Kwa kifupi tu, sie wanasimba kwa nini tunakuwa wajinga kiasi hiki? Huyu Mohamed Dewji alinunua hisa 49%kwa bilioni 20 shilingi za kitanzania. Hadi leo hakuzilipa.Kinachoendelea ni kuchagua wanachama 800 kuwaweka ukumbi wa kisasa wa mikutano wa Jakaya Kikwete,na vibaraka wake kuanza kutoa maneno kemkem.
Simba pekee ina wanachama mamilioni ukiachia wapenzi (club supporters) lakini wamewekwa 800 ili wamsikie ceo atudanganye kwa vijimaneno na majigambo yasiyokuwa na tija.
Isitoshe akaja mkuu wa idara ya fedha akadai eti Dewji katoa bilioni 5 nje ya hizo bilioni 20.Jamani kiakili tu hatuna shida yoyote na hizo pesa za pembeni.
Ikiwa kanunua 49% basi alipe kwanza hizo bilioni 20 kwa klabu na zithibitishwe na wahusika ndio mengine yafuate.
Kila kukicha hawa vibaraka wanakwepa kuitaja hiyo bilioni 20,wanataja katoa bilioni 5 sijui milioni ngapi n.K wanasimba tumemuuzia mohamed dewji asilimia 49 kwa billioni 20 azilipe ndio apewe hisa zake vingenevyo tutakuwa wajinga sana.
Kwa mujibu wa gazeti maarufu la michezo nchini liitwalo mwanaspoti urais wa heshima hupewa mtu aliyewahi kushikilia nafasi hiyo kisha akastaafu kitu ambacho hakijawahi kutokea kwa mo dewji kuwa rais wa klabu hii.
Cheo hiki kiliasisisiwa na akina aden rage akafuata aveva kabla ya kubadilishwa na kurejeshwa nafasi ya uenyekiti ukianzia na nkwabi n.K.
Wanasimba tuamke,vingenevyo aturudishie hiyo asilimia 49 tuiuze kwa mwekezaji ambaye ataweza kununua hata kwa bilioni 40 na sio 20, ambazo kwa maono yangu ni ndogo sana ukilinganisha na ukubwa wa klabu au tuuze hizo asilimia 49 kwenye soko la hisa la Dar,Nairobi,Joburg Afrika Kusini,hata London stock market.
Simba ni timu kubwa sana africa kuliko tunavyofikiria. Uamuzi upo kwenu mamilioni ya wanachama na wapenzi.
Naomba kuwasilisha.
Simba pekee ina wanachama mamilioni ukiachia wapenzi (club supporters) lakini wamewekwa 800 ili wamsikie ceo atudanganye kwa vijimaneno na majigambo yasiyokuwa na tija.
Isitoshe akaja mkuu wa idara ya fedha akadai eti Dewji katoa bilioni 5 nje ya hizo bilioni 20.Jamani kiakili tu hatuna shida yoyote na hizo pesa za pembeni.
Ikiwa kanunua 49% basi alipe kwanza hizo bilioni 20 kwa klabu na zithibitishwe na wahusika ndio mengine yafuate.
Kila kukicha hawa vibaraka wanakwepa kuitaja hiyo bilioni 20,wanataja katoa bilioni 5 sijui milioni ngapi n.K wanasimba tumemuuzia mohamed dewji asilimia 49 kwa billioni 20 azilipe ndio apewe hisa zake vingenevyo tutakuwa wajinga sana.
Kwa mujibu wa gazeti maarufu la michezo nchini liitwalo mwanaspoti urais wa heshima hupewa mtu aliyewahi kushikilia nafasi hiyo kisha akastaafu kitu ambacho hakijawahi kutokea kwa mo dewji kuwa rais wa klabu hii.
Cheo hiki kiliasisisiwa na akina aden rage akafuata aveva kabla ya kubadilishwa na kurejeshwa nafasi ya uenyekiti ukianzia na nkwabi n.K.
Wanasimba tuamke,vingenevyo aturudishie hiyo asilimia 49 tuiuze kwa mwekezaji ambaye ataweza kununua hata kwa bilioni 40 na sio 20, ambazo kwa maono yangu ni ndogo sana ukilinganisha na ukubwa wa klabu au tuuze hizo asilimia 49 kwenye soko la hisa la Dar,Nairobi,Joburg Afrika Kusini,hata London stock market.
Simba ni timu kubwa sana africa kuliko tunavyofikiria. Uamuzi upo kwenu mamilioni ya wanachama na wapenzi.
Naomba kuwasilisha.