Hivi kwanini Tanga hainyang'anywi hadhi ya kuwa Jiji? Ni sehemu ya ajabu sana

Hivi kwa nini Tanga ni Jiji, maana naona pilikapilika kama za majiji mengine hazipo kabisa, ni Mji ambao umepoa mithiri ya Tabora, baiskeli huku ndio nyingi kuliko magari.

Vijiwe vya vijana vipo kila mahala, huku maisha ni mepesi sana, yaani ukiwa na 500 unakula ugali na mboga za majani.

Ukienda kula wali samaki unapewa kibua mzima na wali eti elfu 2. Nyumba za majani zipo mpaka katikati ya mji, nyumba zenye vibaraza vikubwa zile za kizamani ndio zimejaa.

Nyumba za matofali ya tope zipo kila mahala. Nyumba za miti pia bado zipo.

Wale wanawake wazuri wa Kitanga wala huku siwaoni kabisa, hivi hii ndio Tanga niliyokuwa naisikia nikiwa Dar es Salaam. Au kuna Tanga nyingine wakuu? Tofauti na hii ya Forodhani, Chumbageni, 16, Donge, Majani Mapana, Gofu Chini n.k.

Sehemu za kula bata Tanga hazipo kabisa. Wanawake wa huku wanapenda wageni sana kuliko wenyeji sijui kwa nini?

Kiukweli Tanga ni sawa na Tabora tu, Wala Tanga haina hadhi ya kuwa Jiji.
Acha mambo ya ki_se_geju wewe karibu tanga! Ushamba na wivu achana navyo unapofika tanga..nyumbu_si weye
 
Labda amemaanisha huu upande wa kutokea stendi kubwa ya zamani kupandisha barabara ya kwenda "Kwetu pazuri" ila nimepasahau jina kidogo nafikiri panaitwa Chuda wanakaa waarabu na kuna lodge nyingi nzuri nzuri
Ndio kunaitwa Chuda, Chuda ni makazi ya watu wa kipato cha kati, kama umefika Tanga ukaishia Chuda na kutumia kigezo hicho kujudge ni kama Mtu aje Dar afike mwananyamala hAlafu aanze kuponda.
 
Hivi kwa nini Tanga ni Jiji, maana naona pilikapilika kama za majiji mengine hazipo kabisa, ni Mji ambao umepoa mithiri ya Tabora, baiskeli huku ndio nyingi kuliko magari.

Vijiwe vya vijana vipo kila mahala, huku maisha ni mepesi sana, yaani ukiwa na 500 unakula ugali na mboga za majani.

Ukienda kula wali samaki unapewa kibua mzima na wali eti elfu 2. Nyumba za majani zipo mpaka katikati ya mji, nyumba zenye vibaraza vikubwa zile za kizamani ndio zimejaa.

Nyumba za matofali ya tope zipo kila mahala. Nyumba za miti pia bado zipo.

Wale wanawake wazuri wa Kitanga wala huku siwaoni kabisa, hivi hii ndio Tanga niliyokuwa naisikia nikiwa Dar es Salaam. Au kuna Tanga nyingine wakuu? Tofauti na hii ya Forodhani, Chumbageni, 16, Donge, Majani Mapana, Gofu Chini n.k.

Sehemu za kula bata Tanga hazipo kabisa. Wanawake wa huku wanapenda wageni sana kuliko wenyeji sijui kwa nini?

Kiukweli Tanga ni sawa na Tabora tu, Wala Tanga haina hadhi ya kuwa Jiji.
Nilishawahi kwenda sehemu inaitwa ‘La casa Chica’ mwaka 2009 nilipoenda field huko Tanga, na ndio nilionja bia yangu ya kwanza hapo, hivi bado ipo?
 
Tanga ya maajabu sana! Angalia
1. Mtoto atapigwa afe kama hakwenda "chuo", lakini formal school ni hiari yake!
2. Mwanamke anajipamba malaki mwilini lkn angalia nyumba anakotokea, hata Mbwa hawezi kukaa
3. Ni rahisi kuvunja ndoa kuliko kukosa dera.
4. Mwanamke kuwa na Madera 50 ni kawaida
5. Harusi ya kufa MTU ni kibarazani kwenye hema moja, " kinywaji" ni maandazi, maharage , ugali na muziki wa nguvu kwa siku tatu
5. Dini ya mtume SAW ni maisha yao Alfa na omega
6. Mzazi kumtukana mtoto matusi ya nguoni makali mfn mb....ya baba yako kawaida sana mbele ya kadamnasi.. udigoni

7. Mahari ni maelewano kati ya binti na kijana. mara nyingi huwa binti anataka godoro na ni lake akiachika analibeba

8. Ongezea......
Haha, mkuu umetisha sana
 
Kama una Akili Timamu pambana Sana kuishi maeneo haya
1.Dar es salaam
2.Tanga
3.Arusha
4.Mwanza
5.Morogoro
6. Pwani

Mikoa mingine ambayo hutakiwi kuishi Kama unajitambuwa na una Akili nzuri ,maana hata ukikomaa laziima ufe haraka na kuzeeka haraka ni mikoa ya
1.Dodoma
2.Iringa
3.Rukwa
4.Simiyu
5.Tabora
6.singida
7.Songwe
8.Njombe
9.Ruvuma
10.Shinyanga
11.Katavi
12.Mara
13.kigoma, huku ndiyo balaa
14.Na mikoa mingine iliyobaki siyo sehemu ya kuishi binadamu
No research no right to speak

Acha kutuaminisha vitu ambavyo unaamini wewe
 
taja viwanda 10 vilivyopo Tanga
Tanga ina viwanda vingi zaidi ya kumi ila kwa kuwa unataka nikutajie viwanda kumi tu, ni kama ifuatavyo;
1. Kiwanda cha Saruji- Simba Cement.
2. Kiwanda cha chai - Mponde.
3. Kiwanda cha katani.
4. Kiwanda cha chokaa.
5. Kiwanda cha Soda pendwa tanga Anjari.
6. Kiwanda cha Mafuta ya kupaka Babycare.
7. Kiwanda cha Vestline kinatengeneza Powder.
8. Kiwanda cha Mafuta ya kula.
9. Kiwanda cha Mifuko PPTL kange.
10. Kiwanda cha Ngano kange.
11. Kiwanda cha Maziwa kange tangafresh. na vingine vingi tanga raha.
 
Back
Top Bottom