Hivi kwanini upatu unavamia nchi yetu kila siku, tatizo ni nini?

Nyumbalao

JF-Expert Member
Jan 10, 2014
489
518
Kwa kuwa mshauri karibu watu wamekuwa wakiniuliza kuhusu upatu mpya wa D9 Club na jibu langu limekuwa moja tu hiyo ni Deci nyingine ila inashangaza kuwa hao walioamua au waliotayari nikiwaambia hivyo mara moja wanapanick na kutaka kusema wewe hujui na maneno mengi ya kashfa.

Wengine wamefikia kusema huoni wengine wanapata na jibu langu limebaki kuwa hakuna upatu unakuwa na mwisho mzuri full stop. Ila hii trend imenipa muda wa kujiuliza hivi kwanini kila baada ya muda kunazuka vitu kama hivi kulikuwa na kitu kinaitwa Dollar general miaka ya 1999 to 2000, na kikaja kile cha Arusha miaka ya 2003 hapo , ikaja baba yao Deci 2008 to 2009 ikala wakutosha, ikatokea TELEFREE 2013 hii niliipiga vita nikatishiwa na maisha na watu niliowaona walikuwa wanainfluence za sasa 2017 D9 nayo imeshika kasi ubaya sana umekamata wasomi ambao watu wanawaamini sana ila hata kwa kufanya layman googling utaona shida tayari iko kwenye huu mfumo. (Soma hii link D9 CLUB IS A FRAUD – ALERT! - Online Business Training)

Sasa swali ambalo nimewauliza waliokuwa wanakuja kuniomba ushauri D9 inafanya biashara gani? Sport betting, hivi wewe unaweza kwenda kuweka fedha yako kwenye vibanda vya sport bet ukitegemea kuwa tajiri? Ambazo zipo hapa mtaani kwetu jibu lao wengi ni hapana sasa kwanini unaamini kwenye ambayo ina mtandao na lazima uingize mtu au ununue miguu mwenyewe?

Tatizo la upatu ni hili hapa siku biashara inaacha kuingiza watu wapya inakufa na inapokufa ni sehemu ambayo wewe umeshawashawishi ndugu zako hata 20 tuu wajiunge. Mfano saa hizi package iliyo maarufu ni ya $1,996 sawa na milioni 4 ya kitanzania ikiwa na promise ya kupewa $ 171 kila wiki ambayo kwa haraka haraka itakuchukua miezi mitatu ili urudishe hiyo hela ila katika kipindi hicho utakuwa umeingiza watu wengie sema mfano hao 20 watakuwa wameweka milioni 80 na hawa 20 wakitafuta wao 20 kwenye benki ya wenye upatu atakuwa na bilioni 1.6 sasa fikiri hao mianne wakitafuta 20 tena kwahiyo wewe wa kwanza unaufaika mpaka mwisho wa watu 400 kwa hata kudouble hela yako lakini umeshaingiza watu billion 1.6 ambayo wewe umepewa millioni nne.

Hapa ndio maana hakuna serikali duniani inakubali biashara ya upatu au PONZI SCHEME ni hatari kwa taifa, hakunaga hela ambayo unaweza kupata kwa kudhulumu ikakuacha ulale vizuri. Somo tutafute njia halali za kutengeneza fedha bila kuumiza wegine.

Usiku mwema ni kwa amani epuka maneno makali tafakari kwa kina at what expenses you want to acquire wealth,
 
Kwanza mpaka na wewe unakubali kuingizwa kwenye hizi Ponzi scheme ambazo hata hazina chanzo cha uhakika na kinachoeleweka cha kuingiza pesa, basi itabidi uwe layman haswa kwenye financial world.

Fursa yoyote ambayo hili uweze kuwa profitable enough inakulazimu na wewe utafute mwenzako wa kujiunga na wewe, hiyo sio fursa tena bali ni walakini wa fursa!
 
Kuna wapumbavu wanafuatilia huo upumbavu utadhani wamejambwa vile...

Mtu badala ya kutafuta shamba akalime hata pilipili atafaidika maradufu, lakini akishapigiwa stori za hayo mafaida basi akili inamruka kichwani anawaza kashakuwa tajiri...

Hivi hayo madude yangekuwa yanatajirisha watu kihivyo, si kungekuwa na matajiri wengi wenye utajiri utokanao na upatu!!!
 
Kwanza mpaka na wewe unakubali kuingizwa kwenye hizi Ponzi scheme ambazo hata hazina chanzo cha uhakika na kinachoeleweka cha kuingiza pesa, basi itabidi uwe layman haswa kwenye financial world.

Fursa yoyote ambayo hili uweze kuwa profitable enough inakulazimu na wewe utafute mwenzako wa kujiunga na wewe, hiyo sio fursa tena bali ni walakini wa fursa!
mkuu mbona umebadilisha avatar picha yako ile ya lizarazu 98
 
Kwa kuwa mshauri karibu watu wamekuwa wakiniuliza kuhusu upatu mpya wa D9 Club na jibu langu limekuwa moja tu hiyo ni Deci nyingine ila inashangaza kuwa hao walioamua au waliotayari nikiwaambia hivyo mara moja wanapanicki nakutaka kusema wewe hujui na maneno mengi ya kashfa na wengine wamefikia kusema huoni wengine wanapata na jibu langu limebaki kuwa hakuna upatu unakuwa na mwisho mzuri full stop. Ila hii trend imenipa muda wa kujiuliza hivi kwanini kila baada ya muda kunazuka vitu kama hivi kulikuwa na kitu kinaitwa Dollar general miaka ya 1999 to 2000, na kikaja kile cha arusha miaka ya 2003 hapo , ikaja baba yao Deci 2008 to 2009 ikala wakutosha, ikatokea TELEFREE 2013 hii niliipiga vita nikatishiwa na maisha na watu niliowaona walikuwa wanainfluence za sasa 2017 D9 nayo imeshika kasi ubaya sana umekamata wasomi ambao watu wanawaamini sana ila hata kwa kufanya layman googling utaona shida tayari iko kwenye huu mfumo soma hii link D9 CLUB IS A FRAUD – ALERT! - Online Business Training. Sasa swali ambalo nimewauliza waliokuwa wanakuja kuniomba ushauri D9 inafanya biashara gani? spot betting hivi wewe unaweza kwenda kuweka fedha yako kwenye vibanda vya spot bet ukitegemea kuwa tajiri? ambazo zipo hapa mtaani kwetu jibu lao wengi ni hapana sasa kwanini unaamini kwenye ambayo inamtandao na lazima uingize mtu au ununue miguu mwenyewe?
Tatizo la upatu ni hili hapa siku biashara inaacha kuingiza watu wapya inakufa na inapokufa ni sehemu ambayo wewe umeshawashawishi ndugu zako hata 20 tuu wajiunge. Mfano saa hizi package iliyo maarufu ni ya $1,996 sawa na milioni 4 ya kitanzania ikiwa na promise ya kupewa $ 171 kila wiki ambayo kwa haraka haraka itakuchukua miezi mitatu ili urudishe hiyo hela ila katika kipindi hicho utakuwa umeingiza watu wengie sema mfano hao 20 watakuwa wameweka milioni 80 na hawa 20 wakitafuta wao 20 kwenye benki ya wenye upatu atakuwa na bilioni 1.6 sasa fikiri hao mianne wakitafuta 20 tena kwahiyo wewe wa kwanza unaufaika mpaka mwisho wa watu 400 kwa hata kudouble hela yako lakini umeshaingiza watu billion 1.6 ambayo wewe umepewa millioni nne. Hapa ndio maana hakuna serikali duniani inakubali biashara ya upatu au PONZI SCHEME ni hatari kwa taifa, hakunaga hela ambayo unaweza kupata kwa kuzulumu ikakuacha ulale vizuri. Somo tutafute njia halali za kutengeneza fedha bila kuumiza wegine.
Usiku mwema ni kwa amani epuka maneno makali tafakari kwa kina at what expenses you want to acquire wealth,
....masahihisho kidogo,
1.D9 siyo lazima uingize mtu ili utengeneze faida...hiyo ni option tu mojawapo
2.Hizi Biashara zenye risks kubwa siyo kwa kila mtu( hata wenyewe wanatoaga angalizo hili kama disclaimer), wengine endeleeni kulima na kufuga mpaka milele kwa hela za kudunduliza.
3.Mimi niliyethubutu kuwekeza kwenye biashara za aina hii zenye risks kubwa nina miradi ambayo ninaajiri watu kama nyie (sasa hivi nafanya contract farming kilimo cha madodoki kwa ajili ya wachina nimeanza na ekari 20 kule Ruvu ni hela ya D9).
4.Natarajia kuanza mradi mkubwa wa Azolla kwa ajili ya chakula cha mifugo ,nimeshafanya pilot project mwitikio ni mkubwa na order zimekuwa nyingi nayo nitafanya on contractual basis,na hii nitawaajiri watu kama nyie ....hii ni hela toka online business platforms....
5.Inawezekana ni kweli D9 ni upatu lakini NIFANYAJE?,..toa mawazo mbadala ,kwangu naamini no risk no money
6.Tunawahitaji sana watu kama nyie ili tupate nguvu kazi katika miradi yetu inayotokana na kuogopa kwenu...hapo ndipo utakapo mvulia Mungu kofia manake hiyo ni simply balance of nature.....................
 
Kuna wapumbavu wanafuatilia huo upumbavu utadhani wamejambwa vile...

Mtu badala ya kutafuta shamba akalime hata pilipili atafaidika maradufu, lakini akishabigiwa stori za hayo mafaida basi akili inamruka kichwani anawaza kashakuwa tajiri...

Hivi hayo madude yangekuwa yanatajirisha watu kihivyo, si kungekuwa na matajiri wengi wenye utajiri utokanao na upatu!!!


1.Hizi Biashara zenye risks kubwa siyo kwa kila mtu( hata wenyewe wanatoaga angalizo hili kama disclaimer), wengine endeleeni kulima na kufuga mpaka milele kwa hela za kudunduliza.
2.Mimi niliyethubutu kuwekeza kwenye biashara za aina hii zenye risks kubwa nina miradi ambayo ninaajiri watu kama nyie (sasa hivi nafanya contract farming kilimo cha madodoki kwa ajili ya wachina nimeanza na ekari 20 kule Ruvu ni hela ya D9).
3.Natarajia kuanza mradi mkubwa wa Azolla kwa ajili ya chakula cha mifugo ,nimeshafanya pilot project mwitikio ni mkubwa na order zimekuwa nyingi nayo nitafanya on contractual basis,na hii nitawaajiri watu kama nyie ....hii ni hela toka online business platforms....
4.Inawezekana ni kweli D9 ni upatu lakini NIFANYAJE?,..toa mawazo mbadala ,kwangu naamini no risk no money
5.Tunawahitaji sana watu kama nyie ili tupate nguvu kazi katika miradi yetu inayotokana na kuogopa kwenu...hapo ndipo utakapo mvulia Mungu kofia manake hiyo ni simply balance of nature.....................
 
Upo?
Kuna wapumbavu wanafuatilia huo upumbavu utadhani wamejambwa vile...

Mtu badala ya kutafuta shamba akalime hata pilipili atafaidika maradufu, lakini akishabigiwa stori za hayo mafaida basi akili inamruka kichwani anawaza kashakuwa tajiri...

Hivi hayo madude yangekuwa yanatajirisha watu kihivyo, si kungekuwa na matajiri wengi wenye utajiri utokanao na upatu!!!
 
....masahihisho kidogo,
1.D9 siyo lazima uingize mtu ili utengeneze faida...hiyo ni option tu mojawapo
2.Hizi Biashara zenye risks kubwa siyo kwa kila mtu( hata wenyewe wanatoaga angalizo hili kama disclaimer), wengine endeleeni kulima na kufuga mpaka milele kwa hela za kudunduliza.
3.Mimi niliyethubutu kuwekeza kwenye biashara za aina hii zenye risks kubwa nina miradi ambayo ninaajiri watu kama nyie (sasa hivi nafanya contract farming kilimo cha madodoki kwa ajili ya wachina nimeanza na ekari 20 kule Ruvu ni hela ya D9).
4.Natarajia kuanza mradi mkubwa wa Azolla kwa ajili ya chakula cha mifugo ,nimeshafanya pilot project mwitikio ni mkubwa na order zimekuwa nyingi nayo nitafanya on contractual basis,na hii nitawaajiri watu kama nyie ....hii ni hela toka online business platforms....
5.Inawezekana ni kweli D9 ni upatu lakini NIFANYAJE?,..toa mawazo mbadala ,kwangu naamini no risk no money
6.Tunawahitaji sana watu kama nyie ili tupate nguvu kazi katika miradi yetu inayotokana na kuogopa kwenu...hapo ndipo utakapo mvulia Mungu kofia manake hiyo ni simply balance of nature.....................
Hahahaha, ndio yale ya nilikua meneja TRA nikaacha kazi nikajiunga na D9 sasa napata mshahara wa milioni 30 na blah blah nyiiingi, huyo anaedai anapata mshahara wa milioni 30 hana hata gari wala nyumba.

Ukishaona kitu chochote kinakwambia ulete mwanachama mpya utapata kamishemi iogope kama ukomaD9 ni utapeli kama utapeli mwingine, haijalishi wewe unapata au la.

Vipi mzee wewe utasafiri lini kwenda marekani, china, Dubai, maana ndio hua fiksi zenu.
 
Hahahaha, ndio yale ya nilikua meneja TRA nikaacha kazi nikajiunga na D9 sasa napata mshahara wa milioni 30 na blah blah nyiiingi, huyo anaedai anapata mshahara wa milioni 30 hana hata gari wala nyumba.

Ukishaona kitu chochote kinakwambia ulete mwanachama mpya utapata kamishemi iogope kama ukomaD9 ni utapeli kama utapeli mwingine, haijalishi wewe unapata au la.

Vipi mzee wewe utasafiri lini kwenda marekani, china, Dubai, maana ndio hua fiksi zenu.
 
Wenye mafanikio ni wale wasiogopa Risk.

Unaogopa kuacha kazi BOT na kuanzisha Biashara kubwa na mtaji unao.
 
Ahaha...mkuu na wewe umewahi kushiriki ule mchezo?
Hapana mkuu, ila naona kila mkoa wale jamaa wapo, mpaka Dar, mbagara, manzese, Ubungo.. Utakuta watu wamezunguka.. Nashangaa yaani mpaka Leo Kuna watu wajinga... Wanaishia kushinda soda tu.. Naona joketi alikuja katika Kijiwe chenu uko Songea
 
Hapana mkuu, ila naona kila mkoa wale jamaa wapo, mpaka Dar, mbagara, manzese, Ubungo.. Utakuta watu wamezunguka.. Nashangaa yaani mpaka Leo Kuna watu wajinga... Wanaishia kushinda soda tu.. Naona joketi alikuja katika Kijiwe chenu uko Songea
Mkuu nilivyokuwa primary school kwenye ule mchezo mimi nilikula sana biskuti zao! Yaani nilikuwa nalenga biskuti tu mimi wala sio hela, waliokuwa wanaliwa ni wale wapenda hela eti mtu atanunua maringi kumi hili atafute buku wakati vibao vyote vya 500 na 1000 vilikuwa ni vikubwa kuliko size ya mdomo wa ringi na hata hawakushtuka.
 
Back
Top Bottom