Hivi Manji ana manufaa (anafaidika) gani na Yanga

runyaga

JF-Expert Member
Dec 23, 2013
523
241
Manji amewekeza hela zake nyingi Yanga, kama tunavyojua hakuna mfanyabiashara (Manji akiwa mmoja wapo) wanatengeneza hasara; hawezi kufanya kitu kisicho na faida.
Tumeshuhudia Manji akitoa hela yake nyingi kuigharamikia Yanga ikiwepo kulipa mishahara ya wachezaji na kulipa gharama zote za mechi ya TP Mazembe (japo anadaiwa) bila kuonesha faida anayoipata yanga.

Jana kamfukuza Mfaransa akiyeajiriwa kama mtendaji mkuu, japo yeye anasema hakuwahi kuona kazi yoyote ya kufanya chini ya Yanga yetu.
Ile mi nahisi ulikuwa mchezo wa kisiasa ili kuwadanganya wanachama kwamba sasa Yanga inaenda kuendeshwa kimataifa. Mkataba wake umevunjwa jana na lazima kuna malipo ya kuvunja mkataba.

Hizi gharama zote anazolipa Manji kwa manufaa ya Yanga yeye anafaidika nini?
 
Ni hoja nzuri uliyoianzisha!

kabla yakukujibu hoja yako moja kwa moja ...Nipe nafasi ya kukukosoa katika mtazamo wako ambao nauona si sahihi kabisa.

Kwanza kabisa si wafanyabiashara wote wanaingia kwenye mchezo wa soka kwa malengo makuu ya kutengeneza pesa.

Katika kichwa chako , yakupasa ukubaliane na hilo kwanza! Sasa hapa sidhani kama tutabishana katika hili na kulazimisha kuwa Manji yupo pale kutengeneza faida au kwa mapenzi ya mchezo wa soka pekee.

Tu-Assume kuwa mimi na wewe hatujui uwepo wake pale ni kwa lengo la kujenga faida kwake u lah! kwa sababu (hatu)sijawahi kumsikia akisema alijiunga na Yanga kwa malengo ya kujitengenezea faida kwenye Klabu hiyo.

Ukijaribu kufikiri kwa makini utagundua kuwa hakujiunga Yanga SC kwa lengo la kujipatia faida. Hebu zingatia jitihada za hivi majuzi kutaka akabidhiwe klabu ili aiendeshe kifaida zaidi.(Kama angetaka klabu kuiendesha kifaida basi angeshalifanya jitihada za kutosha kukabidhiwa timu), licha ya kuwa palikuwapo na jitihada hizo hapo awali. Hili linaonyesha kuwa hapo awali hakuwahi kuwa na nia ya kuendesha klabu kwa faida ya upande wake.

Kumbuka:-

Yeye (Manji) si mtu/tajiri wa kwanza Duniani kuenesha klabu kwa malengo ya kutaka faida, kun mifano ya matajiri wenye kujihusisha na soka wakiwa na mapenzi na mchezo tu na wala kutengeneza pesa haijawahi kuwa lengo lililo waendesha kuwekeza pesa kwenye mchezo wa soka.

1. Moïse Katumbi Chapwe (TP Mazembe).
2. Patrice Motsepe (Mamelodi Sundown).
3. Amancio Ortega (Deportivo La Coruna).

Hao ni miongoni wa wawekezaji kwenye michezo ambao ni passion driven investors... kuwekeza kwao hakusukumwi na kupata faida klabuni.
Il huwezi kubisha kuwa they'all bussiness people kwamba itokeapo nafasi ya kibiashara katika passion yao, basi huzifuata na kuzitumia.


HIVYO SIONI KAMA NI KOSA KISHERIA KUWEKEZA KWENYE MCHEZO WA SOKA BILA YA KUWA NA MALENGO YA AWALI YA KUPATA FAIDA.

TUSIMSIMANGE TUMUACHE AYAFANYE YALIYO MEMA MACHONI PA MASHABIKI WA DAR ES SALAAM YOUNG AFRICANS SC.
 
Hela zake Manji wewe mtoto wa kiume unataka kujua anapata faida gani je wakati anazitafuta mbona uendi kumsaidia mawazo? Kitu muhimu tafuta zako halafu uoji utazitumiaje upate faida.
 
Elimu yako ndogo mtoa mada,Manji anatangaza biashara zake,yaani jamaa angu una akili sawa na wale wanywa ghahawa wa vijiweni.
 
Hao uliowataja ni wamiliki wa hizo timu. Manji anamiliki Yanga?
Hao kasema Ni wawekezaji so kumiliki Ni kewekeza,kununua hisa Ni kuwekeza hats kukodisha PIA nako Ni kuwekeza,tatizo lenu mikia kupiga kelele Tu timu ikiyumba kidogo stress kibao hadi mnatukana ovyo,poleni yanga mbele kwa mbele
 
Elimu yako ndogo mtoa mada,Manji anatangaza biashara zake,yaani jamaa angu una akili sawa na wale wanywa ghahawa wa vijiweni.
nadhani ungenijibu ivo bila matusi ningeelewa vizuri zaidi make ndo kitu nilitaka kujua.
 
Manji amewekeza hela zake nyingi Yanga, kama tunavyojua hakuna mfanyabiashara (Manji akiwa mmoja wapo) wanatengeneza hasara; hawezi kufanya kitu kisicho na faida.
Tumeshuhudia Manji akitoa hela yake nyingi kuigharamikia Yanga ikiwepo kulipa mishahara ya wachezaji na kulipa gharama zote za mechi ya TP Mazembe (japo anadaiwa) bila kuonesha faida anayoipata yanga.

Jana kamfukuza Mfaransa akiyeajiriwa kama mtendaji mkuu, japo yeye anasema hakuwahi kuona kazi yoyote ya kufanya chini ya Yanga yetu.
Ile mi nahisi ulikuwa mchezo wa kisiasa ili kuwadanganya wanachama kwamba sasa Yanga inaenda kuendeshwa kimataifa. Mkataba wake umevunjwa jana na lazima kuna malipo ya kuvunja mkataba.

Hizi gharama zote anazolipa Manji kwa manufaa ya Yanga yeye anafaidika nini?
Manji anapata faida kubwa sana akiwa amewekeza pale Yanga. Kumbuka faida siyo lazima iwe tangible inaweza kuwa intangible. Hebu nijibu, unapata faida kiasi gani unapofanya mapenzi na mpenzi wako? Bila shaka kuna utamu usiopimika unaupata, au siyo?

Baada ya kutafakari jibu lako hapo juu, sasa ngoja nikupe mifano mingine: Yanga inapochukua ubingwa Manji hujisikia raha sana na pindi Yanga inapoifunga mikia fc Manji hujisikia raha isiyo na kifani (hii ni faida kubwa ambayo ni intangible).

Go go go Manji.
 
Manji anapata faida kubwa sana akiwa amewekeza pale Yanga. Kumbuka faida siyo lazima iwe tangible inaweza kuwa intangible. Hebu nijibu, unapata faida kiasi gani unapofanya mapenzi na mpenzi wako? Bila shaka kuna utamu usiopimika unaupata, au siyo?

Baada ya kutafakari jibu lako hapo juu, sasa ngoja nikupe mifano mingine: Yanga inapochukua ubingwa Manji hujisikia raha sana na pindi Yanga inapoifunga mikia fc Manji hujisikia raha isiyo na kifani (hii ni faida kubwa ambayo ni intangible).

Go go go Manji.
asante sana mkuu, umenipa mwanga kidogo
 
Back
Top Bottom