Hivi kweli Barrick wanaweza kutupenda kufikia kiasi cha kuhatarisha maslahi ya wazungu wenzao wa ACACIA?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,986
144,313
Hili ndio swali ambalo siku zote huwa najiuliza kama hawa wazungu kweli wanaweza kufanya jambo litakaloharisha masilahi yao na hata mahusiano baina yao kwa faida ya Tanzania na watu wake.

Kwa mfano,mimi kama mimi huwa najiuliza, ni nini kiliwafanya Barrick waridhie malipo kiduchu kama sio tu kulinda wenzao?

Halafu wengekuwa upande wetu kama baadhi ya watu wanavyoamini,yale mazungumzo kweli yangekuwa magumu mpaka yachukue muda wote ule wa miezi karibu mitatu kama sikosei?

Nina wasiwasi sana na hawa watu kuwa wameamua kula na vipofu na hata chochote watachokubaliana,ndani yake itakuwa ni kuwalinda tu wenzao Acacia na si vinginevyo.

Na je,ile kesi Acacia waliotufungulia katika Mahakama ya usuluhishi huko nje na ambayo hata aliekuwa waziri wa sheria wakati huo bwana Kabudi alikiri Bungeni kuwa ipo,mbona haitajwi popote?
 
Swali hilo ungejiuliza pia kwa Lisu kuzunguka kwa wazungu kwamba wanatupenda kiasi gani hadi waache mambo yao waje kukupigania wewe hapo ufipa?

Sijui mtapata lini akili enyi ufipa?

Wakifanya kwa upande wa selikali mnaona ni unafiki, lakini Lisu akizunguka na kupiga hodi majumbani mwao kulia lia mnasema kabisa Mungu wabariki wazungu
 
Swali hilo ungejiuliza pia kwa Lisu kuzunguka kwa wazungu kwamba wanatupenda kiasi gani hadi waache mambo yao waje kukupigania wewe hapo ufipa?

Sijui mtapata lini akili enyi ufipa?

Wakifanya kwa upande wa selikali mnaona ni unafiki, lakini Lisu akizunguka na kupiga hodi majumbani mwao kulia lia mnasema kabisa Mungu wabariki wazungu
We ni zero kabisa!!Hiyo ripoti yenye tu kwa watanzania mmeshindwa kuiweka wazi kwasababu ni vituko vitupu sasa ndio utarajia mzungu ahatarishe maslahi ya mzungu wenzake kwa kitu kisicho na mashiko?

Wengukwa wanajijua wana makosa,wengeenda kutushitaki?
 
We ni zero kabisa!!Hiyo ripoti yenye tu kwa watanzania mmeshindwa kuiweka wazi kwasababu ni vituko vitupu sasa ndio utarajia mzungu ahatarishe maslahi ya mzungu wenzake kwa kitu kisicho na mashiko?

Wengukwa wanajijua wana makosa,wengeenda kutushitaki?
Sasa mm nikuulize leo ndio mzungu kawa hatari lakn kwa Lisu mzungu ni mwema sana?
 
Uzi wako unaonyesha kukiri wazungu wana umoja hata kama mwenzao kakosea,lakini sisi kwa sisi kwenye maslahi ya taifa tunagawika kirahisi sana.
Sasa mjifunze hapo ,kugawanyika kwetu ndio mtaji wao
 
Sasa mm nikuulize leo ndio mzungu kawa hatari lakn kwa Lisu mzungu ni mwema sana?
Lissu aliweka wazi kuwa hiyo report ni rubbish tena akawashauri mjitoe kwanza kwenye mikataba ya kimataifa mliyoingia kama mnataka kushindana na hao watu ila kwa akili zenu hamkumuelewa.
 
Uzi wako unaonyesha kukiri wazungu wana umoja hata kama mwenzao kakosea,lakini sisi kwa sisi kwenye maslahi ya taifa tunagawika kirahisi sana.
Sasa mjifunze hapo ,kugawanyika kwetu ndio mtaji wao
Kwa sasa CCM hii ya watu wasiojulikana ni hatari kwa mtanzania kuliko hata hawa wazungu!!!!

Wanapotusaidi kupambana na madikteta tutawaunga mkono kama ambavyo nyinyi huwaunga mikono pale wanapowapa misaada ikiwemo kuwaita wanaume wanapowafurahisha.
 
Barrick ndio mmiliki mkubwa,analinda jina na heshima yake kibiashara duniani. Acacia walianzisha wao pia ilikuwa mbinu yao kwa Africa kufanya deals zao ni sawa na main contract aweke sub contractor.
Japo nae anakuwa na nguvu yake kisheria.
Kwetu sisi ni fursa muhimu, Barrick atabeba msalaba wote kadiri ya makubaliano.
 
Kwa sasa CCM hii ya watu wasiojulikana ni hatari kwa mtanzania kuliko hata hawa wazungu!!!!

Wanapotusaidi kupambana na madikteta tutawaunga mkono kama ambavyo nyinyi huwaunga mikono pale wanapowapa misaada ikiwemo kuwaita wanaume wanapowafurahisha.
Ujinga mlionao mnafikiri taifa likiyumbishwa nyie na koo zenu mtabaki salama,Nchi ikitozwa Magufuli hatoi zake mfukoni ,ni sisi tabaka la chini ndio tunaobeba mzigo,akiwemo na mama yako,nyie endeleeni kujifurahisha mkidhani mnamkomoa Magufuli
 
Barrick ndio mmiliki mkubwa,analinda jina na heshima yake kibiashara duniani. Acacia walianzisha wao pia ilikuwa mbinu yao kwa Africa kufanya deals zao ni sawa na main contract aweke sub contractor.
Japo nae anakuwa na nguvu yake kisheria.
Kwetu sisi ni fursa muhimu, Barrick atabeba msalaba wote kadiri ya makubaliano.
Unoangea utadhani umeona kilichokubaliwa/kitakachokubaliwa!!
 
Uzi wako unaonyesha kukiri wazungu wana umoja hata kama mwenzao kakosea,lakini sisi kwa sisi kwenye maslahi ya taifa tunagawika kirahisi sana.
Sasa mjifunze hapo ,kugawanyika kwetu ndio mtaji wao
Uwe na umoja na mtu aliepania kukuangamiza?

Na uwe na umoja kwa kitu kisicho na mashiko ambacho hata mimi umenificha ili wote tuonekane akili zetu zinafanana?
 
Uwe na umoja na mtu aliepania kukuangamiza?

Na uwe na umoja kwa kitu kisicho na mashiko ambacho hata mimi umenificha ili wote tuonekane akili zetu zinafanana?
Sasa uzi wa kihuruma umeleta wa nini?,si ungeandika kwa ule mtindo wenu wa siku zote wa kuzodoa na kufurahia nchi kukwama tu
 
Swali hilo ungejiuliza pia kwa Lisu kuzunguka kwa wazungu kwamba wanatupenda kiasi gani hadi waache mambo yao waje kukupigania wewe hapo ufipa?

Sijui mtapata lini akili enyi ufipa?

Wakifanya kwa upande wa selikali mnaona ni unafiki, lakini Lisu akizunguka na kupiga hodi majumbani mwao kulia lia mnasema kabisa Mungu wabariki wazungu
Leo Zitto kawaumbua sijui utasema nini tena!!

Hakika wajinga ndio waliwao!!
 
Back
Top Bottom