Hivi kwanini wanawake wengi ni wachawi?

Tajiri Mapesa

JF-Expert Member
Feb 26, 2020
707
693
Habarini za leo wakuu, poleni na mihangaiko ya kila siku.

Wakuu nina swali, ni topic ambayo naifanyia utafiti. Topic inasema hivi, "Hivi kwanini wanawake wengi ni wachawi?" Maana hata tukisimuliwa habari za kuloga lazima tutaambiwa mbibi fulani ndio ameroga. Tukisimuliwa habari za kuloga mume hata hapa jamii forum wapo.

Naombeni majibu wakuu
 
Maelezo yako sio sahii!

Ungehoji ni kwanini wachawi wengi ni wanawake na sio wanawake wengi ni wachawi! Ingawaje unaweza kuona sentensi hizo mbili ni kama zipo sawa lakini kimsingi na kisarufi hazipo sawa hata kidogo. Labda pia huenda ungekuwa sawa kuhoji hivi ni kwanini wanawake wengi wanapenda mambo ya kishirikina hali inayowafanya wao wawe ndio kimbilio na makazi ya majini ukilinganisha na wanaume kwa sababu ukishakuwa na mambo ya kishirikina tu tayari unakuwa ni rafiki wa majini kwavile unakuwa huna tena imani thabiti.

Mtoto akizaliwa, ni wanawake ndio hukimbilia kuwafunga mimavi ya tembo kwamba eti ni dawa asiote! Kwenye mapenzi, nako watataka kwenda kwa waganga wa kienyeji! Wakianzisha hata biashara ya mama nitilie, mambo yakienda sivyo ndivyo mara mbili tatu tu, lazima ashauriwe na shoga ake akatafute "msaada" kwa waganga! Yote hayo ni ushirikina unaochafua nafsi zao na hivyo kuwa kimbilio la majini wanaopenda kuishi kwenye miili michafu kiroho.
 
wanawake si wasamehevu hutunza vinyongo nakutaka kulipa visasi ndo maana wanaupenda ushirikina, ndo maana unaambiwa ukirogwa na mwanamke utapata tabu sana kuliko kurogwa na me

mfano mzuri tu hata kwenye ndoa zetu, ukikosewa na ke utasamehe na kusahau bt wao wanatunza ikitokea umemkosea tena yanaunganishwa mpaka basi, kutunza makosa huleta huibua roho mbaya ya visasi
 
Walifundishwa na shetani pale bustanini

Sisi wanaume ni kama tunawaiga tu hzo dark Art's
 
Maelezo yako sio sahii!

Ungehoji ni kwanini wachawi wengi ni wanawake na sio wanawake wengi ni wachawi! Ingawaje unaweza kuona sentensi hizo mbili ni kama zipo sawa lakini kimsingi na kisarufi hazipo sawa hata kidogo. Labda pia huenda ungekuwa sawa kuhoji hivi ni kwanini wanawake wengi wanapenda mambo ya kishirikina hali inayowafanya wao wawe ndio kimbilio na makazi ya majini ukilinganisha na wanaume kwa sababu ukishakuwa na mambo ya kishirikina tu tayari unakuwa ni rafiki wa majini kwavile unakuwa huna tena imani thabiti.

Mtoto akizaliwa, ni wanawake ndio hukimbilia kuwafunga mimavi ya tembo kwamba eti ni dawa asiote! Kwenye mapenzi, nako watataka kwenda kwa waganga wa kienyeji! Wakianzisha hata biashara ya mama nitilie, mambo yakienda sivyo ndivyo mara mbili tatu tu, lazima ashauriwe na shoga ake akatafute "msaada" kwa waganga! Yote hayo ni ushirikina unaochafua nafsi zao na hivyo kuwa kimbilio la majini wanaopenda kuishi kwenye miili michafu kiroho.
Bravo naamini ushawahi Fanya research nnependa " how to write a resercah topic "
 
Mtoa mada ebu kuwa muwazi ili tujue namna ya kuchangia,achana na habari za kusikia,topic yako una weza thibitiaha kwa kutoa ushahidi wa lifestyle ya kwenu,Mf.Mama yako,dada zako,mashangazi,mashemeji zako nk,ili tuamini unachokisema maana kuleta mada mezani kwa maneno ya wana nzengo haitakuwa na maana
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom