Hivi kweli Tanzania tunastahili kuwa na vyuo vikuu?

Zumbukuku

Member
May 17, 2011
70
26
Wajameni..kuna jamaa yangu anasoma hapo chuo cha fweza IFM, kila siku ananiambia kuna kipindi saa 1 kamili asubuhi, hadi saa 3 usiku..hadi Jumamosi.... hadi Jumapili..Non - stop.... Mara lecturer anafanya kazi Gongolamboto kakosa usafiri kuwahi kipindi..Mara hakuna umeme ..kuna giza hakuna vipindi..ni ubabaishaji mtupu huko home.. Looks like mambo yako holela holela..Hivi kwa haya tunaweza kuwandaa vijana wetu kushindana na wengine duniani katika karne hii ya utandawazi na tekelinalokujia? Au tunatengeneza vijana ambao nao watakuwa wababaishaji, mafisadi..wala rushwa..n.k?

Nadhani bila kuweka siasa mbele au majisifu na uzalendo usio na mpango lazima tukubali tuko nyuma..nyuma .nyuma sana katika suala la elimu..Huwezi kumlinganisha mtu anayegraduate kwenye mazingira kama haya na yule alisoma kwenye University za wenzetu ambazo mazingira pekee ni point of success..

Huu utitiri wa vyuo kama hivi ufutwe..tusiwe na majina tu ya vyuo vikuu bali..vi-qualify kuwa vyuo vikuu..Kalagabaho!
 
Back
Top Bottom