Hivi Magufuli na Lugola wanataka wapigiwe ngoma gani ndio wajue suala la vitambulisho ni tatizo kubwa nchini linasumbua sana watu?

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Mie nashindwa kuelewa. Kila siku nasoma na kusikia matatizo lukuki ambayo watu wanapata kuhusiana na suala la vitambulisho vya taifa. Na tatizo limefanywa kubwa zaidi kwa sababu kwa sasa vitambulisho vya taifa vimeunganishwa na utolewaji wa passport, usajiri wa kampuni, kupata TIN nk.

Kuna watu tumekaa zaidi ya miaka miwili tangu tuwakilishe maombi lakini na kuchukuliwa alama za vidole na bado hatujapata vitambulisho. Watu wamepoteza nafasi za maisha kama kusajiri biashara au kwenda nje masomoni kwa ajili tu ya kutokuwa na kitambuisho cha taifa. Watu wa diaspora kila siku wanalia vitambulisho vya taifa.

Sasa huyu Raisi Magufuli na Waziri wake Lugola, wanataka wapigiwe ngoma gani ili wasikie kilio cha Watanzania kuhusu vitambulisho vya taifa? Hivi katika kufikiri kwao wameona hili sio suala muhimu jambo linaleta usumbufu sana kwa kwa Watanzania?

Kwa nini mnaanzisha mambo makubwa bila kujipanga, huo sio uzembe mnaotaka Watanzania tuondokane nao?
 
Nina uhakika hata wachangiaji humu JF wamechoka kuchangia kuhusu karaha wanazopata kuhusu vitambulisho vya taifa, tumesema sana na hakna cha kusema tena!:rolleyes::rolleyes::rolleyes:

Mara nyingine you just wish uwapate hawa viongozi wa NIDA utandike wote fimbo za makalio, labda watachangamka baada ya hapo. Ikiwezekana hata bosi wao mkuu - viboko vya makalio na kumwambia aende wajipange upya.
 
Tunaposhindwa kusimamia miradi kama hii ya vitambulisho vya taifa, ardhi kupima na kugawa maeneo( mipango miji), kuboresha ubora wa elimu yetu na Huduma ya afya, miradi ya usafirishaji kama udart, kwa kweli ninapata wasi wasi kama serikali yetu itaweza kusimamia miradi sophiscated kama SGR, ATCL au ata kufikia kwenye uchumi wa viwanda.

Sijui kama nitakosea nikisema ukiona kampuni au shirika au nchi au taasisi yoyote inafanya vizuri basi jua pale juu kuna kiongozi mzuri.
 
Niliandika barua kwensa NIDA kuomba kitambulisho kwaajili ya passport eti leo nimeenda badala ya kunipa kitambulisho wananipa barua ya kupeleka uhamiaji.......nchi haina serikali.
 
Mie nashindwa kuelewa. Kila siku nasoma na kusikia matatizo lukuki ambayo watu wanapata kuhusiana na suala la vitambulisho vya taifa. Na tatizo limefanywa kubwa zaidi kwa sababu kwa sasa vitambulisho vya taifa vimeunganishwa na utolewaji wa passport.

Kuna watu tumekaa zaidi ya miaka miwili tangu tuwakilishe maombi lakini na kuchukuliwa alama za vidole na bado hatujapata vitambulisho. Watu wamepoteza nafasi za maisha kama kwenda nje masomoni kwa ajili tu ya kutokuwa na kitambuisho cha taifa. Watu wa dispora kila siku wanalia vitambulisho vya taifa.

Sasa huyu Raisi Magufuli na Waziri wake Lugola, wanataka wapigiwe ngoma gani ili wasikie kilio cha Watanzania kuhusu vitambulisho vya taifa? Hivi katika kufikiri kwao wameona hili sio suala muhimu jambo linaleta usumbufu sana kwa kwa Watanzania?

Kwa nini mnaanzisha mambo makubwa bila kujipanga, huo sio uzembe mnaotaka Watanzania tuondokane nao?
Ni kweli mkuu hili ni tatizo,tena kubwa.Nashauri kama tatizo ni watendaji waondolewe wapewe wenye weledi na moyo wa kuwatumikia Watanzania ili swala la vitambulisho vya taifa ibaki kuwa historia.Or else litoke tamko rasmi,kwamba taasisi yeyote isidai kitambulisho cha taifa, mpaka hapo kila Mtanzania atakapokuwa amepata.Kwa jinsi mambo yalivyo sasa,it's true ni kero,na swala la vitambulisho vya taifa bado ni ngoma mbichi..Nadhani ifike mahali Wa-TZ tuonyeshe seriousness kwenye serious issues.

Hivi kwa nini tuliligongomoa hili swala la vitambulisho kama tulijua hatuna resources za kutosha za kulimaliza?Kuna a reasonable answer kweli,I doubt it.
 
Nina uhakika hata wachangiaji humu JF wamechoka kuchangia kuhusu karaha wanazopata kuhusu vitambulisho vya taifa, tumesema sana na hakna cha kusema tena!:rolleyes::rolleyes::rolleyes:

Mara nyingine you just wish uwapate hawa viongozi wa NIDA utandike wote fimbo za makalio, labda watachangamka baada ya hapo. Ikiwezekana hata bosi wao mkuu - viboko vya makalio na kumwambia aende wajipange upya.
Ningekuwa mi raisi ningetandika ofisi zote za NIDA viboko kumi na hamsa kila mmoja ili watie akili, wamezidi uzembe, mi hadi leo sijapata ID ya taifa hadi siwezi kupiga mishe za kikampuni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali ipo ila labda haina hela za kuchapishia vitambulisho vya Uraia. Sasa uwe unataka kusajili Kampuni Brela na huna hicho kitambulisho... Utaelewa kwamba mbwembwe za Jogoo kuwika hakufanyi kuche mapema.
Mi nimekwamia hapo, sina ID ya taifa so siwezi kufanya usajiri wowote nimekaa tu napoteza muda,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu wao hawajali wala nini.
Nadhani hawajawahi kujali, inaonekana hili swala km lina mkono wa mtu mkubwa maana hawawajibishani wala nini, kuna mtu anakiburi so wananung'unika tu kimya kimya, watu lukuki mambo yamesimama kwa kitambulisho cha taifa ila wao wanachill tu wanaenda ofisini na kurudi nyumbani wanalipwa mishahara mwisho wa mwezi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana mkuu, Nakumbuka nilienda kukata TIN number mwaka 2017 mahali fulani, basi wakataka national ID nikawapa wakashangaa,
Maana katika watu wote pale ni Mimi tuu ndo nilikua na kitambulisho cha taifa, Mimi nilikipata wakati nipo chuo hakika nilibahatika
Hiki kutambulisho kimenifanya nishindwe kupata mkopo wa biashara jaman yani hapa nimechokaje daahh, wakuu wa nchi wapo bize na vitambulisho vya ujasiriamali

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niliandika barua kwensa NIDA kuomba kitambulisho kwaajili ya passport eti leo nimeenda badala ya kunipa kitambulisho wananipa barua ya kupeleka uhamiaji.......nchi haina serikali.
Mkuu, hiyo barua ya kwenda uhamiaji inasemaje, labda itakuruhusu kupewa passport bila kitambulisho.
 
Pole sana mkuu, Nakumbuka nilienda kukata TIN number mwaka 2017 mahali fulani, basi wakataka national ID nikawapa wakashangaa,
Maana katika watu wote pale ni Mimi tuu ndo nilikua na kitambulisho cha taifa, Mimi nilikipata wakati nipo chuo hakika nilibahatika

Sent using Jamii Forums mobile app
Nasikia kuna watu wanakipata ndani ya mwezi mmoja. Hapo ndio nashindwa kuelewa kabisa.
 
Mie nashindwa kuelewa. Kila siku nasoma na kusikia matatizo lukuki ambayo watu wanapata kuhusiana na suala la vitambulisho vya taifa. Na tatizo limefanywa kubwa zaidi kwa sababu kwa sasa vitambulisho vya taifa vimeunganishwa na utolewaji wa passport, usajiri wa kampuni, kupata TIN nk.

Kuna watu tumekaa zaidi ya miaka miwili tangu tuwakilishe maombi lakini na kuchukuliwa alama za vidole na bado hatujapata vitambulisho. Watu wamepoteza nafasi za maisha kama kusajiri biashara au kwenda nje masomoni kwa ajili tu ya kutokuwa na kitambuisho cha taifa. Watu wa diaspora kila siku wanalia vitambulisho vya taifa.

Sasa huyu Raisi Magufuli na Waziri wake Lugola, wanataka wapigiwe ngoma gani ili wasikie kilio cha Watanzania kuhusu vitambulisho vya taifa? Hivi katika kufikiri kwao wameona hili sio suala muhimu jambo linaleta usumbufu sana kwa kwa Watanzania?

Kwa nini mnaanzisha mambo makubwa bila kujipanga, huo sio uzembe mnaotaka Watanzania tuondokane nao?
Siku hizi hata ukirenew driving license tu inapita miezi kadhaa mpk kupata. Kero sana.
 
Back
Top Bottom