Hivi kwa nini wanawake wanajitongozesha kwa Watumishi wa Mungu?

Shetani yuko bize, kwa nini na nyie watu wa Mungu hamtaki kuwa bize?
Nyie ni wavivu kusali tena wavivu kusoma biblia, utamshindaje shetani?
 
Utakuta mtu anafahamu fika kuwa wewe umeokoka, tena ni kiongozi wa kanisa, lakini cha ajabu wanawake haohao wanaokujua vyema, na ambao ni walokole wenzako ndio wanakuwa vimbelembele wa kutaka ufanye nao ngono, na ukiwakemea wanakuambia baada ya dhambi hiyo mtatubu.
Wengine wanaenda mbali zaidi, ukiwakataa wanaanza kukusingizia maneno ya uwongo kuwa unawataka.
Ndugu zanguni, kazi ya Mungu ni ngumu sana na shetani anajiinua sana.
Tuwaombee sana watumishi wa Mungu, wanapita mapito magumu sana kiimani

khaaaaaaa_ya kweli haya,...!

By the way_ulokole ni kitu/dhehebu gani?
 
Hayo ni majaribu unalalamika nini na wewe?
Kwani hukuona Shetani alikuwa anamjaribu yesu
Au wokovu wako ni wa mashaka????
 
hahahahahahahahahahah loohh imenibidi nicheke kwa kweli.. Roulette tatizo la watumishi wengi huwa wanadhani wao hawatendi dhambi "watakatifu"
na hata wakitenda is "someones else fault" na kumbe sote ni binadamu tu dhambi kitu cha kawaida..
Hapo kwenye RED nimekupata vizuri afrodenzi
 
Utakuta mtu anafahamu fika kuwa wewe umeokoka, tena ni kiongozi wa kanisa, lakini cha ajabu wanawake haohao wanaokujua vyema, na ambao ni walokole wenzako ndio wanakuwa vimbelembele wa kutaka ufanye nao ngono, na ukiwakemea wanakuambia baada ya dhambi hiyo mtatubu.
Wengine wanaenda mbali zaidi, ukiwakataa wanaanza kukusingizia maneno ya uwongo kuwa unawataka.
Ndugu zanguni, kazi ya Mungu ni ngumu sana na shetani anajiinua sana.
Tuwaombee sana watumishi wa Mungu, wanapita mapito magumu sana kiimani

Yale yale ya Adam kudai amekula tunda kwa sababu ya mwanamke (Hawa) wakati naye alilitamani baada ya kuletewa.
 
basi kazi ipo dunian hapa............!

Umeona eeh....kuna mdada mmoko frm rwanda siku iyo hakuwa na hela...basi akanipigia simu akaniambia "babeee today Im poor gel, I dont have even single coin"...nilicheka sana!!
 
Umeona eeh....kuna mdada mmoko frm rwanda siku iyo hakuwa na hela...basi akanipigia simu akaniambia "babeee today Im poor gel, I dont have even single coin"...nilicheka sana!!
sasa ulimpa ama?? manake hukawii kuwa uiona anakuchuna manake ndo wanaume wa bongo mlivyo
 
Kujitongosesha??? Mtumishi wa Mungu akitongoza hawezi kusema katongoza, anasema alitongozeshwa, is it? kama kondoo linajileta kwa mchungaji ni ruhusa tosha kwa mchungaji kuila na baadae kujitetea kwamba kondoo ilimshawishi?

Wanawake bana,kwanini msizungumzie alichozungumza mtoa mada?Mnaleta excuse!!Kazi sana!
 
Utakuta mtu anafahamu fika kuwa wewe umeokoka, tena ni kiongozi wa kanisa, lakini cha ajabu wanawake haohao wanaokujua vyema, na ambao ni walokole wenzako ndio wanakuwa vimbelembele wa kutaka ufanye nao ngono, na ukiwakemea wanakuambia baada ya dhambi hiyo mtatubu.
Wengine wanaenda mbali zaidi, ukiwakataa wanaanza kukusingizia maneno ya uwongo kuwa unawataka.
Ndugu zanguni, kazi ya Mungu ni ngumu sana na shetani anajiinua sana.
Tuwaombee sana watumishi wa Mungu, wanapita mapito magumu sana kiimani

Aiseeeee........mimi nina experience tofauti kidogo mikela, kwanza pole na hayo majaribu unayokutana nayo nina imani unaweza kuepukana nayo ukitaka. Ila binafsi kuna tabia inanikera sana kuhusu wachungaji/mitume/manabii kama wanavyojiita. Inasikitisha sana wachungaji kutongoza waumini inasikitisha sanaaaa. Mtu anaenda kwenye maombi halafu mchungaji anakwambia baada ya maombi unione bwana amaenionyesha jambo, unasubiri kusikia hilo jambo anaanza kukupa storiiiii zisio na kichwa wala miguu halafu mwisho anakwambia mpange siku mkapate chai pamoja mara sijui uende nyumbani kwake atatayarisha chakula cha jioni mara sijui kila baada ya maombi watu wakiondoka wewe inabidi ubaki kwa maombi maalumu jamaniiiiiiii tutafika kweli huko mbeleni???!!!!!tabia chafu sanaaaa.

Wachungaji badilikeni kama mnapitia humu ndani........mjiheshimu na kazi zenu. Waumini wanavyokuja kwenye maombi hawaji kutafuta mapenzi kwa wachungaji.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom