Hivi Mhimili wa Mahakama kipaumbele chenu kwa sasa ni kutafsiri lugha za sheria zenu na kuwa kwa Kiswahili?

Status
Not open for further replies.

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Katika nchi yetu kila mwaka huwa tunakuwa na wiki moja ambayo huwa tunaiita ni wiki ya sheria nchini, ambapo tumeianza rasmi tarehe 24/1/2021 na kilele chake kitakuwa tarehe 1/2/2021.

Ninajua kumekuwa na juhudi kubwa sana toka kwenye mhimili mmoja ambao ni serikali "kuulazimisha" mhimili mwingine wa mahakama, ili waweke kipaumbele chao kwa kutafsiri sheria za nchi na kuwa katika lugha ya Kiswahili.

Ninavyojua Mimi katika utawala bora wa sheria, ni lazima kuwepo na "power separation" miongoni ya mihimili mitatu ya dola, ambayo ni "Executive, Legislature and Judiciary'

Ninashoshangaa ni kwa hapa nchini kwetu kwa mkuu mmoja wa Mhimili, ambao ni "Executive" ambapo ni Rais wa nchi, kuagiza mhimili mwingine ambao ni "Judiciary" kuwa ni "lazima" wazitafsiri sheria za mahakama zao kutoka lugha yao rasmi, ambayo ni Kiingereza na kuwa Kiswahili, kwa kile alichokiita wananchi wake wananyimwa haki zao, kwa mhimili huo kutumia lugha ya Kiingereza, ambapo kwa madai yake ni kuwa wananchi wake walio wengi, hawana ufahamu mkubwa wa lugha hiyo, hivyo wananyimwa fursa ya kupata haki yao kwenye mhimili huo wa mahakama.

Hebu tujiulize, hivi ni kwanini mhimili huo hautoi kipaumbele katika mambo ya kisheria, ambayo ndiyo kilio na kipaumbele cha wananchi wengi kwa hivi sasa?

Hebu nitoe mifano ya vipaumbele hivyo:-

1.N i kwanini nchi yetu haitoi kipaumbele kubadilisha sheria ya kutopingwa mahakamani, matokeo ya Urais, mara tu yatangazwapo na Tume ya uchaguzi wa Taifa, tukiwa ndiyo nchi pekee tunaonyima fursa hiyo ya kupeleka mahakamani malalamiko hayo katika kipande hiki cha Bara hili la Afrika?

2. Ni kwanini mahakama zetu kipindi hiki zimetumika kisiasa zaidi, kwa kuendesha kesi nyingi za "kubambika" zinazohusu uhujumu uchumi na utakatishaji pesa, kuliko wakati wowote katika serikali za awamu zilizopita?

3. Ni kwanini DPP amepewa mamlaka makubwa mno ya kuamua nani akae ndani na nani atoke awe huru, katika kile kinachoitwa "plea bargaining" katika kesi zao za "kubambika" katika utawala huu wa awamu hii ya uongozi?

Mimi nadhani hayo ndiyo ya kuyapa kipaumbele katika ubadilishaji wa sheria za mahakama zetu, kuliko hilo la kubadilisha lugha, kwa kuwa hiyo lugha ya Kiingereza ndiyo lugha rasmi ya kimahakama, na siyo kero na kilio cha wananchi wengi hapa nchini kwa hivi sasa, katika kunyimwa haki za kisheria nchini.
 
Mkuu mimi naona kutafsiri Sheria kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili ni jambo zuri sana tu labda uzungumzie kwenye suala la Serikali/Executive kuamuru mahakama/judiciary kufanya hivyo ni kosa kwa mjibu wa katiba kuingilia Uhuru wa muhimili mwengine.

Labda serikali iwe inatoa maoni yake kwa mihimili mingine namna mambo wangependa yawe ili kujenga utawala bora na kuspee up maendeleo nk basi na sio kuamuru.

Ila kwa jambo la kutafsiri Sheria katika lugha inayofahamika na kila raia wa Tanzania ni jambo zuri kabisa kwani Sheria ndio kama fuel katika nchi yeyote aijali ni kipaumbele cha sasa au la!
 
Mkuu mimi naona kutafsiri Sheria kutoka kiingereza kwenda kiswahili ni jambo zuri sana tu labda uzungumzie kwenye suala la Serikali/executive kuamuru mahakama/judiciary kufanya hivyo ni kosa kwa mjibu wa katiba kuingilia Uhuru wa muhimili mwengine...
Joselela
Lakini ndiyo kipaumbele chetu kama nchi kwa hivi sasa?

Ni kwanini hawataki kuzibadilisha sheria ambazo ndizo zinazonyima wananchi haki zao, kama kutopingwa mahakamani kwa matokeo ya urais, Mara tu yanapotangzwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi?
 
Hivi kwa nini Nchi hii watu au mtu kama hawezi au hajui kitu fulani badala ya kujifunza kitu hicho hutumia udhaifu wao kutafuta unafuu?

Law is an art ! na kwa kuwa mambo mengi tumerithi kutoka " common law" hakuna jinsi ya kutojua lugha ya Kiingereza, tuache kudanganya watu kwa temporary gratifications!

Dunia haiwezi kutusubiri sisi na mambo yetu ya ajabu ajabu!

Angalia hata chaguzi zetu kunapotokea disputes au contradictions huoni wananchi, wanahabari au wanasheria nguli tulio nao wanaoweza ku- communicate na Dunia kujua tatizo hapa Tanzania liko wapi?

Fuatilia vyombo vikubwa vya habari Duniani (CNN, BBC, Aljazeera, n.k) kila siku uone live communications zinahusu mataifa gani huku Africa ( utakuta ni Nigeria, Ghana, Kenya, Uganda n.k)!

Angalia hata uchaguzi wa Uganda juzi hapa Dunia imeu- cover sana kwa sababu Waganda wengi wanaweza ku- communicate under foreign language! Kina Robert Kyagulani (Bob Wine) wako eloquent sana! They can talk to the World!

Tanzania hapa ukianza kumhoji mwandishi wa habari au mwanasiasa kuhusu disputes au jambo lolote kuhusu uchaguzi utasikia ," Zeeee, zeeeee, zis, zis , onole (only) , to meee, to meee, to meee!!! Ujinga mtupu!!!

Mwl. Julius Nyerere alishawambia huko nyuma akina Prof. Mulokozi pale UDSM kuwa English ndio Kiswahili cha Dunia hii!

Tujifunze na tukienzi Kiswahili chetu lakini tusi- undermine role ya English katika Dunia tuliyonayo leo.

Huwezi kila "transaction" kubebana na Wakalimani. Kuna mambo mengine ni ya siri sana yanahitaji maximum confidentiality , hivyo kujua English vizuri ni key point tuache kudanganyana!

After all ni ujinga kudanganya watu kuwa wananyimwa haki kwa kuwa sheria ziko kwa Kiingereza ( English)! Haki zinanyimwa kwa contents zilizomo katika Sheria hata kama zimeandikwa kwa Kiswahili!

Mfano. Sheria inayopinga matokeo ya Rais katika Uchaguzi kutopingwa katika Mahakama ikiandikwa kwa Kiswahili itaruhusu Matokeo hayo kupingwa?
 
Hivi kwa nini Nchi hii watu au mtu kama hawezi au hajui kitu fulani badala ya kujifunza kitu hicho hutumia udhaifu wao kutafuta unafuu !!!?..
Umeongea ukweli mtupu Mkuu

Hii nchi sasa hivi inapenda kujishughulisha na "petty issues" kama hizo za kubadilisha sheria na kuwa kiswahili wakati "major issues" kama hizo za nchi yetu kwenye sheria kuweka marufuku, pale Tume ya uchaguzi itakapotangaza matokeo kuwa ni marufuku kutoyapinga matokeo hayo kwenye mahakama yoyote nchini, ikiachwa iendelee!

Hivi tukiwaambia watawala wetu kuwa mmedhamiria kukaa madarakani milele na milele, kwa njia zozote hata zile za haramu, tutakuwa tumekosea kweli?

Hivi kama nyinyi maccm, mna uhakika kuwa mnapata ushindi halali kwenye chaguzi zetu, ni kwanini basi muweke katazo la kutoweza kupeleka kesi kwenye mahakama zozote hapa nchini?

Kwa nini mnajipa majukumu ya ki-mungu mtu, kwa kujiona nyinyi mko sahihi kwa asilimia 100 kwa kila mnalolifanya?
 
Mambo ya hovyo hovyo yasiyo na tija ndio yanapewa kipaumbele.. sijui kama jambo hili hata mkulu analiona la maana . Waziri amekosa ubunifu...
 
Mambo ya hovyo hovyo yasiyo na tija ndio yanapewa kipaumbele.. sijui kama jambo hili hata mkulu analiona la maana . Waziri amekosa ubunifu...
Kwani hujui kuwa Rais Magufuli ndiye analipigia debe sana, hili suala la kubadilisha lugha za kisheria na kuwa Kiswahili?
 
Itabidi hivyo vitabu vya sheria vilivyopo vitafsiriwe kwa kiswahili, ila sijui kama lugha yetu ina mtaji wa maneno wa kutosha kama lugha ya kiingereza, na ni muda gani watachukua kutekeleza hilo jambo.

Mfano wa hili huwa naliona kwenye biblia, toleo la kiswahili lina maneno machache ambayo hayajajieleza kwa undani zaidi ukilinganisha na biblia ya kiingereza ambayo inatoa maelezo ya kujitosheleza zaidi.

Sababu ya kuingiliwa mhimili wa mahakama zaidi inatokana na katiba yetu mbovu ya sasa inayompa Rais mamlaka ya kufanya teuzi za viongozi wa mhimili wa mahakama, majaji na mahakimu wote huteuliwa na Rais.

Lakini pia bajeti ya mhimili wa mahakama inatolewa na serikali (executive) baada ya kupitishwa na bunge (judiciary), hili nalo kwa mtazamo wangu linachangia kufifisha juhudi za mahakama zetu kuwa huru na kujiamulia mambo yao bila kuingiliwa na mihimili mingine.
 
Mwigulu Nchemba hajui chochote kwenye Sheria! Aache siasa za kijinga kwenye mambo ya msingi ili tu kumfurahisha " Mteuzi " wake!

Anajifanya na maskafu ya Bendera ya Taifa shingoni muda wote ,eti uzalendo ! na hili la kubadili Sheria ziwe kwa Kiswahili eti uzalendo wakati anasomesha watoto wake FEZA SCHOOLS ambako usikute analipa milioni 5 mpaka 7 kwa mtoto wa Primary school!

Danganyeni " wanyonge" mliozoea kuwadanganya!

Tatizo la haki katika Sheria zetu haliko katika Lugha bali liko katika contents ( maudhui)!

Hata hivyo ni aibu kuwa na Waziri wa Sheria asiyejua chochote katika Sheria!
Hii inawezekana tu hapa Tanzania! Nchi ambayo usishangae hata fundi uchomeleaji ( Welder ) anaweza kufanya kazi ya Udaktari (Utabibu wa binadamu)!
 
Katika nchi yetu kila mwaka huwa tunakuwa na wiki moja ambayo huwa tunaiita ni wiki ya sheria nchini, ambapo tumeianza rasmi tarehe 24/1/2021 na kilele chake kitakuwa tarehe 1/2/2021...
Wamekosa kazi walitegemea kupiga perdiem za kesi za ubunge na udiwani wapinzani wamesusa sasa imekula kwao, hakuna mtu anaimani tena na hizi mahakama zao.
 
Mwigulu Nchemba hajui chochote kwenye Sheria! Aache siasa za kijinga kwenye mambo ya msingi ili tu kumfurahisha " Mteuzi " wake!...
Mahakama zenyewe zimegeuzwa tawi la chama tawala, lugha inatusaidia nini? watu wanawekwa ndani bila sababu za msingi, mbona polisi wanatumia kiswahili kuendesha mambo yao na bado uonevu upo sana tu!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom