Hivi kwanini Serikali na wabunge wa CCM mliamua kutukatili wafanyakazi suala la mafao?

Nov 21, 2018
29
26
Nasikitika sana kuona serikali inatulazimisha kuwa maskini. Ni ngumu sana kwa mfanyakazi kuwa tajiri kwa kutegemea kuajiriwa.

NSSF wanapokea kiasi cha asilimia 20 (10 kwangu + 10 mwajiri) hapo hapo Serikali nayo wanakata kiasi cha asilimia zisizopungua 25 mpaka 30 ya mshahara wangu kama kodi.

Sasa inafika Mahali nataka kujiajiri nifanye biashara zangu nashindwa kutokana na kuminywa sana.

Najifariji na pesa yangu iliyopo NSSF kwamba nitaichukua nikafanyie biashara nayo nakuta viongozi na wabunge CCM nao wameikodolea macho na tiyari wameshaiwekea pin kwamba siwezi kuichukua mpaka nifikishe miaka 55 ya kustaafu au 60.

Sasa najaribu kujiuliza Miaka 60 nitaweza kufanya biashara ya ushindani kweli? jibu ni hapana na pia kipindi hicho nguvu zimeshapungua.

Ombi langu kwa viongozi na wabunge Jaribuni tena kuangalia hili swala msituburuze sana jamani haki yangu nipeni yakwenu chukueni Msitumie wingi wenu bungeni mkafikiria kwamba sisi ndio tumewatuma mimi binafsi sipendezwi kabisa na ndio zenu Bungeni. Kila kitu nyie "ndio".

USHAURI KWA NSSF

Fanyeni mchakato wa kukopesha wanachama wenu kama mtu ana kiasi fulani cha pesa basi awe na uwezo wa kukopa angalau nusu ya kiasi alichonacho kwenu ni njia pia ya kukuza uchumi kwenu.

Najua mtakuja na majibu ya Marekani hawafanyi hivi. wala sehemu zingine hawafanyi hivi sasa huwa najiuliza kikiwa kizuri kwenu mnaanza kujitetea na sheria za nchi zingine. Sio kila kitu cha kuiga nasi tufanye klitu wao watuige.

Nikiacha kazi nipewe pesa zangu. Mnafanyia biashara hata kuongezeka haziongezeki hivi unakuja kunipa milioni 100 nina miaka 60 sii kutaka kuniletea mtihani. Ndio maana watumishi wengi wakistahafu ndio wanajenga nyumba na pesa ya kustafia.

Tanzania kuna vitu vingi sana ambavyo serikali wanaweza wakafanya na wala wasitegemee pesa za wanachama wa NSSF.

Mfano serikali kuwekeza kwenye matumizi ya gas kwenye magari madogo na uzuri gas tunazalisha wenyewe hakuna shida, pia kuwekeza kwenye miundombinu kama reli za majiji; mfano kuchukua abiria kutoka Kibaha mpaka Mbande, Mbande Mpaka posta, Gongo la Mboto mpaka Posta, Yombo mpaka Posta nakadhalika.
 
Mkuu hili jambo linaumiza sana, wenye mamlaka wanasema lengo ni kumsaidia mfanyakazi uzeeni najiuliza hizo hela wakikaa nazo mpaka mtumishi afikishe umri uliowekwa kisheria je anakuwa na sifa za kupewa pension au anapewa tu kiasi alichokatwa wakati wa utumishi wake?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kupoteza muda kuwategemea wabunge wa ccm (ambao ndio wengi) usitarijie lolote la maana. Kumbuka ndio waliopitisha sheria kandamizi za mifuko kulipa kwa mkupuo 33% kabla Raisi hajaingilia kati!
Kuwategemea hawa wabunge wa ccm ni kupoteza muda na wakati.

Dawa hapa ni TUCTA kwenda mahakamani kudai haki za wafanayakzi ktk mafao, sema na TUCTA yenyewe hakuna viongozi bali siku hizi kuna wachumia tumbo!
 
We ulisha ambiwa ni yawanyonge unataka wanyonge kama ninyi muishe halafu iitwe serikali ya mabeberu au? Lazima muendelee kuwa wanyonge ili iitwe serikali ya wanyonge

Turud kwenye mada.. Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni
 
Ni afadhari wangesema mfanyakazi aliyeachishwa kazi anaweza kuyachukua mafao yake miaka 3 baada ya kuacha kazi na sio mpaka afanikiwe kufikisha miaka 55/60
 
Hapa serikali ilikosea sana na kibaya Zaidi ilibagua hao wabunge na viongozi wengine wao wakistaafu wanapewa chao chote kwa watumishi ndio shida. hii sio kwa ajili ya kumsaidia mtumishi bali ni kumnyonya
 
Wengi wa Watanzania huwa hawaamini tusemapo......"adui mkubwa wa Nchi hii ni CCM" cku zote inaweka sheria Kandamizi Kwa wapiga kura wake...

Hao hao Wabunge wa CCM kwa kutumia wingi wao waliipinga Katiba ya Jaji Joseph Sinde Warioba, ambayo kimsingi ingepunguza matumizi ya hovyo ndani ya Serikali yetu....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah. Inaumiza sana wadau. Yaani hata wajaribu tuu kusema wanachama wafike kwenye offisi za NSSF wapige kura tuone au waanzishe web ambayo mwanachama atawezakupiga kura tuu yaani unaingiza No.

zako za NSSF then inaweza kupiga kura uone kama wanachama watasema huo upuuzi wa kusubiria miaka 55. wizi wizi wizi mtupuuuuu CCM.

Cha kushangaza hao hao wabunge wanaopitisha watoto wao wanakuja kuwa waajiriwa na wabunge wengine kutokana ni vijana baada ya ubunge kuisha wanakuja kuwa waajiriwa.

Laana haitaacha kuwatafuna
 
Ndugu yangu pole wewe, na pole sote kwa changamoto hii, kwa kweli hali ni mbaya sana, kuna ndugu yangu alikuja kuniomba ushauri kuhusu changamoto anazopitia kuhusu mafao yake ya NSSF, na alitaka kufanya maamuzi magumu na mabaya sana, nimamwambia ' Omba Mungu akuongoze, achana na NSSF, tafuta vyanzo vingine mbadala vya kipato ili maisha yaendelee'.
 
Hapa serikali ilikosea sana na kibaya Zaidi ilibagua hao wabunge na viongozi wengine wao wakistaafu wanapewa chao chote kwa watumishi ndio shida. hii sio kwa ajili ya kumsaidia mtumishi bali ni kumnyonya
Ndio wanasiasa wetu hao! Wao wanajali maslahi yao tu ila ya wapiganaji kura hayawahusu.
 
  • wameweka miaka 55 hadi 60 wakati mamlaka yao halali inasema wastani wa maisha ya kuishi mtanzania ni miaka 45,. this is real definition of rubbish.
  • Hyo miaka 55 hadi 60 labda kwa wajapani
 
Kwa ufupi kabisa Serikali zote za Africa ni wakoloni weusi, tena bora hata mkoloni Mzungu maana kuna wakati aliona haya.
Hawa viongozi mimi imefika wakati nawaombea mabaya tu, kwa jinsi wanavyotufanyia sisi watu wanyonge, kuna wakati pia najiuliza hivi hakuna namna tukafungua kesi za kikatiba?
Maana kulalama bila Action kwa wakoloni hawa weusi ni kazi bure kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wabunge wa CCM wakiwa mle ndani akili zao wanaziacha nje! Nimehangaika sana na NSSF. Nawachukia sana sana na serikali yao. Nasubiri Loan Board wanidai niwaambie wakachukue pesa NSSF

Kitochi Original
 
Kwa ufupi kabisa Serikali zote za Africa ni wakoloni weusi, tena bora hata mkoloni Mzungu maana kuna wakati aliona haya.
Hawa viongozi mimi imefika wakati nawaombea mabaya tu, kwa jinsi wanavyotufanyia sisi watu wanyonge, kuna wakati pia najiuliza hivi hakuna namna tukafungua kesi za kikatiba?
Maana kulalama bila Action kwa wakoloni hawa weusi ni kazi bure kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
hahaha wakoloni weusi sio
 
Ni kupoteza muda kuwategemea wabunge wa ccm (ambao ndio wengi) usitarijie lolote la maana. Kumbuka ndio waliopitisha sheria kandamizi za mifuko kulipa kwa mkupuo 33% kabla Raisi hajaingilia kati!
Kuwategemea hawa wabunge wa ccm ni kupoteza muda na wakati.

Dawa hapa ni TUCTA kwenda mahakamani kudai haki za wafanayakzi ktk mafao, sema na TUCTA yenyewe hakuna viongozi bali siku hizi kuna wachumia tumbo!
Wachumia tumbo
 
Back
Top Bottom