Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,477
- 30,130
Nianze bandiko langu kwa kunukuu sheria mama ya nchi hii ambayo ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, ibara ya 18(1) ambayo inasema hivi "Kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi na pia ana Uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa na mtu yoyote" mwisho wa kunukuu
Nimenukuu ibara hiyo ili tuone katika sakata hili alilolianzisha Spika Ndugai ya kumuita CAG, Profesa Mussa Assad, katika kamati yake ya maadili, hapo tarehe 21/01/2019, tena kwa kupitia vyombo vya habari na kwa kutumia vitisho vya hali ya juu kuwa asipofika mwenyewe kwa hiari yake ataletwa kwa pingu, kama lina uhalali
Baada ya kunukuu ibara hiyo muhimu kwenye sheria mama, ambayo ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tuangalie hivi kwa kutoa mawazo yake nje yanayohusu nchi yake, Profesa Assad amefanya kosa gani hadi aitwe kwenye kamati ya maadili ya Bunge, tena kwa kupigwa mkwara mzito kuwa ataburuzwa kwenye kamati hiyo hata kwa pingu??
Nakumbuka kwenye awamu ya nne, mbunge wa Kibamba Mheshimiwa, John Mnyika aliwahi muita Rais wa awamu hiyo, Jakaya Kikwete, kuwa ni dhaifu, mbona Rais huyo hakutumia vyombo vyake vya usalama kumweka ndani??
Badala yake Rais huyo mstaafu wa awamu ya nne, akaamua "kupotezea" tu kwa kuwa alijua huyo Mnyika hakufanya kosa, Bali ametumia haki yake ya kikatiba
Ninachojiuliza mbona Spika Ndugai anatumia nguvu kubwa sana, katika kulilinda Bunge lake linapoitwa dhaifu, hadi kutaka kulitumia Jeshi letu la Polisi liwalete watuhumiwa hao kwenye kamati hiyo wakiwa wamefungwa pingu mikononi??
Hivi ni kitu gani anachojihami nacho Spika Ndugai hadi awe mbogo kiasi hicho kikubwa??
Hivi siyo kweli kuwa Bunge lake siyo dhaifu??
Kama siyo kweli ilikuwaje Bunge lake likaondoa Bunge Live wakati wananchi karibu wote walikuwa wanataka kuwaona wawakilishi wao namna wanavyotoa hoja zao za namna wanavyoisimamia serikali yetu??
Hivi kama Bunge lake siyo dhaifu inakuwaje kwenye Bajeti za maendeleo zinafika chini ya asilimia 30 kwenye maeneo mengi??
Hivi inakuwaje kama Bunge lake siyo dhaifu, baadhi ya maeneo "yapendelewe' kupita kiasi na kupata zaidi ya asilimia 200 ya bajeti iliyotengwa ya maendeleo na Bunge??
Kama Bunge lake siyo dhaifu, hivi ile triliion 1.5 aliyoitolea Maelezo CAG, kuwa matumizi yake hayajulikani, hivi ni juhudi gani Bunge lake limechukua kuihoji serikali ziliko hizo shilingi trillion 1.5??
Hivi kama Bunge lake siyo dhaifu, anaweza kuelezea serikali inapata wapi pesa yake taslimu ya kununua hizi ndege za dreamliners na Airbus zinazokuja nchini ambazo hazijatengewa pesa hizo na chombo pekee cha kupanga bajeti, ambacho ni Bunge??
Haya ni baadhi ya maswali machache ambayo tunamtaka Spika Ndugai ayajibu
Nimenukuu ibara hiyo ili tuone katika sakata hili alilolianzisha Spika Ndugai ya kumuita CAG, Profesa Mussa Assad, katika kamati yake ya maadili, hapo tarehe 21/01/2019, tena kwa kupitia vyombo vya habari na kwa kutumia vitisho vya hali ya juu kuwa asipofika mwenyewe kwa hiari yake ataletwa kwa pingu, kama lina uhalali
Baada ya kunukuu ibara hiyo muhimu kwenye sheria mama, ambayo ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tuangalie hivi kwa kutoa mawazo yake nje yanayohusu nchi yake, Profesa Assad amefanya kosa gani hadi aitwe kwenye kamati ya maadili ya Bunge, tena kwa kupigwa mkwara mzito kuwa ataburuzwa kwenye kamati hiyo hata kwa pingu??
Nakumbuka kwenye awamu ya nne, mbunge wa Kibamba Mheshimiwa, John Mnyika aliwahi muita Rais wa awamu hiyo, Jakaya Kikwete, kuwa ni dhaifu, mbona Rais huyo hakutumia vyombo vyake vya usalama kumweka ndani??
Badala yake Rais huyo mstaafu wa awamu ya nne, akaamua "kupotezea" tu kwa kuwa alijua huyo Mnyika hakufanya kosa, Bali ametumia haki yake ya kikatiba
Ninachojiuliza mbona Spika Ndugai anatumia nguvu kubwa sana, katika kulilinda Bunge lake linapoitwa dhaifu, hadi kutaka kulitumia Jeshi letu la Polisi liwalete watuhumiwa hao kwenye kamati hiyo wakiwa wamefungwa pingu mikononi??
Hivi ni kitu gani anachojihami nacho Spika Ndugai hadi awe mbogo kiasi hicho kikubwa??
Hivi siyo kweli kuwa Bunge lake siyo dhaifu??
Kama siyo kweli ilikuwaje Bunge lake likaondoa Bunge Live wakati wananchi karibu wote walikuwa wanataka kuwaona wawakilishi wao namna wanavyotoa hoja zao za namna wanavyoisimamia serikali yetu??
Hivi kama Bunge lake siyo dhaifu inakuwaje kwenye Bajeti za maendeleo zinafika chini ya asilimia 30 kwenye maeneo mengi??
Hivi inakuwaje kama Bunge lake siyo dhaifu, baadhi ya maeneo "yapendelewe' kupita kiasi na kupata zaidi ya asilimia 200 ya bajeti iliyotengwa ya maendeleo na Bunge??
Kama Bunge lake siyo dhaifu, hivi ile triliion 1.5 aliyoitolea Maelezo CAG, kuwa matumizi yake hayajulikani, hivi ni juhudi gani Bunge lake limechukua kuihoji serikali ziliko hizo shilingi trillion 1.5??
Hivi kama Bunge lake siyo dhaifu, anaweza kuelezea serikali inapata wapi pesa yake taslimu ya kununua hizi ndege za dreamliners na Airbus zinazokuja nchini ambazo hazijatengewa pesa hizo na chombo pekee cha kupanga bajeti, ambacho ni Bunge??
Haya ni baadhi ya maswali machache ambayo tunamtaka Spika Ndugai ayajibu