Hivi maisha kwenye nchi za kiarabu mfano Iraqi, Afghanistan, Syria etc huwa yakoje?

kyagata

JF-Expert Member
Oct 18, 2016
6,495
12,591
Hivi na huko watu huwa wanalala wanapata usingizi kama hapa kwetu Tanzania?
Watu huwa wanakaa vijiweni kama huku kwetu na kupiga story? Wanafunzi wanaenda shule? Viongozi wa Serikali wanaheshimiwa? Watu wanapendana kama hapa kwetu bongo?
Kuna mtu huko asiyemiliki bunduki au mabomu?
 
Kijana tembea uone. Maisha unayoyaona kwenye CNN na TV channels nyinginezo...ni tofauti na uhalisia. Mfano Iraq ni middle income country. Mwaka huu bajeti yao ni zaidi ya dola billion 90! Hiyo ni bajeti tuu.......Ingawa imekuwa nchi ya vita toka Uhuru! GDP ya Tanzania ni billion 55! Ukweli ni kwamba, hivi vita mara nyingi ni hujuma za wanaharamu wa magharibi wanaotaka kurudisha nyuma wenzao.

Umeshawahi kusikia Iraq ina import chakula? Ingawa maisha yao yote wamekuwa vitani? kabla ya vita mfanya kazi wa ndani Syria alikuwa anakwenda kazini na gari yake!

Africa tutafuta namna ya kujiongeza. Hakuna namna.
 
Mmh ngoja wazee wa kimataifa waje kutujuza
Mimi nina experience ya kwenye movie na series tu
 
Swali kama hili nadhani litakuwa limeulizwa na mtoto wa mwisho wa mwenye ID.
 
Tatizo vyombo vya habari vingi kuhusu mashariki yakati vinaoneshaga mabaya yake ila mazur yake hapana. mfano swala kama umaskin na ugonjwa wa ukimwi nchi kama zile huwa wanatushangaa sisi tunaezaje kuish na matatzo hayo hali sis tuna angalia vita vyao. so wamezoea hali zao
 
Kijana tembea uone. Maisha unayoyaona kwenye CNN na TV channels nyinginezo...ni tofauti na uhalisia. Mfano Iraq ni middle income country. Mwaka huu bajeti yao ni zaidi ya dola billion 90! Hiyo ni bajeti tuu.......Ingawa imekuwa nchi ya vita toka Uhuru! GDP ya Tanzania ni billion 55! Ukweli ni kwamba, hivi vita mara nyingi ni hujuma za wanaharamu wa magharibi wanaotaka kurudisha nyuma wenzao.

Umeshawahi kusikia Iraq ina import chakula? Ingawa maisha yao yote wamekuwa vitani? kabla ya vita mfanya kazi wa ndani Syria alikuwa anakwenda kazini na gari yake!

Africa tutafuta namna ya kujiongeza. Hakuna namna.
Acha kujifariji mabomu uchwao inataka kusema CNN wanasema uongo
 
Wamejaaliwa nishati ya mafuta ndio umekuwa mkosi kwao wamekalia ushia na usuni na kugombana..mara nyingine ukijaaliwa utajiri wa madini ni laana fulani.
 
nilikuwa kwenye conference somwhere, nikakutana na mafghan, anakaa kabul na anafanya kazi kabul university, kwa kifupi life linasonga kama kawa ila mabomu/milipuko wanayasikia na life linaendelea
 
Kijana tembea uone. Maisha unayoyaona kwenye CNN na TV channels nyinginezo...ni tofauti na uhalisia. Mfano Iraq ni middle income country. Mwaka huu bajeti yao ni zaidi ya dola billion 90! Hiyo ni bajeti tuu.......Ingawa imekuwa nchi ya vita toka Uhuru! GDP ya Tanzania ni billion 55! Ukweli ni kwamba, hivi vita mara nyingi ni hujuma za wanaharamu wa magharibi wanaotaka kurudisha nyuma wenzao.

Umeshawahi kusikia Iraq ina import chakula? Ingawa maisha yao yote wamekuwa vitani? kabla ya vita mfanya kazi wa ndani Syria alikuwa anakwenda kazini na gari yake!

Africa tutafuta namna ya kujiongeza. Hakuna namna.
naomba unipe life experience ya huko mkuu.me nimeuliza kulingana ninayoyaona huko CNN na BBC
 
Back
Top Bottom