Dickson Ng'hily
JF-Expert Member
- Oct 22, 2010
- 451
- 485
Ndugu zangu wana JF, taarifa ya uongozi wa kampuni ya Africa Media Group ambao ndio wanamiliki wa Kituo cha Televisheni cha Channel 10 wa kuitaka Serikali kuanzisha uchunguzi huru ili kubaini sababu na mazingira ya kuuawa kwa mwandishi Daudi Mwangosihuyo ni ya kuungwa mkono....
Hata hivyo iliniuma zaidi pale Mhariri Mkuu wa Channel Ten, Dina Chahalimbaye kusema kuwa Mrehemu hakuwa mwajiliwa wa kituo hicho..Alikuwa na maana gani hapa? Hivi kweli toka mwaka 2006 mpaka leo hawakuwa wamempatia ajira Mwanahabari huyu? Hivi ni mpaka lini Channel 10 na vyombo vingine vya habari vitakujatoa ajira rasmi kwa watu wao? Mwangosi amekumbwa na umauti akiwa kazini sasa anaposema hakuwa mwajiriwa wa Channel 10, Je! Ndo kusema hakutakuwa na malipo yeyote kwa familia?
Maskini Mwangosi, naandika kwa uchungu sana ndugu yangu, hivi ni nani leo ataiangalia familia yako? Ni nani atachukua jukumu la kusomesha watoto wako! Kama Channel 10 ingekuwa imekuajiri basi walau NSSF yako ingesaidia..Watoto na Mke wako wanalia, wanalia kwa sababu hawatakuona tena, wanalia kwa sababu hawatapata mapenzi yako tena, wanalia kwa sababu bread winner wao hayupo tena...Wanaangalia maisha mbele, hawaoni tumaini lolote, ni giza totoro....hawajui sasa maisha yataendaje...Eeeeh mwenyezi Mungu isaidie hii familia...
Hata hivyo iliniuma zaidi pale Mhariri Mkuu wa Channel Ten, Dina Chahalimbaye kusema kuwa Mrehemu hakuwa mwajiliwa wa kituo hicho..Alikuwa na maana gani hapa? Hivi kweli toka mwaka 2006 mpaka leo hawakuwa wamempatia ajira Mwanahabari huyu? Hivi ni mpaka lini Channel 10 na vyombo vingine vya habari vitakujatoa ajira rasmi kwa watu wao? Mwangosi amekumbwa na umauti akiwa kazini sasa anaposema hakuwa mwajiriwa wa Channel 10, Je! Ndo kusema hakutakuwa na malipo yeyote kwa familia?
Maskini Mwangosi, naandika kwa uchungu sana ndugu yangu, hivi ni nani leo ataiangalia familia yako? Ni nani atachukua jukumu la kusomesha watoto wako! Kama Channel 10 ingekuwa imekuajiri basi walau NSSF yako ingesaidia..Watoto na Mke wako wanalia, wanalia kwa sababu hawatakuona tena, wanalia kwa sababu hawatapata mapenzi yako tena, wanalia kwa sababu bread winner wao hayupo tena...Wanaangalia maisha mbele, hawaoni tumaini lolote, ni giza totoro....hawajui sasa maisha yataendaje...Eeeeh mwenyezi Mungu isaidie hii familia...