Hivi kwanini hununui na kusoma vitabu?

Bonheur Travels Tanzania

JF-Expert Member
Dec 29, 2020
252
499
Salaam,

Tunaendelea kutatua changamoto na kutoa elimu kwa umma katika nyanja mbalimbali.

Uzi huu tutautumia kujua sababu za watu kutosoma vitabu hasa hapa nchini Tanzania. Lazima kuna shida mahali!

Wataalamu wameshaeleza na kuthibitisha kuwa usomaji wa vitabu husaidia kunoa ubongo, kubadilisha tabia za mtu/jamii, kumsaidia kudhibiti mazingira, biashara na faida nyingine lukuki ikiwemo burudani na kusafiri kimawazo, kihisia na kujifunza.

Pia mtu anayesoma na asiyesoma vitabu utofauti wao mkubwa upo kwenye namna ya kufikiri na kutatua changamoto.

Labda tukuulize wewe ambaye huna utaratibu wa kujisomea vitabu; Kwanini hununui kitabu na kusoma? Je, hupendi au basi tu? Nini kifanyike upate ari ya kusoma vitabu?

Funguka, tuzungumze.
 
Halaf wengi ni choka mbaya, watu wa fantasies. Yaan nitoke kibaruan nmechoka nisilale nisome kitabu. Vitabu nilivyosoma toka darasa la kwanza mpaka namaliza chuo kikuu miaka mi4 vinatosha sana kwa maarifa.
Kama sababu ni kuchoka na kazi, vipi kujisomea kwa siku za mapumziko?
 
Kusoma vitabu kwangu sio desturi wala sina mazoea japo nina softcopy ya baadhi ya vitabu.

Mpaka siku hiyo niwe na vibe la kusoma ndio utaniona nimetulia, na mara nyingi huwa sisomi kwa muda mrefu unakuta dakika kadhaa tu nishakua bored naacha.

Sijawahi soma kitabu mwanzo mpaka mwisho nikakimaliza.
 
Issue ni kusoma vitabu au ni lazima tuvinunue kwanza hivyo vitabu? Mpangilio wa maneno katika kichwa cha uzi wako unaonesha msisitizo ni kununua (biashara) na si kusoma.

Kama tulivyoeleza, tulianza na kununua ili kupima commitment. Mtu anayesoma vitabu huwa ananunua pia japo sio mara zote.

Bado swali la kusoma ni halali; wewe ni msomaji wa vitabu?
 
Binafsi sikukuzwa hivyo ndio maana nashindwa kusoma, ila kununua nanunua kimtindo, huku nilipo boss wangu anasoma sana vitabu, amenishawishi nisome nikamwambia anilipe kwa kila kitabu ntakachosoma akaniona hamnazo.
Hukukuzwa hivyo. Sababu nzuri na ina mashiko.

Kwahiyo unaamini mtoto akikuzwa na tabia ya kusoma vitabu atadumu nayo, siyo?

Na wewe ambaye angalau unanunua mara moja moja, unadhani unahitaji kusaidiwaje ili upate ari ya kusoma?
 
Kusoma vitabu kwangu sio desturi wala sina mazoea japo nina softcopy ya baadhi ya vitabu.

Mpaka siku hiyo niwe na vibe la kusoma ndio utaniona nimetulia, na mara nyingi huwa sisomi kwa muda mrefu unakuta dakika kadhaa tu nishakua bored naacha

Sijawahi soma kitabu mwanzo mpaka mwisho nikakimaliza

Mpaka siku uwe na vibe.

Nini huwa kinakuboa haraka hivyo mkuu hadi ushindwe kusoma kitabu mpaka mwisho: Je, ni kitabu kuwa kirefu chenye kurasa nyingi au unachosoma hakikufurahishi tena?
 
Napenda kusoma vitabu vya riwaya tu, yan napenda haswa. Ila viwe kwa Kiswahili MF. Damu na Machozi, Rais Anampenda Mke Wangu, Mfadhili, Vuta N'kuvute, Takadini and the like.

Vya kiingereza nasomeaga kwenye app ya AnyBook, nina think big hardcopy ila kusoma ni kipengele. Nikijitahidi sana pg 4/5 nachoka, nakuwa bored. Nashindwa kuendelea mpaka miezi kadhaa mbele.
 

Similar Discussions

10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom