Hivi kwanini viongozi wa Tanzania hasa CCM wanachanganyikiwa sana inapofikia hatua ya kuondolewa madarakani?

nguruka wa kig0ma

JF-Expert Member
Jan 16, 2020
2,946
2,929
Wanajamvi saalam!

Nimekuwa nikitafakari sana juu ya viongozi wa nchi hii hasa ccm ktk awamu hii. Siwaelewi kabisa, kwanini wanapoona dalili za kuondolewa madarakani wanachanganyikiwa kuliko hata vichaa wanaookota chakula majalalani.

Wanabadirika rangi kila muda. Mfano mbunge wa Mtama, nimemsikia bungeni akimfagilia Mkuu wa Malaika, kuwa aongezewe muda ili akamilishe kazi walizomtuma na kuwa kuwepo kwenye nafasi ile hakubahatisha bali CCM ilimchangua.

Amechambua maeneo kadha ikiwemo uchumi. Nape amesahau kuwa mwaka jana tu alishirikiana na baadhi ya makada wa CCM kutaka kumwangusha Mkuu wa Malaika. Leo anabadirika rangi kumfagilia njia mkuu wa malaika, mahali pasipo stahili.

Kwanini hakumfangilia njia kwenye vikao vya chama ambavyo vina mamlaka ya uteuzi. JE, HUKU SIYO KUCHANGANYIKIWA?

Nape alipotumbuliwa kwa sakata la Makonda, watu wengi walikuwa nyuma yake,walisamehe kosa lake la kufungia bunge live, WALIMUHURUMIA SANA.

Watu walijua kuwa Nape ni mtu mwenye kusimamia kauli zake, hata yalipovuja yale maongezi yao, watu wakaendelea kumwamini. Nimepata taabu sana baada ya kumsikiliza jana aliyokuwa anatapika bungeni.

Ndipo najiuliza: Hawa viongozi wa awamu hii wapo kwa ajili ya kuusimamia ukweli au kujipendekeza ili wapate uteuzi?
Nini kinawachanganya? Mbona hatukuona viroja kama hivi awamu zilizopita?

Anayejua jibu sahihi karibuni.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uhuru wa kujieleza mnaosema CCM hautaki uwepo ,huko upinzani uko wapi? Nape katoa maoni yake( uhuru wa kutoa maoni) Kama mtanzania ila wapinzani wamekusanyana kupinga maoni binafsi ya mtu.

Watu wa Kama Mdee, Lissu au Mbowe na wengineo wanaposema Rais Magufuli hafai, wanakuwa wapo sahihi?
 
Ndugu mleta mada. Nape hakuchanganyikiwa, aliyekuwa hivyo ni wewe.

Nape nj mwana CCM, ni lazima ampigie debe Raiso wa Chama Chake, kama nyie mnavyowapigia debe viongozi wenu.

Kajifunze unafiki wa siasa, ambao uko kila mahali penye siasa ulimwenguni. Ukitaka utakatifu nenda Msikitini au Kanisani, na huko poa siku hizi kuna siasa, itabidi ujifungie chumbani kwako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeelewa point zangu?
Viongozi hawa kubadirika kwenye kauli na misimamo yao.
Uhuru wa kujieleza haupingwi kinachopingwa ni kwamba ktk jambo moja, leo unasema nyeusi kesho blue.
Hicho ndicho kinapingwa. Nape anajikanganya sana, fuatilia toka kufungia bunge live mpk alipofikia hivi sasa.
HII IPO KWA VIONGOZI WENGI WA AWAMU HII, ISIPOKUWA ANTON MTAKA.

Hebu muangalie na makonda, juzi tu anashangaa watu kufunga maduka eti kwasababu ya corona.
Asubuhi kaja na lingine atakamata wazurulaji.
HUU NI UONGOZI?
HUU NI UHURU WA KUTOA MAONI AU KUJIELEZA? KUWA NA AKILI KIDGO
Uhuru wa kujieleza mnaosema CCM hautaki uwepo ,huko upinzani uko wapi? Nape katoa maoni yake( uhuru wa kutoa maoni) Kama mtanzania ila wapinzani wamekusanyana kupinga maoni binafsi ya mtu.

Watu wa Kama Mdee, Lissu au Mbowe na wengineo wanaposema Rais Magufuli hafai, wanakuwa wapo sahihi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu mleta mada , Nape hakuchanganyikiwa, aliyekuwa hivyo ni wewe.

Nape nj mwana CCM, ni lazima ampigie debe Raiso wa Chama Chake, kama nyie mnavyowapigia debe viongozi wenu.

Kajifunze unafiki wa siasa, ambao uko kila mahali penye siasa ulimwenguni. Ukitaka utakatifu nenda Msikitinj au Kanisani, na huko poa siku hizi kuna siasa, itabidi ujifungie chumbani kwako

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkindi, mahali sahihi ni bungeni au ktk vikao vya chama?
Au huyajui majukumu ya bunge ktk vikao vyake. Rudi shule kaka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanajamvi saalam!
Nimekuwa nikitafakari sana juu ya viongozi wa nchi hii hasa ccm ktk awamu hii.
Siwaelewi kabisa, kwanini wanapoona dalili za kuondolewa madarakani wanachanganyikiwa kuliko hata vichaa wanaookota chakula majalalani.

Wanabadirika rangi kila muda
Mfano mbunge wa mtama, nimemsikia bungeni akimfagilia mkuu wa malaika, kuwa aongezewe muda ili akamilishe kazi walizomtuma na kuwa kuwepo kwenye nafasi ile hakubahatisha bali ccm ilimchangua.

Amechambua maeneo kadha ikiwemo uchumi.
Nape amesahau kuwa mwaka jana tu alishirikiana na baadhi ya makada wa ccm kutaka kumwangusha mkuu wa malaika.
Leo anabadirika rangi kumfagilia njia mkuu wa malaika,mahali pasipo stahili.
Kwanini hakumfangilia njia kwenye vikao vya chama ambavyo vina mamlaka ya uteuzi!! JE HUKU SIYO KUCHANGANYIKIWA?

Nape alipotumbuliwa kwa sakata la makonda,watu wengi walikuwa nyuma yake,walisamehe kosa lake la kufungia bunge live,WALIMUHURUMIA SANA.

Watu walijua kuwa Nape ni mtu mwenye kusimamia kauli zake,hata yalipovuja yale maongezi yao,watu wakaendelea kumwamini.
Nimepata taabu sana baada ya kumsikiliza jana aliyokuwa anatapika bungeni.

Ndipo najiuliza hawa viongozi wa awamu hii wapo kwa ajili ya kuusimamia ukweli au kujipendekeza ili wapate uteuzi?
Nini kinawachanganya?
Mbona hatukuona viroja kama hivi awamu zilizopita?

Anayejua jibu sahihi karibuni.



Sent using Jamii Forums mobile app
Magufuli kasema hataki kuongeza muda.

Mkapa kasema Magufuli hataongeza muda.

Kwa nini watu hawakubali tu hili?

Mkapa on presidential term-limits

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Umeelewa point zangu, au umekuja na pombe kichwani?
Viongozi hawa kubadirika kwenye kauli na misimamo yao.
Uhuru wa kujieleza haupingwi kinachopingwa ni kwamba ktk jambo moja, leo unasema nyeusi kesho blue.
Hicho ndicho kinapingwa. Nape anajikanganya sana, fuatilia toka kufungia bunge live mpk alipofikia hivi sasa.
HII IPO KWA VIONGOZI WENGI WA AWAMU HII, ISIPOKUWA ANTON MTAKA.

Hebu muangalie na makonda, juzi tu anashangaa watu kufunga maduka eti kwasababu ya corona.
Asubuhi kaja na lingine atakamata wazurulaji.
HUU NI UONGOZI?
HUU NI UHURU WA KUTOA MAONI AU KUJIELEZA? KUWA NA AKILI KIDGO

Sent using Jamii Forums mobile app
Unachopaswa kujua hakuna mwanasiasa asiyejikanyaga hasa pale anapotaka kutetea ugari wake ukitka kujua rudi ya Ukawa na Lowasa kisha rudi hapo kwa Nape ndio utajua mwanasiasa ni mtu wa aina gani ila sasa sisi Watanzania huwa tunaangalia upande mmoja ule tunaoupinga ila tunauunga mkono huwa hatuuangalii na ndio shida inapoanzia hapo sasa ila kama tungekuwa tunaangalia pande zote basi tungeshajua wanasiasa tulionao wana rangi gani..
 
Wanajamvi saalam!
Nimekuwa nikitafakari sana juu ya viongozi wa nchi hii hasa ccm ktk awamu hii.
Siwaelewi kabisa, kwanini wanapoona dalili za kuondolewa madarakani wanachanganyikiwa kuliko hata vichaa wanaookota chakula majalalani.

Wanabadirika rangi kila muda
Mfano mbunge wa mtama, nimemsikia bungeni akimfagilia mkuu wa malaika, kuwa aongezewe muda ili akamilishe kazi walizomtuma na kuwa kuwepo kwenye nafasi ile hakubahatisha bali ccm ilimchangua.

Amechambua maeneo kadha ikiwemo uchumi.
Nape amesahau kuwa mwaka jana tu alishirikiana na baadhi ya makada wa ccm kutaka kumwangusha mkuu wa malaika.
Leo anabadirika rangi kumfagilia njia mkuu wa malaika,mahali pasipo stahili.
Kwanini hakumfangilia njia kwenye vikao vya chama ambavyo vina mamlaka ya uteuzi!! JE HUKU SIYO KUCHANGANYIKIWA?

Nape alipotumbuliwa kwa sakata la makonda,watu wengi walikuwa nyuma yake,walisamehe kosa lake la kufungia bunge live,WALIMUHURUMIA SANA.

Watu walijua kuwa Nape ni mtu mwenye kusimamia kauli zake,hata yalipovuja yale maongezi yao,watu wakaendelea kumwamini.
Nimepata taabu sana baada ya kumsikiliza jana aliyokuwa anatapika bungeni.

Ndipo najiuliza hawa viongozi wa awamu hii wapo kwa ajili ya kuusimamia ukweli au kujipendekeza ili wapate uteuzi?
Nini kinawachanganya?
Mbona hatukuona viroja kama hivi awamu zilizopita?

Anayejua jibu sahihi karibuni.



Sent using Jamii Forums mobile app
Nakubaliana na wewe kabisa.....mtu akishindwa kusimamia anachokiamini ni sawa na mfu.
Nape nimemdharau sana.
Angalia na upinzani pia mtu kama mashinji yaani pamoja na kujaza mashahada kibao kumbe ni makaratasi tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanajamvi saalam!

Nimekuwa nikitafakari sana juu ya viongozi wa nchi hii hasa ccm ktk awamu hii. Siwaelewi kabisa, kwanini wanapoona dalili za kuondolewa madarakani wanachanganyikiwa kuliko hata vichaa wanaookota chakula majalalani?

Anayejua jibu sahihi karibuni.
Mkuu Nguruka wa Kigoma, mimi nikiwa mwana CCM mtarajiwa, kwanza sii kweli kuwa kuna dalili zozote za CCM kuondolewa madarakani. Umechanganya wasiwasi wa Mbunge kutokupitishwa kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM, na CCM kuondolewa madarakani.
Hiyo ya Nape, wasiwasi wake ni wa kweli, lakini sio wasiwasi wa CCM kuondolewa madarakani, bali ni wasiwasi wa kutoteuliwa kusimama kwa tiketi ya CCM, na sii Nape pekee yake bali wote waliotumbuliwa na Magufuli, anaweza kuwa fykelea mbali, akiwemo January, Mwigulu, Ngeleja, Kitwanga, etc, hivyo hawa kuchanganyikiwa ni halali yao.

Lakini tukija kwa upande wa CCM, CCM iko imara na itatawala milele Tanzania!.
Kupata maendeleo ya kweli, Watanzania ni lazima tujifunze kuukubali ukweli!. Hili la CCM kutawala milele ni kweli!. - JamiiForums
Mkubali mkatae, huo ndio ukweli wenyewe.
P
 
Nape sahivi amekalia kuti kavu , ajiandae kukaa benchi, ccm inawatu wachafu Magufuli mqenyewe akasome.

Alichofanya Nnape Nauye jana Bungeni ilikuwa ni IBADA YA KUABUDU NA KUMTUKUZA MALAIKA MKUU...!
Nnape a.k.a. Nnepi anajiona ana DHAMBI kubwa Sana ya kiasi na kutoabudu ibada za malaika MKUU a.k.a JIWE kutoka Rock City!
Hivo Nnepi lazima afanye ibada za nguvu I'll malaika MKUU asije akamsahau kwene Ufalme wake wa 2021~2025!
Nnape amekuwa nepi ya kuvaliwa na Jiwe kwa Hakika.Tumesikia alivyo kuwa alifanya IBADA ZA USIKU WA MANANE akiomba na KUABUDU huku akilia apate KUSAMEHEWA DHAMBI ZAKE...!!!
Nape amesahau alivomsaidia malaika MKUU kuupata Ufalme. Kila Mtz anajua jinsi Mzee Abdulrhaman Kinana akisaidiana na Nnape walivopiga — ya nguvu ili Jiwe aupate Ufalme. Lakini leo Jiwe huyuhuyu amegeuka kuwa shetani kwa Kinana na Nnape. Mzee Kinana mpaka sasa Yuko detention ya Kisiasa kwa muda wa mwaka 1&1/2....,!!!!
 
Umeelewa point zangu, au umekuja na pombe kichwani?
Viongozi hawa kubadirika kwenye kauli na misimamo yao.
Uhuru wa kujieleza haupingwi kinachopingwa ni kwamba ktk jambo moja, leo unasema nyeusi kesho blue.
Hicho ndicho kinapingwa. Nape anajikanganya sana, fuatilia toka kufungia bunge live mpk alipofikia hivi sasa.
HII IPO KWA VIONGOZI WENGI WA AWAMU HII, ISIPOKUWA ANTON MTAKA.

Hebu muangalie na makonda, juzi tu anashangaa watu kufunga maduka eti kwasababu ya corona.
Asubuhi kaja na lingine atakamata wazurulaji.
HUU NI UONGOZI?
HUU NI UHURU WA KUTOA MAONI AU KUJIELEZA? KUWA NA AKILI KIDGO

Sent using Jamii Forums mobile app
Uhuru wa kutoa maoni hauna ukomo wa ufikiri, hivyo unabadilika kadiri mawazo yanavyobadilika na hii inatokana na uwezo walionao watu kuyatazama Mambo yajayo.

Kwa mfano: Rais Magufuli alivyoanza waliokuwa wanampinga walikuwa wengi lakini kadiri siku zilivyosonga wengine wakabadili mawazo na wengine wakaenda mbali na kumfuata CCM. Uhuru wa kutoa maoni walikuwa nao na wakautumia lakini mawazo na uelewa wao juu ya anayofanya Rais ulivyobadilika wakajikuta wamebadili mawazo.

Nape yupo sahihi, kubadilika kwa mtu kutokana na alichosema awali ni Jambo la kawaida. Tunazidiana vingi kichwani wengine ni wepesi kuelewa Jambo na wengine wanachukua muda kuelewa Jambo hilohilo hivyo ni suala la muda kabla ya kumlaumu mtu
 
Back
Top Bottom