mara nyingi sana nikisikia mtu fulan amefariki basi ntasikia sifa lukuki kwa marehemu tena unakuta sifa nyingine hata hazimuhusu marehemu hivi hii husababishwa na nini?
Kwa kawaida sisi binadamu hujawa na roho za huzuni na kumbukumbu ya mazuri ya marehemu wala siyo mabaya , mabaya ya marehemu siyo huwezi kuyafikiri lasivyo utakuwa kichaa
Tunawasifia marehemu hata kama hawakustahili sifa kwasababu sisi wenyewe ni WATUPU...hatuna la kujisifia, hatujiamini na tunaogopa tukifa hatutakumbukwa kwa lolote. Kuwasifia marehemu kwetu ni kuweka akiba ili nasi tukifa waliobaki watusifie hata kama katika uhai wetu hatukuwahi kufanye jambo lolote la kuisaidia jamii.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.