ruaharuaha
JF-Expert Member
- Feb 14, 2018
- 3,554
- 3,749
Nieleweshe? Siku zote unaanza kusaidia ndugu zako, jirani, watu kama wewe.
Of course ukiwa tajiri mkumbwa una uwezo zaidi wa kuwasaidia watu wengine, wengi duniani.
Kwani usichoelewa ni nini? Hivi we kwa akili yako mzungu bepari akupe hela ya bure (msaada) kwani we ni mwana wao? Iko hivi kwa kila sh moja wanayokupa wao wanapata sh mbili na zaidi. Juzi Bill Gates kasema use billions to save trillions! Kwa ufupi ni kwamba hao wazungu hata watoto wao waliotoka viunoni mwao hawawapi pesa ya bure wakishafikia umri fulani. Wakupe wewe kwani we ni nani?Hijui serikali yako inapanga Bajeti inayotegemea hela za wahisani miaka 60 baada ya uhuru?
Na barabara, hospitali, shule (elimu), kuzuia Rushwa, nidhamu serikalini, kuondoa ukiritimba. Huduma chap chap.Unahitaji vitu vitatu tu kupata maendeleo kwa kasi: mifumo ya Reli, Umeme wa kutosha na kilimo bora.
Magufuli akijaribu kufanya hayo nyie ndo wakwanza kupinga. Nyie pamoja na vizazi vyenu mtamshukuru JPM kwa reli ya SGR na Nyerere hydropower station.
Unajua maana ya kujitolea lakini?Kwanini tusizipokee sisi ambapo wakiwa wakimbizi ndio tutakaoathirika zaidi?
Unajua wangapi wamekufa, maisha ya vijana cut short.
Maisha ya wanajeshi, vijana wetu unaweza kuyawekea thamani gani?
Tunajitolea maisha yetu, ya vijana wetu kuwalinda.
Basi mpe wewe huyo mzungu bepari pesa bila mashartiKwani usichoelewa ni nini? Hivi we kwa akili yako mzungu bepari akupe hela ya bure (msaada) kwani we ni mwana wao? Iko hivi kwa kila sh moja wanayokupa wao wanapata sh mbili na zaidi. Juzi Bill Gates kasema use billions to save trillions! Kwa ufupi ni kwamba hao wazungu hata watoto wao waliotoka viunoni mwao hawawapi pesa ya bure wakishafikia umri fulani. Wakupe wewe kwani we ni nani?
Huo unaouita msaada si msaada kama unavyofikiria. Kwa uchumi waliofikia (ukizingatia pia sehemu ya uchumi wao inategemea nchi zinazoitwa maskini za Afrika) ni faida kwao kurejesha kiasi katika nchi zinakotoka malighafi za uchumi wao.