Hivi kwanini ajenda ya mafisadi imekufa kwa vyama vyote?

Ne Mbwitu

JF-Expert Member
Aug 23, 2020
275
801
Dr Slaa na Lissu ndo waasisi wa ajenda ya kupambana na mafisadi. Hawa waliwataja orodha ya mafisadi ( list of shame) pale Mwembeyanga Temeke bila hofu wala kupepesa macho. Baadae wababe hawa walizunguka nchi nzima na ajenda hii katika uchaguzi wa mwaka 2010.

Baada ya mmoja wa mafisadi waliotajwa Mwembeyanga, yaani Lowassa, kuingia upinzani, ajenda ya ufisadi ikafa midomoni mwa ukawa na kuhamia kwa CCM na Magufuli. Katika kampeni zake, Magufuli aliahidi kujenga mahakama ya mafisadi ili Lowassa ashtakiwe na afungwe.

Hivi sasa Lowassa amerudi CCM.

Katika uchaguzi huu, pande zote mbili yaani CCM na Upinzani umeua ajenda ya ufisadi. Lakini sio kwamba ufisadi haujafanyika awamu hii. Upo tena babalao ufisadi.

Sasa ni jambo la kushangaza, hakuna hata mgombea mmoja anayekerwa na ufisadi. Sio Lissu wala sio Magufuli. Je, kuna siri gani?
 
Serikali ya ccm inawalinda mafisadi na chadema nao wakachukua fisadi moja wakataka kulipeka ikulu,watu walipohoji kuhusu hilo fisadi wakajibiwa kwa swali "kama fisadi mbona hashtakiwi"? watu wakaufyata kimya.

Halafu leo hivyo vyama vyeje kuongelea ufisadi kwenye kampeni? Bora viongelee mengine tu.
 
2454298_Screenshot_2020-07-12-20-49-41.jpg
 
Uzi Kama huu,bavicha wanaurukaaa na kwenda nyuzi zinazowafurahisha nafsi zao.

WaTZ hawajawahi kua wajinga kwa miaka 10 mfululizo,Leo uniambie ni Fisadi papa,kesho umsafishe kwa dodoki Kisha umlete Kama mgombea uraisi.
Ndo mana wanaonekana matapeli tu
 
Agenda ya Ufisadi haiwezi kuwepo kwenye uchaguzi wa aina hii. Ukabulu unaofanywa na CCM ndiyo itakuwa agenda kuu ya uchaguzi au kampeni za mwaka huu. CCM wameamua kufanya dhurma ya wazi halafu wa nakuja na propaganda za uvunjaji amani.
 
Watu wamegundua ni bora 💯💯💯 kuwa na Rais Fisadi kuliko Joka 🐍🐍🐍katili lisilo na utu.

Utu na ubinadamu umekuwa adimu sana kiasi kwamba watu wanautafuta kwanza kabla ya kukimbilia kufuta Ufisadi

Yaani ni bora Ufisadi kuliko Ukatili.
 
..ajenda ya ufisadi ilikuwa haiwagusi wananchi.

..cdm walihangaika nayo lakini ajenda hiyo haikuonekana kuwapa matokeo mazuri ktk sanduku la kura.

..ilipofika mwaka 2015 wakaamua kuachana na ajenda hiyo na kumchukua EL kuwa mgombea wao.

..imani ya CDM ilikuwa kwamba ili kuishinda CCM unapaswa kuleta mpasuko ktk chama hicho, na waliamini EL angeleta mpasuko ktk CCM.

..CCM walirithi ajenda ya ufisadi wakati wa kampeni za 2015, lakini hata wao hawakupata chochote kikubwa kutokana na ajenda hiyo.

..Kwa hiyo baada ya 2015 vyama vyote vimefikia conclusion kwamba ajenda ya ufisadi hailipi ktk siasa za Tz.
 
Dr Slaa na Lissu ndo waasisi wa ajenda ya kupambana na mafisadi. Hawa waliwataja orodha ya mafisadi ( list of shame) pale Mwembeyanga Temeke bila hofu wala kupepesa macho. Baadae wababe hawa walizunguka nchi nzima na ajenda hii katika uchaguzi wa mwaka 2010.

Baada ya mmoja wa mafisadi waliotajwa Mwembeyanga, yaani Lowassa, kuingia upinzani, ajenda ya ufisadi ikafa midomoni mwa ukawa na kuhamia kwa CCM na Magufuli. Katika kampeni zake, Magufuli aliahidi kujenga mahakama ya mafisadi ili Lowassa ashtakiwe na afungwe.

Hivi sasa Lowassa amerudi CCM.

Katika uchaguzi huu, pande zote mbili yaani CCM na Upinzani umeua ajenda ya ufisadi. Lakini sio kwamba ufisadi haujafanyika awamu hii. Upo tena babalao ufisadi.

Sasa ni jambo la kushangaza, hakuna hata mgombea mmoja anayekerwa na ufisadi. Sio Lissu wala sio Magufuli. Je, kuna siri gani?
Kampeni zikianza itakuwa siyo agenda ya mafisadi tena, bali kampeni ya LIFISADI LIKUU, KIONGOZI LA MAFISADI LILILOIBA TRILLION 1.5
 
Ufisadi hauonekani kuwa tatizo kwa nchi yetu, hata huyu uchwara aliyeikwapua na kuanzisha kile alichokiita mahakama ya mafisadi ila hakuna washtakiwa.... rejea ripoti ya CAG Assad na ukwapuzi wa 1.5 trillions!

Wananchi wameendelea kuteseka na maisha magumu tena zaidi, kama tumedhibiti ufisadi lakini neema hakuna... tumeona sio tatizo labda tujaribu kuokoteza agenda zingine!
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom