Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,185
- 307
Jana kwenye taarifa ya habari kulikuwa na kioja ambapo waziri Gaudencia Kabaka alikuwa anatoa taarifa kwa bosi wake juu ya utendaji wa Machinga Complex. Kwa mtu mwenye madaraka ya waziri kutokuwa na majibu au uwezo wa kutatua matatizo madogo ya mawasiliano na watendaji waliochini yake na kusubiri mpaka ziara ya rais kuelezea changamoto ile ni aibu. Ninaamini mawaziri ndio watu walio karibu zaidi na rais kuliko watu wowote Tanzania, na kama kweli watendaji wa manispaa walikuwa wakaidi kwake alitakiwa aombe msaada kwa waziri mkuu, vile vile inaonekana hakuna atakaloweza kuwasaidia vijana kwa jinsi nilivyomuona