Hivi kwanini Wilaya ya Rombo kuna tatizo kubwa sana la Network?

Waziri wa Kaskazini

JF-Expert Member
Dec 12, 2015
6,967
14,713
Sijawahi kuelewa kwanini hii Wilaya mitandao ya sim inasumbua sana network, ukiwa na smartphone network kuipata hadi uende sehemu yenye mnara wa simu.

- Miaka ya nyuma nilikuwa natumia laini ya safaricom ya Kenya nilikuwa napata network na Internet ya uhakika.

- Ukija upande wa radio ndiyo kabisa yaani wananchi wa hii wilaya wanaskiliza radio za Kenya zaidi ya radio za Tanzania asilimia 90 wanaskiliza radio za nchi jirani Kenya

TCRA tatizo ni nini?
 
Aaah matatizo ya kimipaka Chief, usiwe na wasiwasi.

kule nimefanikiwa kukaa kati ya 2009-2012. Kiufupi ni karibia Kilimanjaro yote na sio Rombo pekee + Moshi V pamekuwa affected sana na mitandao ya hapo Kenya, haswa Safaricom

Njoo kwenye Radio..nilikuwanikiturn on, KBC hiyo hapo, mara citizen, sijui Anguo fm hujakaa sawa Milele FM kule vurugu vurugu tu!

Kipindi hicho nilikuwa sana mdau wa Radio citizen Chemichemi ya Ukweli; hivi wakina Joyce Gituro, Josephat Odipo + Christine Ojambo bado wapo?
 
Rombo ipo kwenye milima sana. Ni vigumu network kushika kwenye milima maana signal zinakua blocked na vilima. Ukiweza kufanya coverage upande mmoja wa mlima basi upande unaofuatia hakuna network.

Solution hapa ni kuweka repeater na signal booster au kuongeza idadi ya minara.

G1800/U2100 band itawafaa sana maama wanafanya coverage ndogo kuliko sasa walivyoweka G900 wakati ni useless tu.

G stand for GSM

The number ni frequency.
 
Rombo ipo kwenye milima sana. Ni vigumu network kushika kwenye milima maana signal zinakua blocked na vilima. Ukiweza kufanya coverage upande mmoja wa mlima basi upande unaofuatia hakuna network.

Solution hapa ni kuweka repeater na signal booster au kuongeza idadi ya minara.

G1800/U2100 band itawafaa sana maama wanafanya coverage ndogo kuliko sasa walivyoweka G900 wakati ni useless tu.

G stand for GSM

The number ni frequency.
Kuongeza minara linaweza kusaidia hii imagine kuna sehemu unakuwa hupatikani kabisa ilhali simu haijazima lakini ikiishajiunga safaricom basi unakuwa kama hupatikani.
 
Aaah matatizo ya kimipaka Chief,usiwe na wasiwasi.
kule nimefanikiwa kukaa kati ya 2009-2012..kiufupi Kilimanjaro sio Rombo wala Moshi V pamekuwa affected sana na mitandao ya hapo Kenya!..haswa Safaricom

Njoo kwenye Radio..nilikuwanikiturn on,KBC hiyo hapo,mara citizen,sijui Anguo fm hujakaa sawa Milele fm kule vurugu vurugu tuu!

Kipindi hicho nilikuwa sana mdau wa Radio citizen Chemichemi ya Ukweli..hivi wakina Joyce Gituro,Josephat Odipo + Christine Ojambo bado wapo?
Nini maana ya Anguo kiongoz,tuanze na hili
 
Hivi hiyo wilaya ya Rombo ndio wanaume wanakula sana gambe mpaka wanawake wanalazimika kwenda kutafuta wanaume Kenya
 
Aaah matatizo ya kimipaka Chief, usiwe na wasiwasi.

kule nimefanikiwa kukaa kati ya 2009-2012. Kiufupi Kilimanjaro sio Rombo wala Moshi V pamekuwa affected sana na mitandao ya hapo Kenya, haswa Safaricom

Njoo kwenye Radio..nilikuwanikiturn on, KBC hiyo hapo, mara citizen, sijui Anguo fm hujakaa sawa Milele FM kule vurugu vurugu tu!

Kipindi hicho nilikuwa sana mdau wa Radio citizen Chemichemi ya Ukweli; hivi wakina Joyce Gituro, Josephat Odipo + Christine Ojambo bado wapo?
Marehemu waweru mbulu
 
Suala la redio hata Mwanza maeneo ya Igoma mbugani redio zote kubwa hata RFA hazishiki. Yaani hapo ndo jiji wanaita.
Kuna redio moja tu ya Kiislam ndiyo inashika. Maajabu sana, maana hapo ni jijini
 
Sijawahi kuelewa kwanini hii Wilaya mitandao ya sim inasumbua sana network, ukiwa na smartphone network kuipata hadi uende sehemu yenye mnara wa simu.

- Miaka ya nyuma nilikuwa natumia laini ya safaricom ya Kenya nilikuwa napata network na Internet ya uhakika.

- Ukija upande wa radio ndiyo kabisa yaani wananchi wa hii wilaya wanaskiliza radio za Kenya zaidi ya radio za Tanzania asilimia 90 wanaskiliza radio za nchi jirani Kenya

TCRA tatizo ni nini?
Changamoto ya net kule ni kubwa na kero ya muda sasa. Kero nyingine kule ni ulevi wa kupindukia, aise hii kwa rombo imekuwa kero kubwa mno. Jamaa wanapiga ile kitu yao sijui inaitwaje jina nimesahau.

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Rombo ipo kwenye milima sana. Ni vigumu network kushika kwenye milima maana signal zinakua blocked na vilima. Ukiweza kufanya coverage upande mmoja wa mlima basi upande unaofuatia hakuna network.

Solution hapa ni kuweka repeater na signal booster au kuongeza idadi ya minara.

G1800/U2100 band itawafaa sana maama wanafanya coverage ndogo kuliko sasa walivyoweka G900 wakati ni useless tu.

G stand for GSM

The number ni frequency.
Hapo nimeelewa GSM tu, bila shaka ni yule anayeiweka timu ya wananchi mjini?
 
Serikali ya Tanzania imewafungia njia zote za biashara warombo. Kwa jiografia ya Rombo, kulipaswa kuwe na free borders na kenya. Rombo imeungana na county ya kajiado, huku kukiwa na mahusiano ya kibiashara na kabila la wakamba.

Tuanzie hapo, ili kukuza ushirikiano wa jumuiya ya Afrika Mashariki
 
Back
Top Bottom