Hivi kwanini Watanzania wengi hawapendi kuomba kazi kwenye mashirika ya Kimataifa?

Perry

JF-Expert Member
Feb 24, 2011
10,043
2,000
Nilikua nabadilishana mawazo na mmama mmoja hivi mkenya ambaye ni HR kwenye NGO fulani ya kimataifa inayojishughulisha na masuala ya kuhudumia wakimbizi kwa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara akawa ananiambia watz wengi hatupendi kujihangaisha na kuomba kazi za kimataifa.

Akatolea mfano NGO yao ilitangaza nafasi kama 8 kwa raia wa Tanzania tu, ila cha ajabu ni watanzania wawili tu waliojitokeza kuomba hizo kazi tena na wao baada ya kuwashortlist cha ajabu kwenye interview hawakutokea ikabidi nafasi zichukuliwe na wakenya..

Sasa naye akawa anashangaa watanzania tuna matatizo gani huku tunalia hakuna ajira lkn tunakuwa wazito kutuma maombi ya kazi pindi zinapotolewa..

Kwa kweli me nilichomjibu ni kwamba kwa watanzania ili uonekane una kazi basi ni lazima uajiriwe na serikali hivo wengi wao wanapenda kuomba kazi huko sasa sijui kama jibu langu lilikua sahihi au sio sahihi wakuu?
 
Yaani hiyo case moja ndio tayari umehitimisha kuwa Watanzania wengi hawapendi kuomba kazi kwenye mashirika ya kimataifa!!??
 
Inawezekana kabisa Watanzania hatukuwa na sifa hizo ila SIO KWELI kwamba hatupendi kuomba kazi kwenye mashirika hayo, mimi binasi nayapenda sana na ninatamani nipate kazi huko na si serikalini na pia huwa wanawekana na wao wakati mwingine.
 
nilikua nabadilishana mawazo na mmama mmoja hivi mkenya ambae ni hr kwenye ngo flani ya kimataifa inayojishughulisha na masuala ya kuhudumia wakimbizi kwa nchi za kusini mwa jangwa la sahara.akawa ananiambia watz wengi hatupendi kujihangaisha na kuomba kazi za kimataifa.akatolea mfano ngo yao ilitangaza nafasi kama 8 kwa raia wa tanzania tu,ila cha ajabu ni watanzania wawili tu waliojitokeza kuomba hizo kazi tena na wao baada ya kuwashortlist cha ajabu kwenye interview hawakutokea ikabidi nafasi zichukuliwe na wakenya..sasa nae akawa anashangaa watanzania tuna matatizo gani huku tunalia hakuna ajira lkn tunakua wazito kutuma maombi ya kazi pindi zinapotolewa..kwa kweli me nilichomjibu ni kwamba kwa watanzania ili uonekane una kazi basi ni lazima uajiriwe na serikali hivo wengi wao wanapenda kuomba kazi huko sasa sijui kama jibu langu lilikua sahihi au sio sahihi wakuu?
hapana
hauko sahihi.
binafsi sipendelei kuomba kazi serikalini kwa sasa, ila kila nikiomba kwenye taasisi za kimataifa natoswa.
nina degree ya Mass Communication, major in Broadcasting
 
We unajua mashart yao kwenye hzo application zao hapo ndio kwenye tatzo kuna vitu ving sana kias. Kwamba watu weng inawakatisha tamaa wa. Waseme waweke vgezo kama vile vya utumish uone
 
nilikua nabadilishana mawazo na mmama mmoja hivi mkenya ambae ni hr kwenye ngo flani ya kimataifa inayojishughulisha na masuala ya kuhudumia wakimbizi kwa nchi za kusini mwa jangwa la sahara.akawa ananiambia watz wengi hatupendi kujihangaisha na kuomba kazi za kimataifa.akatolea mfano ngo yao ilitangaza nafasi kama 8 kwa raia wa tanzania tu,ila cha ajabu ni watanzania wawili tu waliojitokeza kuomba hizo kazi tena na wao baada ya kuwashortlist cha ajabu kwenye interview hawakutokea ikabidi nafasi zichukuliwe na wakenya..sasa nae akawa anashangaa watanzania tuna matatizo gani huku tunalia hakuna ajira lkn tunakua wazito kutuma maombi ya kazi pindi zinapotolewa..kwa kweli me nilichomjibu ni kwamba kwa watanzania ili uonekane una kazi basi ni lazima uajiriwe na serikali hivo wengi wao wanapenda kuomba kazi huko sasa sijui kama jibu langu lilikua sahihi au sio sahihi wakuu?
Tatizo wana masharti magumu sana mfano wanataka uzoefu mkubwa sana ie 5 working experinece kwa Officer wakati kwa NGO za kibongo mtu mwenye experience hiyo ni manager, na kingine Watanzania wengi wanakimbia kwani lugha ni tatizo.
 
Tatizo wana masharti mengi mara uandike composition isiyopungua kurasa mbili sasa hayo yote ya nini?
If you are not willing to do extra beyond your comfort zone then you will just remain where you are..Hiyo excuse ya kushindwa kuandika composition ni ya kitoto sana
 
Back
Top Bottom