Hivi kweli toka 2006 Daudi Mwangosi hajapewa ajira ya channel 10?

Dickson Ng'hily

JF-Expert Member
Oct 22, 2010
451
485
Ndugu zangu wana JF, taarifa ya uongozi wa kampuni ya Africa Media Group ambao ndio wanamiliki wa Kituo cha Televisheni cha Channel 10 wa kuitaka Serikali kuanzisha uchunguzi huru ili kubaini sababu na mazingira ya kuuawa kwa mwandishi Daudi Mwangosihuyo ni ya kuungwa mkono....

Hata hivyo iliniuma zaidi pale Mhariri Mkuu wa Channel Ten, Dina Chahalimbaye kusema kuwa Mrehemu hakuwa mwajiliwa wa kituo hicho..Alikuwa na maana gani hapa? Hivi kweli toka mwaka 2006 mpaka leo hawakuwa wamempatia ajira Mwanahabari huyu? Hivi ni mpaka lini Channel 10 na vyombo vingine vya habari vitakujatoa ajira rasmi kwa watu wao? Mwangosi amekumbwa na umauti akiwa kazini sasa anaposema hakuwa mwajiriwa wa Channel 10, Je! Ndo kusema hakutakuwa na malipo yeyote kwa familia?

Maskini Mwangosi, naandika kwa uchungu sana ndugu yangu, hivi ni nani leo ataiangalia familia yako? Ni nani atachukua jukumu la kusomesha watoto wako! Kama Channel 10 ingekuwa imekuajiri basi walau NSSF yako ingesaidia..Watoto na Mke wako wanalia, wanalia kwa sababu hawatakuona tena, wanalia kwa sababu hawatapata mapenzi yako tena, wanalia kwa sababu bread winner wao hayupo tena...Wanaangalia maisha mbele, hawaoni tumaini lolote, ni giza totoro....hawajui sasa maisha yataendaje...Eeeeh mwenyezi Mungu isaidie hii familia...

 
Hivi hiki kituo kinamilikiwa na nani? Ha ha ha ha ha! Kwa kadhia hii don't be surprised kuambiwa ni Chadema. Hapa hakuna jinsi ya kukwepa kujadili watu na matukio badala ya masuala. I am very sory for that.
 
Ushauri Kwako Dickson-ng-hily

Na wewe jiulize tokea umejiunga JF (22 Oct 2010) umetoa mchango gani kwa kuimarisha chama TEMEKE?

Naona muda mwingi huku online, Get out imarisha Chama Temeke
 
Last edited by a moderator:
Jana huyo mdada msemaji wa chanel ten,alikuwa akihojiwa na dw kweli alikuwa anajiumauma sana maana hata chanel ten wamemdhulum haki nyingi sana mwangosi kumfanya part time for 6yrs!!!!ina maana ndani ya miaka sita hiyo hawajaajili???ubaguzi na uonevu mkubwa,na hii si kwa mwangosi ila kuna watu kibao ni part time mda mrefu,mfumo ulishaharibika ubaguzi kila sehemu,waajili wetu wako juu ya sheria,wapenda rushwa,na ndio maana ukihoji suala lolote kuhusu haki zako kwa mwajili,unakuwa unajenda uadui,yote hii ni mfumo kandamizi na onevu,wa magamba.
 
Ndugu zangu wana JF, taarifa ya uongozi wa kampuni ya Africa Media Group ambao ndio wanamiliki wa Kituo cha Televisheni cha Channel 10 wa kuitaka Serikali kuanzisha uchunguzi huru ili kubaini sababu na mazingira ya kuuawa kwa mwandishi Daudi Mwangosihuyo ni ya kuungwa mkono....

Hata hivyo iliniuma zaidi pale Mhariri Mkuu wa Channel Ten, Dina Chahalimbaye kusema kuwa Mrehemu hakuwa mwajiliwa wa kituo hicho..Alikuwa na maana gani hapa? Hivi kweli toka mwaka 2006 mpaka leo hawakuwa wamempatia ajira Mwanahabari huyu? Hivi ni mpaka lini Channel 10 na vyombo vingine vya habari vitakujatoa ajira rasmi kwa watu wao? Mwangosi amekumbwa na umauti akiwa kazini sasa anaposema hakuwa mwajiriwa wa Channel 10, Je! Ndo kusema hakutakuwa na malipo yeyote kwa familia?

Maskini Mwangosi, naandika kwa uchungu sana ndugu yangu, hivi ni nani leo ataiangalia familia yako? Ni nani atachukua jukumu la kusomesha watoto wako! Kama Channel 10 ingekuwa imekuajiri basi walau NSSF yako ingesaidia..Watoto na Mke wako wanalia, wanalia kwa sababu hawatakuona tena, wanalia kwa sababu hawatapata mapenzi yako tena, wanalia kwa sababu bread winner wao hayupo tena...Wanaangalia maisha mbele, hawaoni tumaini lolote, ni giza totoro....hawajui sasa maisha yataendaje...Eeeeh mwenyezi Mungu isaidie hii familia...


Dickson, navyofahamu Marehemu alikuwa analipwa na Channel Ten kwa mkataba wa jinsi anavyoreport story... hilo si geni kabisa katika Uandishi wa Habari na sector zingine kama Afya, Ufundishaji hasa wa Vyuo Vikuu na wengi wanafanya Bongo na Duniani.

Na wakati mwingine Unaweza kufaidika zaidi kama ukiwa Unalipwa kwa style hii na Mtu anakuwa huru sana kufanya mambo binafsi kuliko kuwa mwajiriwa. Kuhusu NSSF, unaweza kuwa Mwanachama na Kufaidi mafao yote hata kama sio Mwajiriwa....
 
Ndugu zangu wana JF, taarifa ya uongozi wa kampuni ya Africa Media Group ambao ndio wanamiliki wa Kituo cha Televisheni cha Channel 10 wa kuitaka Serikali kuanzisha uchunguzi huru ili kubaini sababu na mazingira ya kuuawa kwa mwandishi Daudi Mwangosihuyo ni ya kuungwa mkono....

Hata hivyo iliniuma zaidi pale Mhariri Mkuu wa Channel Ten, Dina Chahalimbaye kusema kuwa Mrehemu hakuwa mwajiliwa wa kituo hicho..Alikuwa na maana gani hapa? Hivi kweli toka mwaka 2006 mpaka leo hawakuwa wamempatia ajira Mwanahabari huyu? Hivi ni mpaka lini Channel 10 na vyombo vingine vya habari vitakujatoa ajira rasmi kwa watu wao? Mwangosi amekumbwa na umauti akiwa kazini sasa anaposema hakuwa mwajiriwa wa Channel 10, Je! Ndo kusema hakutakuwa na malipo yeyote kwa familia?

Maskini Mwangosi, naandika kwa uchungu sana ndugu yangu, hivi ni nani leo ataiangalia familia yako? Ni nani atachukua jukumu la kusomesha watoto wako! Kama Channel 10 ingekuwa imekuajiri basi walau NSSF yako ingesaidia..Watoto na Mke wako wanalia, wanalia kwa sababu hawatakuona tena, wanalia kwa sababu hawatapata mapenzi yako tena, wanalia kwa sababu bread winner wao hayupo tena...Wanaangalia maisha mbele, hawaoni tumaini lolote, ni giza totoro....hawajui sasa maisha yataendaje...Eeeeh mwenyezi Mungu isaidie hii familia...


Rai yangu kwa wote wanaoua watu (mtu mmoja mmoja, gang, serikali) waache kabisa kwani ni kutumbukiza familia zao kwenye umasikini ulio kithiri kwa ghafla mno. Hizi habari za tulikuwa tunapambana na majambazi, tulikuwa tunatuliza ghasia sio za msingi kabisa. Kuuwa bread winner ni sawa na kuua familia yake passively.
 
kwanza RIP DAUD MWANGOSI
jamani hawa Waandishi wanatafuta habari na kuzituma ni mpaka ikubaliwe ndio analipwa kwani huko kwenye vyombo vya habari nako kuna kuchuja. Ndio maana utaona habari uliyoiona au picha zinarudiwa katika kituo kingine.
Wanachofanya, hata wewe sio lazima uwe Kanjanja fuma tukio, piga picha labda Jengo linaanguka,au Bomu linapigwa hiyo picha ilinde na utaiuza vizuri ha Al-Jazeera na Channel 10 hawatakuzuia.
Hizi picha zote za tukio la Nyalolo la mabomu aliyepiga picha hana habari km zimesambaa Dunia nzima hivyo hawezi dai ni zake au za ITV kwa sababu walienda waandishi 8 kweny tukio wakarudi 6
Channel 10 km wamemwajiri watalazimika kumlipa BIMA ya kuwa kazini akiwachukulia picha, NSSF na masurufu kibao ndio maana nasema sasa hivi usalama kazini sio kwa MaDr tu hata wafanyakazi wengine
 
MMh haata si elewi nasikia kizunguzungu tuu na huyu mama Dinah alilisema kwa ufasaha kujivua mzigo mapemaaaa,jamani
 
kwanza RIP DAUD MWANGOSI
jamani hawa Waandishi wanatafuta habari na kuzituma ni mpaka ikubaliwe ndio analipwa kwani huko kwenye vyombo vya habari nako kuna kuchuja. Ndio maana utaona habari uliyoiona au picha zinarudiwa katika kituo kingine.
Wanachofanya, hata wewe sio lazima uwe Kanjanja fuma tukio, piga picha labda Jengo linaanguka,au Bomu linapigwa hiyo picha ilinde na utaiuza vizuri ha Al-Jazeera na Channel 10 hawatakuzuia.
Hizi picha zote za tukio la Nyalolo la mabomu aliyepiga picha hana habari km zimesambaa Dunia nzima hivyo hawezi dai ni zake au za ITV kwa sababu walienda waandishi 8 kweny tukio wakarudi 6
Channel 10 km wamemwajiri watalazimika kumlipa BIMA ya kuwa kazini akiwachukulia picha, NSSF na masurufu kibao ndio maana nasema sasa hivi usalama kazini sio kwa MaDr tu hata wafanyakazi wengine
Channel 10 wanadai hakuwa mwajiliwa hivyo sina hakika kama walikuwa wamemkatia bima...
 
Dickson, navyofahamu Marehemu alikuwa analipwa na Channel Ten kwa mkataba wa jinsi anavyoreport story... hilo si geni kabisa katika Uandishi wa Habari na sector zingine kama Afya, Ufundishaji hasa wa Vyuo Vikuu na wengi wanafanya Bongo na Duniani.

Na wakati mwingine Unaweza kufaidika zaidi kama ukiwa Unalipwa kwa style hii na Mtu anakuwa huru sana kufanya mambo binafsi kuliko kuwa mwajiriwa. Kuhusu NSSF, unaweza kuwa Mwanachama na Kufaidi mafao yote hata kama sio Mwajiriwa....
Ni kweli mkuu hamenya, ni kweli kuwa hata kama si mwajiliwa unaweza kulipwa NSSF ila ni pale tu utakapo kuwa mwanachama wa mfuko huo...Na hapa itakubidi uchangie asilimia zote 20...Ila kama umeajiliwa, mwajili anatoa kumi na wewe kumi so inakuwa rahisi...Afu ni watanzania wachache sana ambao wanajichangia wao wenyewe katika mifuko hii ya pensheni...
 
Hivi hiki kituo kinamilikiwa na nani? Ha ha ha ha ha! Kwa kadhia hii don't be surprised kuambiwa ni Chadema. Hapa hakuna jinsi ya kukwepa kujadili watu na matukio badala ya masuala. I am very sory for that.

Inawezekana eeeeh! Apology accepted ...

 
Part time for 6 years hii inanikumbusha yule wa ITV naye alifariki akiwa kibaraua
 
...Inawezekana David alikuwa na mkataba wa kuwa FREELANCER wa Channel 10 kwa maana ya kulipwa kwa kila habari anayopeleka na ikatumiwa na kituo hicho. Watu wengi tu wanafanya hivyo. Vyombo vingi vya Habari waandishi wao wa Mikoani sio waajiriwa no ma-freelancer tu.
Ina uzuri wake lakini inabidi hela unayopata uitunze kweli kweli kwa ajili ya matatizo kama haya. Nawahurumia sana familia ya Ndugu yetu ambaye ndio kwanzaa First-born wake yupo sekondari. Mungu wetu Mwema awalinde katika wakati mgumu huu na unaokuja...
 
Back
Top Bottom