Hivi kwanini wasomi wa Tanzania wanaamini kuajiriwa ni Serikalini tu?

Kuna tatizo sana kwa watanzania wasomi kuamini kuaijiriwa mpaka upate kazi serikalini. Hii mindset tunaweza kuiondoaje kwa wasomi? Mfano hai ni kwenye hizi ajira za walimu na wafanyakazi afya idadi kubwa imejitokeza kuomba ajira hizo na kupelekea kuonesha kuwa hapa Tanzania kuna tatizo kubwa la ajira kwenye hizo kada kitu ambacho si kweli.

Mimi binafasi kuna jamaa zangu watano wameajiriwa shule binafsi na wengine wana maendeleo mazuri tu mpaka kujenga lakini kila ajira zikitangazwa wanakimbizana kuomba serikalini na kuwaaribia wengine ambao hawajapata pa kujishikiza,kuna mmoja nilimpigia nikamwambia kabisa usithubutu hata kidogo kutoka hapo kibaruani ulipo eti unakuja serikalini utajutia sna,maendeleo aliyonayo mimi niliyepo serikalini hata robo simfikii lakini wazazi wake wanamshinikiza aombe serikalini kila mara. Kuna jamaa wengine tunaofahamiana wapo hospitali binafsi na wana maisha mazuri lakini na wao wana hiyo mindset.

Ushauri kwa serikali. Iandae mpango kazi wa urasimishaji ajira kwenye sekta binafsi na mashirika pamoja na waliopo serikalini. Kwa uchunguzi wangu unaonesha kuwa hawa wafanyakazi waliopo sekta binafsi hawatambuliki popote hata kodi hawalipi lakini wapo wengi sana walioajiriwa sekta binafsi. Mwenye takwimu sahihi ya idadi ya mashule na vituo vya afya binafsi alete hapa uone idadi yao ilivyokubwa na bado shule na hospitali zinaongezeka kila mwaka lakini bado watu wanasema hakuna ajira. Mtu kuajiriwa sekta binafsi anajiona kama vile amejishikiza huku akiwainda kuingia serikalini.

Ushauri mwingine kwa serikali, izidi kuwabana hawa wamiliki wa hizo taasisi binafsi wahakikishe wakitimiza mahitaji yanatakiwa kwa muajiriwa kama bima,mkataba mzuri na usalama kazini.
Private jobs hakuna security of employment. Wakati wowote unaweza kufukuzwa kazi. Mfano mwaka jana kipindi cha corona wengi waliachishwa kazi na hawajarudi kazini. Najua mtu mpaka leo anahangaika hajapata kazi. Kungkuwa na security nadhani watu wangeprefer kuajiriwa huko. Serikalini hakuna aliyefukuzwa na waliendelea kulipwa mishahara. Serikalini mpaka ufukuzwe ni process ndefu. Kwenye sekta binafsi unaajiriwa kwa mkataba wa miaka michache sana miwili nadhani. Mtu anataka akipata kazi iwe ya kudumu e.g unakaa 30 yrs na hata pensheni itakuwa nzuri. Ila kwa sasa fursa ni nyingi za kujiajiri. Tatizo kuijua hiyo fursa na nadhani mtaji pia ni tatizo. Wasomi wanaweza kujiajiri.
 
Acha upotoshaji ( uchochezi )
Watu ni wavivu kufanya kazi, sekta binafsi unapigika balaa, serikalini hata uwe mlevi wa kulewa siku nzima na kazi unafanya kwa kusuasua utaendelea kuwepo na mshahara pale pale. Hiyo ndo security ambayo wengi wanaitaka.
 
Watu ni wavivu kufanya kazi, sekta binafsi unapigika balaa, serikalini hata uwe mlevi wa kulewa siku nzima na kazi unafanya kwa kusuasua utaendelea kuwepo na mshahara pale pale. Hiyo ndo security ambayo wengi wanaitaka.
Nayo ni faida kwani unapenda upunda
 
Kwa tuliofanya kazi sector binafsi na sasa tupo serikalin tunajua shida ya sector binafsi mshahara tarehe 50 ,bima za afya za kubumba ,full kubanwa na kufuatiliana fuatiliana hata kama serikalin mshahara pungufu wa ule wa mwanzo ni heri nipate hii 300k ya uhakika kuliko 500k ya masimango
 
Kuna mtu wangu wa karibu anapokea 800k Take home 580k Bonus za katikati ya mwezi za kutosha ..yaani inafika mpaka milioni moja ukijumlisha na mshahara .. kasoma diploma pekee,
Shirika binafsi.. ety kwa shinikizo la wazazi kaaply ajira za serikali.. namwangalia nacheka hihiii...
Hivi nurse ngazi ya diploma serikalini analipwa Tsh ngapi vile?
 
Asikudanganye mtu ndugu yangu serikalini patamuuu haswa haswa !!! Sector binafsi ni shida tupu tupu tupu uliza uambiwe !!! Serikalin pesa ni ya uhakika kuliko sector binafsi!!! Serikalini walim walio fundisha muda wako juuu sana mshahara mfano aliyefundisha 10 years plus anaongelea G ambaya nafikiri itakya 1600,000/ per month !!! Nani sekta binafsi atakulipa hiyo!??
Watu wanakopa benk mpaka 40,000,000/ wapi sector binafsi ataruhusi hiyo!?? Bima za afya kwa familia nk !!! Watu wanapigwa kiinua mgongo mpaka 150,000,000/
Na bado monthly pension 800,000/ kila mwezi mpaka ufe na kutibiwa bure mpaka ufe!!! Nani mwenye akili atakataa hilo!!??
Private ni mavi takataka asikwambie mtu !!! Uliza private gani inaweza lipa mwalimu hata 1200,000!?? Zipo ngapi!!???
Haya madogo yanadanganyana.
Neno "security ya kazi" bado ni msamiati kwao.
 
Ni kwasababu serikalini kuna job security.

Private companies ni nzuri ila mikataba yao ni mifupi

Na haina guarantee kama kampuni ita renew mkataba na wewe pindi mkataba wako unapoisha
 
Kwa sababu hata wewe ni Kati ya wajinga sambamba na hao wasomi kwa sababu huelewi changamoto za mfumo wa.elimu walioupata.
 
Kuna mtu wangu wa karibu anapokea 800k Take home 580k Bonus za katikati ya mwezi za kutosha ..yaani inafika mpaka milioni moja ukijumlisha na mshahara .. kasoma diploma pekee,
Shirika binafsi.. ety kwa shinikizo la wazazi kaaply ajira za serikali.. namwangalia nacheka hihiii...
Hivi nurse ngazi ya diploma serikalini analipwa Tsh ngapi vile?
Tsh 680,000 Gross
 
Kuna tatizo sana kwa watanzania wasomi kuamini kuaijiriwa mpaka upate kazi serikalini. Hii mindset tunaweza kuiondoaje kwa wasomi? Mfano hai ni kwenye hizi ajira za walimu na wafanyakazi afya idadi kubwa imejitokeza kuomba ajira hizo na kupelekea kuonesha kuwa hapa Tanzania kuna tatizo kubwa la ajira kwenye hizo kada kitu ambacho si kweli.

Mimi binafasi kuna jamaa zangu watano wameajiriwa shule binafsi na wengine wana maendeleo mazuri tu mpaka kujenga lakini kila ajira zikitangazwa wanakimbizana kuomba serikalini na kuwaaribia wengine ambao hawajapata pa kujishikiza,kuna mmoja nilimpigia nikamwambia kabisa usithubutu hata kidogo kutoka hapo kibaruani ulipo eti unakuja serikalini utajutia sna,maendeleo aliyonayo mimi niliyepo serikalini hata robo simfikii lakini wazazi wake wanamshinikiza aombe serikalini kila mara. Kuna jamaa wengine tunaofahamiana wapo hospitali binafsi na wana maisha mazuri lakini na wao wana hiyo mindset.

Ushauri kwa serikali. Iandae mpango kazi wa urasimishaji ajira kwenye sekta binafsi na mashirika pamoja na waliopo serikalini. Kwa uchunguzi wangu unaonesha kuwa hawa wafanyakazi waliopo sekta binafsi hawatambuliki popote hata kodi hawalipi lakini wapo wengi sana walioajiriwa sekta binafsi. Mwenye takwimu sahihi ya idadi ya mashule na vituo vya afya binafsi alete hapa uone idadi yao ilivyokubwa na bado shule na hospitali zinaongezeka kila mwaka lakini bado watu wanasema hakuna ajira. Mtu kuajiriwa sekta binafsi anajiona kama vile amejishikiza huku akiwainda kuingia serikalini.

Ushauri mwingine kwa serikali, izidi kuwabana hawa wamiliki wa hizo taasisi binafsi wahakikishe wakitimiza mahitaji yanatakiwa kwa muajiriwa kama bima,mkataba mzuri na usalama kazini.
wewe acha huko njoo huku private sector sisi tuje huko..
 
Hii ni kweli, Nina classmate wangu alikua anafundisha Private anakula 900k take home, akaomba ajira za serikali akapata bila kujiuliza akaenda,
Nikijana kabisa 28 yrs anakimbilia serikalini, kuanza kuwaza kiinua mgongo na vijisababi vingine vya kijinga Eti security.
Pole sana
 
Sekta binafsi kuna ile kitu bosi akiamka vibaya tu hauna chako pale na pia hizi sekta binafsi zina yumba kiuchumi unashangaa umepunguzwa na wengi wa wasomi hatupendi njia zingine za kujipatia kipato ukishaajiriwa basi umemaliza unatulia unategemea mshahara tu
 
Niko sector binafsi mwaka wa 9 huu ila sio kwenye ualimu, na wala sijawahi kujitoa kwakweli. Naona maisha yangu yako Safi na kama ni salary inapanda hata enzi zile serikali haipandishi kwa wafanyakazi wake.
Benefits zipo nyingi tu, km bima ya afya, housing allowance, air time allowance, staff development, promotions za hapa na pale, mwajiri katufanyia mambo ukitaka kukopa anakuwa mdhamini wake, napata social security fund
So, inategemea kwakweli. Sio sekta binafsi zote Ni majanga.
Taja wapi!!! ???
 
Ahsante sana Ndugu you said it all.Tangu Mwaka 2015 nilikuwa sector binafsi lakini yalionikuta nilijuta kwa nini nilikataa kwenda kureport ajira yangu serikalini mwaka 2017.

Nilifukuzwa kazi nikiwa nina week 2 kwenda kufunga Ndoa.

Sa hivi nipo Serikalini nina peace of mind japo mshahara sio wa kufanyia Anasa kwa kuwa ni kiduchu.
Utapanda tuu wala usihofu mambo yatakaa sawa tuu!!!ukiona MTU anatetea sekta binafs hasa hizo shule zao jua huyo ni kiherehere mzoefu
 
Kazi kubwa ya serikali sio kudhibiti sekta binafsi bali kuitengeneza mazingira mazuri iweze kuwa na ushindani wa wafanyakazi ili waweze kulipwa vizuri.

Kutajirikia katika ajira yoyote ni jambo gumu sana sio sekta binafsi tu hata serikalini ni hivyo hivyo. Wengi wanotajirika serikalini ni wezi na mafisadi na kwa sababu sio rahisi kuwajibishwa serikalini ukifanya ufisadi tofauti na kwenye kampuni binafsi.
Tatizo ni serikali yenyewe inashindwa dhibiti private sectors

Kampuni hazilipi vizuri..
Mikataba hakuna..
Kampuni za outsourcing zinazidi ongezeka..

Wakati fulani Tigo ilikuwa mshahara unaanza 1milion..sasa wakaleta outsourcing company ukashushwa hadi laki kadhaa..

Huo mfano mmoja
Ukienda Vodacom hivyo hivyo

Nani ana ndoto za kuajiriwa Azam au Mo?

Wanakuwaje matajiri lakini kampuni zao hazivutii kabisa wafanyakazi?
Hata bonus Tu hakuna achilia mbali shares kwa wafanyakazi..
 
Back
Top Bottom