Kwa mtizamo ambao sio timamu sana wabongo wengi tunafikiri soka ni mchezo maarufu sana,upande wa serikali ndio kabisa hakuna mipango endelevu kabisaa chukua mfano,tunawanunua makocha kwa pesa ya kutupwa kufundi mpira watu wenye miaka zaid ya 25 wakati kwa wale wanaojua soka la kimataifa mchezaji akitimiza umri huo maana yake ndio amezeeka.Bado hata hao makocha wakifika hakuna jipya tunaloliona zaid ya ule ule mpira wetu wa Anao,anao BUSARA ingekuwa kuwachukua wazawa kuwapeleka nje kwenye koz za ukocha na warudi kuimarisha kwanza soka la watoto mfano tunao kwenye nchi kama GHANA &NIGERIA kuliko kupoteza mapesa mengi kwa kuwalipa hao makocha wa nje.Tukirudi katika mfumo wa lig yetu ndio kichekesho hakuna soka la maana linalochezwa uwanjan zaid ya majigambo kwenye vyombo vya habari.Lig imekosa matangazo kitaifa na kimataifa ingawa sisi wenyewe tunajivunia utumbo huu.Ukija kwenye zawad! Masikini utatamani kulia kwan lig inachezwa zaid ya miezi 6 lakini bingwa anapata kombe na fedha isiyozid 50mil wakati huo huo mshindi mmoja wa BONGO STAR SEARCH(BSS) anapewa zaidi ya 30mil,hv kweli soka litakuwaje maarufu kwa mtizamo wetu dhaifu usio na hoja angavu na zenye mantiki.?,nadhani tunahitaji mabadiliko.