Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,985
- 144,312
Ukweli ni kwamba, nchi zetu hizi zinazoendelea, hasa hizi za Afrika, hazipigi hatua kubwa kimaendeleo na kuondokana na umasikini kutokana na mambo kama rushwa, ubinafsi wa viongozi, kukosekana kwa utawala bora, demokrasia,katiba mbovu,vipaumbele vibovu, n.k. huku chanzo kikuu kikiwa ni nchi nyingi za kiafrika kuwa na watawala wabovu.
Ushahidi wa hili ni uwepo wa baadhi ya nchi za Asia zilizopata uhuru katika miaka ambayo nchi nyingi za kiafrika nazo zilikuwa zinapata uhuru ila leo ziko mbali sana kimaendeleo mfano, Malaysia, Singapore,n.k.
Sasa najiuliza, kama Magufuli angekuwa ni Rais katika mojawapo ya Nchi Wahisani, angekubali kuendelea kutoa misaada kwa hizi nchi masikini au angezisimanga kwa maneno makali kuwa zinaendekeza umasikini na hivyo nchi yake isingetoa misaada?
Nawaza sana.
Ushahidi wa hili ni uwepo wa baadhi ya nchi za Asia zilizopata uhuru katika miaka ambayo nchi nyingi za kiafrika nazo zilikuwa zinapata uhuru ila leo ziko mbali sana kimaendeleo mfano, Malaysia, Singapore,n.k.
Sasa najiuliza, kama Magufuli angekuwa ni Rais katika mojawapo ya Nchi Wahisani, angekubali kuendelea kutoa misaada kwa hizi nchi masikini au angezisimanga kwa maneno makali kuwa zinaendekeza umasikini na hivyo nchi yake isingetoa misaada?
Nawaza sana.