ndiyo unaotenda haki hapa nchini na ndiyo kimbilio la wanyonge wa nchi hii

Tunafahamu kuwa mhimili mwingine wa Bunge tayari "ushatekwa" na mhimili wa Executive na unatekeleza yale inayoagizwa.....

Itakapotokea wananchi wakakosa Imani na mhimili wa mahakama, basi ujue kama nchi tutakuwa tumefikia hatua mbaya sana na tunaomba mhimili huo wa mahakama utende haki

Mungu ibariki Tanzania
 
Uamsho wapo mahabusu miaka 5 hii waislam tumepiga kelele mpaka leo wapo ndani. Lema na Sugu waliwekwa ndani sasa Mbowe na Matiko wapo ndani. Wote hao amri kutoka juu ndio imewaweka ndani, na wala sio uamuzi wa kisheria wa mahakama. Bora mahakama za Somali kuliko hizi za kisutu


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Mahakama hai - serve justice kama inavyotakiwa kufanya, inafuata maelekezo kutoka juu badala ya kufuata vifungu vya sheria vinasemaje.

Watu hawana aibu kabisa yani.
Yaani ni hatari sana.........

Mahakama inajua wazi kuwa mawakili wa upande wa utetezi walifungua kwa hati ya dharura mahakama kuu, lakini kwa namna ya "delaying tactics" inayoonyeshwa katika shauri hilo inatia shaka kama mhimili wa mahakama "haujatekwa" na mhimili wa Executive!
 
Yaani ni hatari sana.........

Mahakama inajua wazi kuwa mawakili wa upande wa utetezi walifungua hati ya dharula mahakama kuu, lakini kwa namna ya "delaying tactics" inayoonyeshwa katika shauri hilo inatia shaka kama mhimili wa mahakama "haujatekwa" na mhimili wa Executive
Ni jambo la ajabi mahakama kisema CJADEMA wafuatilie hati ya dharura...yani hawajui. Na mahakama kuu na rufani nazo zipo tu.

Tunayoona kwenye korosho na wafanyabiashara itakuja kwa kila kiumbe haijalishi ni chama gani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani ni hatari sana.........

Mahakama inajua wazi kuwa mawakili wa upande wa utetezi walifungua hati ya dharula mahakama kuu, lakini kwa namna ya "delaying tactics" inayoonyeshwa katika shauri hilo inatia shaka kama mhimili wa mahakama "haujatekwa" na mhimili wa Executive
Kumbuka salamu kutoka juu alizopewa Lowasa kwa viongozi hasa wa CHADEMA
 
Mkibanwa mbavu mnadai mahakama inaingiliwa mara ohoo haitendi haki,mkishinda kesi mnajigamba eti nyie ni akili kubwa.
Nasemaje mzee Mashauri kaza hapo hapo.
2019 mtasoma namba za kila rangi.
Tulia hapo hapo dawa ikuingie.
Umeelewa vizuri Mada iliyopo mezani..?unaonyesha ni jinsi gani ulivyo Zuzu.
 
Uamsho wapo mahabusu miaka 5 hii waislam tumepiga kelele mpaka leo wapo ndani. Lema na Sugu waliwekwa ndani sasa Mbowe na Matiko wapo ndani. Wote hao amri kutoka juu ndio imewaweka ndani, na wala sio uamuzi wa kisheria wa mahakama. Bora mahakama za Somali kuliko hizi za kisutu


Ndukiiiii ‍♂️‍♂️‍♂️
'...bora mahakama za Somalia sio hizi za Kisutu".

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunashuhudia "figisu figisu" nyingi sana zikiendelea katika kesi ya akina Mbowe ikifanyiwa "delaying tactics" huku kiongozi huyo Mkuu wa Chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema, pamoja na mbunge mwenzake Esther Matiko, wakiendelea kusota gerezani Segerea kwa kile kilichoitwa kuidharau mahakama ya Kisutu, tokea mwezi Novemba mwaka Jana, ukiwa huu ni mwezi wa 2 wako mahabusu!

Tunafahamu pia kuwa mawakili wa Mbowe walipeleka hati ya dharula mahakama kuu, baada ya mahakama ya Kisutu kufuta dhamana ya watuhumiwa hao wawili

Tunafahamu kuwa mtu hawezi kupewa adhabu ya kifungo hadi pale mahakama itakapodhibitisha pasipo shaka yoyote kuwa mtu huyo ametenda kosa la jinai

Hivi hiki kitendo cha watuhumiwa hao wawili kukaa gerezani kwa mwezi wa pili sasa tutakiitaje kama siyo kuhukumiwa "indirect" kufungwa gerezani??

Sasa imakuwaje hawa akina Mbowe "wanakomolewa" kwa kukaa mahabusu ikiwa ni mwezi wa pili sasa, wakati mahakama haijawahukumu kuwa wametenda kosa la jinai kwa tuhuma walizofunguliwa nazo mashitaka??

Au tuseme mhimili huo wa mahakama nao "umetekwa" na mhimili wa Executive, kwa kuwa tuliwahi kumsikia Mheshimiwa Rais Magufuli akitoa onyo hadharani kuwa viongozi wa Chadema wataozea jela??

Ni vyema mhimili wa mahakama ukajiosha katika kutenda haki na ukajitoa katika "kufikirika" kuwa unatumika na mhimili wa Executive katika maagizo yake

Kwani ni mhimili huo pekee ndiyo unaotambulika kuwa ndiyo unaotenda haki hapa nchini

Tunafahamu kuwa mhimili mwingine wa Bunge tayari "ushatekwa" na mhimili wa Executive na unatekeleza yale inayoagizwa.....

Itakapotokea wananchi wakakosa Imani na mhimili wa mahakama, basi ujue kama nchi tutakuwa tumefikia hatua mbaya sana na tunaomba mhimili huo wa mahakama utende haki

Mungu ibariki Tanzania
dharula = dharura

itakapodhibitisha = itakapothibitisha
 
Mahakama imekandamizwa na jiwe
Ninecheka sana hii kauli, lakini kinachoendelea kwa Upinzani kinatia uchungu na hakitakiwa kuvumiliwa kwa namna yoyote, ni ujinga kudhani unahaki juu ya Uhuru na haki ya kiumbe wa Mungu, Afrika ina laana na laana inatokana na matendo ya viongozi wake kwa wananchi wanao waongoza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi hii Mihimili yote mitatu kwa sasa inaongozwa na mtu mmoja tu. Na matokeo yake ndiyo haya yanayoonekana hivi sasa. Watafsiri Sheria wanaona ni bora kwenda likizo wasikilizie upepo unavumaje. Wasije wakatenda haki huku mwenye mihimili yake akisononeka.

Mhimili wa Mahakama utakuja kulemewa na majukumu kama ilivyotokea kwa ule mwingine kwenye suala la korosho. Matokeo yake ni aibu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom