Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,185
- 307
Ijumaa nilisikitishwa na taarifa ya Radio One kuwa serikali imezionya halmashauri za wilaya ambazo hazitajumuisha ununuzi wa matrekta kwenye bajeti zake za 2011/2012 kuwa bajeti zake hazitapitishwa na serikali.
Kwa maana nyingine ni kuwa halmashauri zitakuwa zikishindana kununua matrekta ili kusudi kuwalidhisha "wakubwa" kwani kutonunua trekta ni kutokuunga mkono sera ya kilimo kwanza.
Kwa maoni yangu, matrekta siyo kipaumbele cha kila wilaya. Angalau nina uhakika na mikoa ya Shinyanga, Mwanza, na Mara kwa kiwango kikubwa matrekta siyo kipaumbele namba moja kwani wanatumia plau za kukokotwa na ng'ombe/punda na wanalima kwa kiwango kikubwa bila kuvuna kadri ya jitihada zao kwa sababu hakuna uhakika wa mvua, nadhani kilimo kwanza ingekuwa na maana zaidi kwa wakulima hawa kama wangejengewa mabwawa na kuimarisha kilimo cha umwagiliaji badala ya kununuliwa matrekta.
Kuzilazimisha kila wilaya zinunue matrekta siyo kuwakomboa watanzania masikini bali ni kuwanufaisha watengenezaji wa matrekta haya pamoja na mawakala wao. Umefika wakati sasa viongozi wetu watusaidie kupinga sera zinazolenga kuwanufaisha wachache na kuwaacha walio wengi wakitweta katika umasikini uliokithiri.
Ifike mahali sasa wananchi ndio waamue nini wanataka badala ya wanasiasa kuja na kauli mbiu zisizokuwa na kichwa wala miguu ambazo zina malengo ya kuwanyonya watanzania badala ya kuwasaidia.. Kwangu mimi RUZUKU inayotolewa kwa matrekta yatakayouzwa kwenye wilaya ambazo matrekta siyo kipaumbele cha kwanza ni UFISADI
Kwa maana nyingine ni kuwa halmashauri zitakuwa zikishindana kununua matrekta ili kusudi kuwalidhisha "wakubwa" kwani kutonunua trekta ni kutokuunga mkono sera ya kilimo kwanza.
Kwa maoni yangu, matrekta siyo kipaumbele cha kila wilaya. Angalau nina uhakika na mikoa ya Shinyanga, Mwanza, na Mara kwa kiwango kikubwa matrekta siyo kipaumbele namba moja kwani wanatumia plau za kukokotwa na ng'ombe/punda na wanalima kwa kiwango kikubwa bila kuvuna kadri ya jitihada zao kwa sababu hakuna uhakika wa mvua, nadhani kilimo kwanza ingekuwa na maana zaidi kwa wakulima hawa kama wangejengewa mabwawa na kuimarisha kilimo cha umwagiliaji badala ya kununuliwa matrekta.
Kuzilazimisha kila wilaya zinunue matrekta siyo kuwakomboa watanzania masikini bali ni kuwanufaisha watengenezaji wa matrekta haya pamoja na mawakala wao. Umefika wakati sasa viongozi wetu watusaidie kupinga sera zinazolenga kuwanufaisha wachache na kuwaacha walio wengi wakitweta katika umasikini uliokithiri.
Ifike mahali sasa wananchi ndio waamue nini wanataka badala ya wanasiasa kuja na kauli mbiu zisizokuwa na kichwa wala miguu ambazo zina malengo ya kuwanyonya watanzania badala ya kuwasaidia.. Kwangu mimi RUZUKU inayotolewa kwa matrekta yatakayouzwa kwenye wilaya ambazo matrekta siyo kipaumbele cha kwanza ni UFISADI