Hivi Makonda hana kipaji cha kushawishi hadi atumie pesa?

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,272
47,268
Makonda ameahidi kutoa mil. 10, kwa mwalimu, ambaye wanafunzi wake watafanya vizuri.

Makonda ameahidi kutoa zawadi ya gari aina ya Nissan Pick Up kwa Mwenyekiti wa Mtaa pamoja na pesa kwa wajumbe ambao mtaa wao utaongoza kwa usafi.

Makonda atangaza zawadi ya Milioni 1 kwa askari polisi atakayepambana na jambazi na kulishinda.

Makonda ameahidi kugawa pikipiki kwa bodaboda kwa marejesho ya sh. 25,000 kwa wiki.

Paul Makonda awapambanisha Christian Bella na Banana Zoro Kwa Mil 50 kila mmoja.

Makonda ameahidi kujenga makao makuu ya bakwata kwa bilioni 5 na milioni 80.

Makonda ameahidi mil. 100 kuwajengea viwanda machinga.

Makonda ameahidi pesa......

Mbali ya kuhoji anapozipata, hivi ndio kusema hana uwezo kabisa wa kushawishi wananchi kujiletea maendeleo yao hadi atumie pesa?

Najiuliza tu.
 
Ndiyo uone kuwa hawa watu ufisadi na njia za mkato ndiyo pumzi yao ya uhai.
Nadhani Mange Kimambi atakuwa anajua anazipataje hizo hela.
 
Kamati ya maadili imchunguze na kumpeleka kwenye mahakama ya mafisadi kuna mambo mawili yule anayempongezakwamba mchapa kazi anampa hela toka hazina maana tunasikia anagawa mwenyewe au mafisadi home shopping centre wakwepa kodi aka GSMwanamumwagia mapesa waendelee kuibia nchi
 
Kipaji ni karama huwezi pata kipaji kwa kutafuta kama vile kupata degree kwa kusoma
 
Ndio maana DC wake Polepole akawa anamdharau akiacha walambane midomo na yule wa aina yake Hapi. Style hiyo mwenye upeo atakudharau ila mwenye nanihii atakupongeza
 
fika kituo cha polisi kilicho karibu ujisalimishe kwa kumtukana mungu wa dsm mkuu, unasema hana convicing power bila pesa???
 
Si kama mgombea fulani wa urais
Yeye hata kuongea hawezi anaamini pesa ndiyo kila kitu
Matokeo yake watu wakala pesa
Urais wakamnyima
 
Tuache kuwa na mawazo mkando watu wanapesa mjini nyingi tu sema ni jinsi gani wewe kama kiongozi unaweza kuwashawish waweze kukusaidia ili utimize lengo lako katika kuwasaidia wananchi wako sabodo alikuwa anamwaga pesa chama kimoja hivi tulihoji hicho chama kinapate pesa hapa namkumbuka mzee wa msoga alisha wahi kusema huko duniani pesa zipo nyingi ni wewe ujue jinsi ya kuzichangamkia ili uzipate nashauri na meya wa jiji nae kama angekuwa kama makonda naona dar ingekuwa mbali
 
Tuache kuwa na mawazo mkando watu wanapesa mjini nyingi tu sema ni jinsi gani wewe kama kiongozi unaweza kuwashawish waweze kukusaidia ili utimize lengo lako katika kuwasaidia wananchi wako sabodo alikuwa anamwaga pesa chama kimoja hivi tulihoji hicho chama kinapate pesa hapa namkumbuka mzee wa msoga alisha wahi kusema huko duniani pesa zipo nyingi ni wewe ujue jinsi ya kuzichangamkia ili uzipate nashauri na meya wa jiji nae kama angekuwa kama makonda naona dar ingekuwa mbali
Kama kiongozi sio mbunifu hata agawe pesa kila siku hawezi kuleta maendeleo zitaishia midomoni kama za tasaf.
 
Makonda ameahidi kutoa mil. 10, kwa mwalimu, ambaye wanafunzi wake watafanya vizuri.

Makonda ameahidi kutoa zawadi ya gari aina ya Nissan Pick Up kwa Mwenyekiti wa Mtaa pamoja na pesa kwa wajumbe ambao mtaa wao utaongoza kwa usafi.

Makonda atangaza zawadi ya Milioni 1 kwa askari polisi atakayepambana na jambazi na kulishinda.

Makonda ameahidi kugawa pikipiki kwa bodaboda kwa marejesho ya sh. 25,000 kwa wiki.

Paul Makonda awapambanisha Christian Bella na Banana Zoro Kwa Mil 50 kila mmoja.

Makonda ameahidi kujenga makao makuu ya bakwata kwa bilioni 5 na milioni 80.

Makonda ameahidi mil. 100 kuwajengea viwanda machinga.

Makonda ameahidi pesa......

Mbali ya kuhoji anapozipata, hivi ndio kusema hana uwezo kabisa wa kushawishi wananchi kujiletea maendeleo yao hadi atumie pesa?

Najiuliza tu.
Najua hakuna mtu wa cdm anayeweza SIFIA AU KUPONGEZA jitihada zaMakonda juu ya bodaboda coz ulikuwa mtaji mkubwa wa cdm kwa Dar ila kwa speed hii 2020 LAZIMA MAJIMBO yote Dar yarudi pia ili ndio tatizo letu kubwa Watanzania la kumpinga mtu mwenye nia ya dhati na mitazamo chanya ya kusaidia jamii,,sio kila ahadi mzazi anayotoa kwa mwanae ili afanye vizuri ama shuleni au popote uwa tunatekeleza kwa 100% so mwacheni kijana afanye kazi
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom