Ngwanakilala
JF-Expert Member
- Jun 25, 2011
- 774
- 1,456
Habari za mchana waungwana,
Nimekua najiuliza hili swali labda kuna wataalamu watusaidie. Ni kwanini hakuna vijiji au marafiki au vikundi au taasisi zinazo anzisha bima ya kuwakinga wanachama wake na majanga - community based? zikasajiliwa na kufuata taratibu zote za TIRA
Tumeona kuna taasisi, vikundi na makundi mengi yameanzisha mabenki na vikoba ili kusaidiana kifedha. Kwamfano wanajeshi wana saccos yao, Mapolsi wana Saccos yao, wapo wana vijiji, wapo wafanyakazi wanao fanyakazi pamoja wameanzisha saccos na vikoba ili kusaidiana kifedha. Wpo watu wameanzisha mpaka benki kama Mbinga Community Bank nk
Jambo ambalo sielewi ni kwanini model hiyohiyo haitumiki katika bima za kijikinga kwa majanga? Kwa mfano kwanini wafanyakazi wa mashirka makubwa yenye wafanyakazi zaidi ya 300 kama CRDB, Tigo, Aitel, NSSF, Vodacom au wanajeshi , mapolisi au wanakijiji fulani au watu wa mkoa fulani wanaoishi Dar es salaam wenye umoja wao wasiwekeane utaratibu wa kwamba kila mwana chama awe analipa kiasi fulani chafedha kila mwezi kama bima / kinga ya majanga fulani. Mnaweza kudefine hayo majanga yakawa kama 5 tu ili kulimit exposure. Mnaweza kusema kila mwanachama achange 50,000 kila mwezi kama bima ya ajali ya gari, moto wa nyumba au gari, kufiwa na mume au mke au mtoto na kupoteza ajira. na wakaandika kabisa yaani waka define ukipata janga lifuatalo utalipwa kiasi kifuatacho - choice is yours.
Ajali ya gari - million 5 (kama tutajiridhisha ajali ni genuine)
Moto wa nyumba - Million 10 (kama tutajirisha mto ni genuine)
kufiwa na mke au mume - million 5
Kufiwa na mtoto - million 3
Hasara katika biashara yako - million 7 (kama tutajirisha hasara ni genuine)
Kupoteza kazi/ ajira - million 7
Hii ni bima unayolipia premium ndogo nayo inakupa protection ndogo lakini ya uhakika
Just thinking out loud - ni kwanini hii model haipo katika jamii?
Tujadiliane
Nimekua najiuliza hili swali labda kuna wataalamu watusaidie. Ni kwanini hakuna vijiji au marafiki au vikundi au taasisi zinazo anzisha bima ya kuwakinga wanachama wake na majanga - community based? zikasajiliwa na kufuata taratibu zote za TIRA
Tumeona kuna taasisi, vikundi na makundi mengi yameanzisha mabenki na vikoba ili kusaidiana kifedha. Kwamfano wanajeshi wana saccos yao, Mapolsi wana Saccos yao, wapo wana vijiji, wapo wafanyakazi wanao fanyakazi pamoja wameanzisha saccos na vikoba ili kusaidiana kifedha. Wpo watu wameanzisha mpaka benki kama Mbinga Community Bank nk
Jambo ambalo sielewi ni kwanini model hiyohiyo haitumiki katika bima za kijikinga kwa majanga? Kwa mfano kwanini wafanyakazi wa mashirka makubwa yenye wafanyakazi zaidi ya 300 kama CRDB, Tigo, Aitel, NSSF, Vodacom au wanajeshi , mapolisi au wanakijiji fulani au watu wa mkoa fulani wanaoishi Dar es salaam wenye umoja wao wasiwekeane utaratibu wa kwamba kila mwana chama awe analipa kiasi fulani chafedha kila mwezi kama bima / kinga ya majanga fulani. Mnaweza kudefine hayo majanga yakawa kama 5 tu ili kulimit exposure. Mnaweza kusema kila mwanachama achange 50,000 kila mwezi kama bima ya ajali ya gari, moto wa nyumba au gari, kufiwa na mume au mke au mtoto na kupoteza ajira. na wakaandika kabisa yaani waka define ukipata janga lifuatalo utalipwa kiasi kifuatacho - choice is yours.
Ajali ya gari - million 5 (kama tutajiridhisha ajali ni genuine)
Moto wa nyumba - Million 10 (kama tutajirisha mto ni genuine)
kufiwa na mke au mume - million 5
Kufiwa na mtoto - million 3
Hasara katika biashara yako - million 7 (kama tutajirisha hasara ni genuine)
Kupoteza kazi/ ajira - million 7
Hii ni bima unayolipia premium ndogo nayo inakupa protection ndogo lakini ya uhakika
Just thinking out loud - ni kwanini hii model haipo katika jamii?
Tujadiliane