Hivi kwanini Spika Ndugai anageuka mbogo sana Bunge lake linapoitwa dhaifu na kuamua kumuita mtu huyo kwenye Kamati ya maadili?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,477
30,130
Nianze bandiko langu kwa kunukuu sheria mama ya nchi hii ambayo ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, ibara ya 18(1) ambayo inasema hivi "Kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi na pia ana Uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa na mtu yoyote" mwisho wa kunukuu

Nimenukuu ibara hiyo ili tuone katika sakata hili alilolianzisha Spika Ndugai ya kumuita CAG, Profesa Mussa Assad, katika kamati yake ya maadili, hapo tarehe 21/01/2019, tena kwa kupitia vyombo vya habari na kwa kutumia vitisho vya hali ya juu kuwa asipofika mwenyewe kwa hiari yake ataletwa kwa pingu, kama lina uhalali

Baada ya kunukuu ibara hiyo muhimu kwenye sheria mama, ambayo ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tuangalie hivi kwa kutoa mawazo yake nje yanayohusu nchi yake, Profesa Assad amefanya kosa gani hadi aitwe kwenye kamati ya maadili ya Bunge, tena kwa kupigwa mkwara mzito kuwa ataburuzwa kwenye kamati hiyo hata kwa pingu??

Nakumbuka kwenye awamu ya nne, mbunge wa Kibamba Mheshimiwa, John Mnyika aliwahi muita Rais wa awamu hiyo, Jakaya Kikwete, kuwa ni dhaifu, mbona Rais huyo hakutumia vyombo vyake vya usalama kumweka ndani??

Badala yake Rais huyo mstaafu wa awamu ya nne, akaamua "kupotezea" tu kwa kuwa alijua huyo Mnyika hakufanya kosa, Bali ametumia haki yake ya kikatiba

Ninachojiuliza mbona Spika Ndugai anatumia nguvu kubwa sana, katika kulilinda Bunge lake linapoitwa dhaifu, hadi kutaka kulitumia Jeshi letu la Polisi liwalete watuhumiwa hao kwenye kamati hiyo wakiwa wamefungwa pingu mikononi??

Hivi ni kitu gani anachojihami nacho Spika Ndugai hadi awe mbogo kiasi hicho kikubwa??

Hivi siyo kweli kuwa Bunge lake siyo dhaifu??

Kama siyo kweli ilikuwaje Bunge lake likaondoa Bunge Live wakati wananchi karibu wote walikuwa wanataka kuwaona wawakilishi wao namna wanavyotoa hoja zao za namna wanavyoisimamia serikali yetu??

Hivi kama Bunge lake siyo dhaifu inakuwaje kwenye Bajeti za maendeleo zinafika chini ya asilimia 30 kwenye maeneo mengi??

Hivi inakuwaje kama Bunge lake siyo dhaifu, baadhi ya maeneo "yapendelewe' kupita kiasi na kupata zaidi ya asilimia 200 ya bajeti iliyotengwa ya maendeleo na Bunge??

Kama Bunge lake siyo dhaifu, hivi ile triliion 1.5 aliyoitolea Maelezo CAG, kuwa matumizi yake hayajulikani, hivi ni juhudi gani Bunge lake limechukua kuihoji serikali ziliko hizo shilingi trillion 1.5??

Hivi kama Bunge lake siyo dhaifu, anaweza kuelezea serikali inapata wapi pesa yake taslimu ya kununua hizi ndege za dreamliners na Airbus zinazokuja nchini ambazo hazijatengewa pesa hizo na chombo pekee cha kupanga bajeti, ambacho ni Bunge??

Haya ni baadhi ya maswali machache ambayo tunamtaka Spika Ndugai ayajibu
 
Muhurumie mgonjwa.
Ndiyo maana tunamuuliza Spika Ndugai hivi kuna athari gani kwa mtu kutoa maoni yake kuhusiana na mwenendo wa nchi yake na kukiita chombo chake cha Bunge ni dhaifu??

Hivi inapotokea kwa mfano watani wa jadi Simba na Yanga, mmoja wake akamuita mwenzake timu dhaifu

Hivi si ndiyo timu iliyoitwa dhaifu siku ya mechi itajitahidi imfunge huyo mtani wake wa jadi ili kuthibitisha kuwa siyo dhaifu??

Hivi kama chombo cha Bunge kinaitwa dhaifu, hivi si ndiyo chombo hicho kingefanya juhudi ili kiwathibitishie wananchi kuwa chombo hicho siyo dhaifu??

Badala ya Spika Ndugai kutaka kutumia mabavu ya kuwaleta watuhumiwa hao kwenye kamati ya maadili ya Bunge tena wakiwa wamefungwa pingu mikononi!
 
Ndiyo maana tunamuuliza Spika Ndugai hivi kuna athari gani kwa mtu kutoa maoni yake kuhusiana na mwenendo wa nchi yake na kukiita chombo chake cha Bunge ni dhaifu??

Hivi inapotokea kwa mfano watani wa jadi Simba na Yanga, mmoja wake akamuita mwenzake timu dhaifu

Hivi si ndiyo timu iliyoitwa dhaifu siku ya mechi itajitahidi imfunge huyo mtani wake wa jadi ili kuthibitisha kuwa siyo dhaifu??

Hivi kama chombo cha Bunge kinaitwa dhaifu, hivi si ndiyo chombo hicho kingefanya juhudi ili kiwathibitishie wananchi kuwa chombo hicho siyo dhaifu??

Badala ya Spika Ndugai kutaka kutumia mabavu ya kuwaleta watuhumiwa hao kwenye kamati ya maadili ya Bunge tena wakiwa wamefungwa pingu mikononi??
Ni nadra sana kwa Mwafrika kuukubali ukweli na kuufanyia kazi bila inda/kinyongo.Maoni yangu kwa ufupi ni hayo mkuu.
 
Hahaahaa......:D:D
Kwa sababu:Mtu mzima wa mwili na akili akipokwa mavazi yake yenye kumsitiri mwili wote huchutama. Na ndiyo matarajio yetu wengi ili akipiga yowe kuomba msaada apelekewe lubega ajisitiri. Sasa ukishuhudia mtu huyo kaachwa mtupu halafu anapanda juu ya paa la nyumba na kudai mavazi yake kwa hasira iliyofura unapata jibu gani? 😂😂😂😂😂
 
Wakuu mpo munaendelea na mada kuhusu huyu jamaa hata usiumize kichwa najua walijipanga kututawala kitemi ndio sababu ya kiburi chote wakiamini hakuna wakuja kuwahoji kisheria kwakua bunge ni rabble stamps mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Huo ndiyo ukweli kwa asilimia 100

Ndugai anajua kuwa CAG, Mussa Assad ameuelezea ukweli mchungu na yeye Spika Ndugai anaamini kazi ya mhimili wake wa Bunge siyo kuisimamia serikali, badala yake ni kukubaliana na serikali kwa asilimia 100 kwa kila kinacholetwa pale Bungeni!

Hicho ndiyo kiini cha CAG kutishwa kama "nyau" kuwa ataletwa kwenye kamati ya maadili huku akiwa amefungwa pingu na Jeshi la Polisi
 
Huo ndiyo ukweli kwa asilimia 100

Ndugai anajua kuwa CAG, Mussa Assad ameuelezea ukweli mchungu na yeye Spika Ndugai anaamini kazi ya mhimili wake wa Bunge siyo kuisimamia serikali, badala yake ni kukubaliana na serikali kwa asilimia 100 kwa kila kinacholetwa pale Bungeni!

Hicho ndiyo kiini cha CAG kutishwa kama "nyau" kuwa ataletwa kwenye kamati ya maadili huku akiwa amefungwa pingu na Jeshi la Polisi
Na hapo ndipo swali huzuka:Wana ubavu wa kulikana jina walilobatizwa(bunge,mahakama,sehemu ilo baki ya kiutendaji)? The United Republic of Gangsters! Kila kitu wao ni kutishia au kutumia mabavu tu. Kwa nini?
 
Unajua watu wa nchi unayoiongelea muda huu wamelala bado unamuwaza MWANAUME mwenzio Ndugai mida hi?, hivi hamnaga hata mademu wa kuwaweka bize msikae mnawaza siasa?,watu wamemjadili Spika Weeeeeeeeeeee, na thread Kama 50 au zaidi bado unaumiza kichwa kuhusu Ndugai na CAG?, yote yaliyoongelewa karibu wiki bado hujagundua unapoteza muda wako bure?,hivi ukiwakuta Spika na CAG next week wanakula msosi meza moja IKULU utafanyaje?, Ndo maana mimi huwa siwafichi kuwaita WAPUMBAVU, tafuteni kazi za kuwaweka bize siasa zinawaletea ujinga vichwani mwenu.
 
Unajua watu wa nchi unayoiongelea muda huu wamelala bado unamuwaza MWANAUME mwenzio Ndugai mida hi?, hivi hamnaga hata mademu wa kuwaweka bize msikae mnawaza siasa?,watu wamemjadili Spika Weeeeeeeeeeee, na thread Kama 50 au zaidi bado unaumiza kichwa kuhusu Ndugai na CAG?, yote yaliyoongelewa karibu wiki bado hujagundua unapoteza muda wako bure?,hivi ukiwakuta Spika na CAG next week wanakula msosi meza moja IKULU utafanyaje?, Ndo maana mimi huwa siwafichi kuwaita WAPUMBAVU, tafuteni kazi za kuwaweka bize siasa zinawaletea ujinga vichwani mwenu.
Wakati unapost huu UZUZU wewe hukuwa na Demu? Na kama ulikuwa naye amekuruhusuje kuacha kumkumbatia na kuanza kuandika upuuzi? Kama hukuwa na Demu ulishidwaje kutafuta badala yake ukaja kuleta Upupu huku JF?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nianze bandiko langu kwa kunukuu sheria mama ya nchi hii ambayo ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, ibara ya 18(1) ambayo inasema hivi "Kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zizote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi na pia ana Uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa na mtu yoyote" mwisho wa kunukuu

Nimenukuu ibara hiyo ili tuone katika sakata hili alilolianzisha Spika Ndugai ya kumuita CAG, Profesa Mussa Assad, katika kamati yake ya maadili, hapo tarehe 21/01/2019, tena kwa kupitia vyombo vya habari na kwa kutumia vitisho vya hali ya juu kuwa asipofika mwenyewe kwa hiari yake ataletwa kwa pingu, kama lina uhalali

Baada ya kunukuu ibara hiyo muhimu kwenye sheria mama, ambayo ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tuangalie hivi kwa kutoa mawazo yake nje yanayohusu nchi yake, Profesa Assad amefanya kosa gani hadi aitwe kwenye kamati ya maadili ya Bunge, tena kwa kupigwa mkwara mzito kuwa ataburuzwa kwenye kamati hiyo hata kwa pingu??

Nakumbuka kwenye awamu ya nne, mbunge wa Kibamba Mheshimiwa, John Mnyika aliwahi muita Rais wa awamu hiyo, Jakaya Kikwete, kuwa ni dhaifu, mbona Rais huyo hakutumia vyombo vyake vya usalama kumweka ndani??

Badala yake Rais huyo mstaafu wa awamu ya nne, akaamua "kupotezea" tu kwa kuwa alijua huyo Mnyika hakufanya kosa, Bali ametumia haki yake ya kikatiba

Ninachojiuliza mbona Spika Ndugai anatumia nguvu kubwa sana, katika kulilinda Bunge lake linapoitwa dhaifu, hadi kutaka kulitumia Jeshi letu la Polisi liwalete watuhumiwa hao kwenye kamati hiyo wakiwa wamefungwa pingu mikononi??

Hivi ni kitu gani anachojihami nacho Spika Ndugai hadi awe mbogo kiasi hicho kikubwa??

Hivi siyo kweli kuwa Bunge lake siyo dhaifu??

Kama siyo kweli ilikuwaje Bunge lake likaondoa Bunge Live wakati wananchi karibu wote walikuwa wanataka kuwaona wawakilishi wao namna wanavyotoa hoja zao za namna wanavyoisimamia serikali yetu??

Hivi kama Bunge lake siyo dhaifu inakuwaje kwenye Bajeti za maendeleo zinafika chini ya asilimia 30 kwenye maeneo mengi??

Hivi inakuwaje kama Bunge lake siyo dhaifu, baadhi ya maeneo "yapendelewe' kupita kiasi na kupata zaidi ya asilimia 200 ya bajeti iliyotengwa ya maendeleo na Bunge??

Kama Bunge lake siyo dhaifu, hivi ile triliion 1.5 aliyoitolea Maelezo CAG, kuwa matumizi yake hayajulikani, hivi ni juhudi gani Bunge lake limechukua kuihoji serikali ziliko hizo shilingi trillion 1.5??

Hivi kama Bunge lake siyo dhaifu, anaweza kuelezea serikali inapata wapi pesa yake taslimu ya kununua hizi ndege za dreamliners na Airbus zinazokuja nchini ambazo hazijatengewa pesa hizo na chombo pekee cha kupanga bajeti, ambacho ni Bunge??

Haya ni baadhi ya maswali machache ambayo tunamtaka Spika Ndugai ayajibu

Hasheeem Thabiti ni kijana mrefu sana.
Akitokea mtu maeneo ya Morogoro akimwambia kuwa wewe Thabiti ni mfupi sana na huwezi kucheza basketball .
Nadhani Hasheeem atabaki kucheka tu na kuendelea na safari zake.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hasheeem Thabiti ni kijana mrefu sana.
Akitokea mtu maeneo ya Morogoro akimwambia kuwa wewe Thabiti ni mfupi sana na huwezi kucheza basketball .
Nadhani Hasheeem atabaki kucheka tu na kuendelea na safari zake.


Sent using Jamii Forums mobile app
That' very true

Hivi nini kingempungukia iwapo Spika Ndugai angejifanya kampuuza CAG??

Kama CAG kadai Bunge lake ni dhaifu na yeye Ndugai anaamini kuwa Bunge lake siyo dhaifu, basi maisha yangeendelea tu kama ambavyo Rais mstaafu, Jakaya Kikwete aliitwa dhaifu na Mbunge John Mnyika na yeye akapotezea...........

Badala ya kuamuru vyombo vyake vya usalama vimuweke ndani Mnyika, kwa kuwa huyo Rais mstaafu alijua kuwa Mnyika ametumia haki yake ya kikatiba
 
Hivi Spika Ndugai ameshaisoma Katiba ya nchi ambayo ndiyo sheria mama nchi hii??

Katika ibara ya 143(6) inasema hivi nanukuu "Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu HATALAZIMIKA kufuata amri au maagizo ya mtu mwingine yoyote au idara yoyote ya serikali, lakini Maelezo haya ya ibara ndogo hayataizuia Mahakama kutumia madaraka yake kwa ajili ya kuchunguza kama Mdhibiti Mkuu wa Hesabu ametekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii" mwisho wa kunukuu

Kwa Maelezo hayo hapo juu ni kuwa Spika Ndugai hana mamlaka ya kumuita CAG kwenye kamati yake ya maadili na chombo pekee kilichopewa mamlaka ya kum-summon CAG ni mahalama. OVA
 
Kwa sababu ni team moja na Magufuli mafisadi wezi na majambazi na wanamission za kuondolea uhai watu kama ilivyotokea kwa Lissu spika na naibu wake wote walijuwa
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom