Mafiningo
JF-Expert Member
- Sep 5, 2016
- 4,436
- 4,646
Asijiuzuru, aende tu akapige makofi akunje njaro zake vema mfukoni.Wakuu Salaam:
Nazunguka kila site kufatilia kinachojiri kuhusu matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika juzi.
Mh.Aidah Khenan ameshinda kupitia CHADEMA dhidi ya Kessy kule Nkasi Kaskazini. Sasa kinachoshangaza ni baadhi ya watu ambao pia wana Profile nzuri tuu kwa namna fulani wanapendekeza hata huu Ubunge alioshinda huyu Mh. aupige chini.
Ubunge ni kazi kama kazi zingine na yeye pia anao wanaomwangalia na ndicho alichokua anapigania muda wote wa kampeni.
Ule ulikua ni uchaguzi na yeye ndiyo katangazwa, kwanini watu wanapendekeza na kutoa maoni kabisa asikubali na wala asiende bungeni wakati ndiyo yeye katangazwa?