Hivi, kwani TANESCO ni nini hasa??!!!

C.K

JF-Expert Member
Nov 5, 2010
394
162
Hivi hakuna uwezekano wa kuwa na makampuni yanayotoa huduma ya umeme zaidi ya moja kama ilivyo kwa makampuni ya simu za mkononi?? Kwa nini TANESCO wawe monopoly kiasi hicho?, kwani TANESCO ni nini hasa??!!!!! Au na hilo nalo tudai kama tunavyodai Katiba ya nchi na Tume nyingine ya uchaguzi?!

Ona sasa eti wanataka kupandisha gharama za umeme kwa asilimia 18%, mambo gani haya?! Au ndo tushaanza kulipa gharama za uchaguzi za C*M za mat-shirt, kofia, mabango na noti walizo kuwa wanagawa bure?!. Ufisadi huu jamani. Na bado, huo ni mwanzo tu.

Tusikubali, hakuna kukubali!! Tuungane na CHADEMA kulipinga hili.
 
Sio kwamba wanataka kupandisha.. ndio zishapanda hivyo, halafu yule mjin..a juzi anasema mgao utakua historia! pambaf kabisa, goodnight nalalaa sitaki maneno na mtu
 
TANESCO = Tanganyika Elecricity Society Copcop.

Sina maana kuwa nataka kujua kirefu cha neno TANESCO, kama hujui ni Tanzania Electricity Supply Company. Kuwa serious kwenye mambo yanayohitaji userious!
 
Sina maana kuwa nataka kujua kirefu cha neno TANESCO, kama hujui ni Tanzania Electricity Supply Company. Kuwa serious kwenye mambo yanayohitaji userious!

Wewe ndo kilaza kweli, yaani mpaka hapo ulipo hujui TANESCO ni nini hasa? Wewe ni mtanzania au mkimbizi mahali fulani?

Please be specific with your query.
 
vache kumshambulia mtoa hoja anahitaji msaada wa kifikra. Kiukweli tanesco wanatetea maslah wanahitaji pesa walizohonga wakati wa kampeni.
 
Sina maana kuwa nataka kujua kirefu cha neno TANESCO, kama hujui ni Tanzania Electricity Supply Company. Kuwa serious kwenye mambo yanayohitaji userious!
Mkuu, Hapo ndipo ujue unapambana na wapevu wa fikra! Great thinkers!!
Tanesco! Ndio njia pekee iliyobaki ya kukomba vijisenti vya wadanganyika walivojiwekea akiba baada ya EPA na wale mapacha wawili kufariki kifo cha kawaida RICHMOND na nduguye DOWANS. usisahau ikiisha hiyo kuna na la ATCL linakuja mda si mrefu....
 
wafanyakazi 5000. vishoka 5000. kazi kwelikweli, wale ubinafsi na uroho wa madaraka ukabila na udini ni mambo ya ndani bila kusahau rushwa , imejaa kwa kiwango kikubwa miongoni mwa wafanyakazi kiasi kuitana majina eti wengine ni SLP( WAMESOMA ZAMANI) na dot com ( wamesoma sasa) vyote hivi vinachangia kuliangamiza shirika na ndio maana kila kukicha hawana njia mbadala wa kutatua tatizo la umeme zaidi ya kushughulikia maslahi yao. serikali nayo kwa upande wake maamuzi ya kisiasa ndio yanazidisha ugumu wa kupata ufumbuzi wa matatizo ya tanesco, matokeo yake sas ule ugonjwa wa serikali wa kuona jicho moja kuwa kodi ni lazima itokane na bia, sigara, na soda ndio hilohilo limeamia huko kwa kudhani dawa ya upatikanaji wa umeme utaletwa na kupandisha bei kila mwezi, HOVYO KABISA
 
wafanyakazi 5000. vishoka 5000. kazi kwelikweli, wale ubinafsi na uroho wa madaraka ukabila na udini ni mambo ya ndani bila kusahau rushwa , imejaa kwa kiwango kikubwa miongoni mwa wafanyakazi kiasi kuitana majina eti wengine ni SLP( WAMESOMA ZAMANI) na dot com ( wamesoma sasa) vyote hivi vinachangia kuliangamiza shirika na ndio maana kila kukicha hawana njia mbadala wa kutatua tatizo la umeme zaidi ya kushughulikia maslahi yao. serikali nayo kwa upande wake maamuzi ya kisiasa ndio yanazidisha ugumu wa kupata ufumbuzi wa matatizo ya tanesco, matokeo yake sas ule ugonjwa wa serikali wa kuona jicho moja kuwa kodi ni lazima itokane na bia, sigara, na soda ndio hilohilo limeamia huko kwa kudhani dawa ya upatikanaji wa umeme utaletwa na kupandisha bei kila mwezi, HOVYO KABISA

kuwepo wasomi wa sasa na wazamani si hoja ya msingi maana sehemu nyingi za kazi zina-structure hiyo. Chamsingi ni serikali ku-liberalize sekta hii nyeti. Kinyume chake ilitakiwa kuwa efficient kiasi cha kufikia watu wengi na kudhibiti mapato yake bila kuwepo ulazima wa kuongeza bei kila mara kama inavyofanya sasa. Nashangaa wachumi wetu serikalini wanafanya nini katika kudhibiti hili. "monopolist" siku zote hutafuta kunyonya wateja na ni kitu sahihi kwa mfanyabiashara yeyote. Swali la kujiuliza ni: kila siku tunaambiwa TANESCO inatafuta kujiendesha, maana yake inakuwa kampuni ya biashara na si huduma ya serikali? kama jibu ni ndiyo, basi yaruhusiwe makampuni mengine binafsi kufanya uzalishaji na usambambaji wa umeme bila kulazimika kuiuzia TANESCO maana sekta itakuwa huru kupambana kibiashara. Matokeo ya zoezi hili ni nafuu kwa mtumiaji "consumer" maana atakuwa na uwezo wa kuhama kutoka mtoa huduma mmoja kwenda mwingine tena kwa "switching costs" ndogo sana.
 
Back
Top Bottom