HorsePower
JF-Expert Member
- Aug 22, 2008
- 3,612
- 2,566
Juzi na jana, kupitia taarifa ya hbr ya ITV nilisikia hbr ya dada mmoja aliyefiwa na mumewe ambaye likuwa anadai mirathi yake kwenye kampuni la waarabu na huyo boss wake akamtumia meseji nyingi kuwa waonane usiku kuanzia saa nne akiwa pekee yake na amuache mtoto wake mchanga ili aweze kumsaidia.
Alipojaribu kumreport kituoni (maana mazingira yanaonyesha unyanyasaji na rushwa ya ngono) alikutana na polisi (mwanamke) na huyo polisi badala ya kumsaidia yule mama (asinyanyaswe kwa kutoa rushwa ya ngono kupata haki yake) alimnyang'anya simu na kuzifuta zile meseji kuondoa ushahidi (na hii inaonyesha rushwa toka kwa yule boss.)
Matukio kama haya ya wanawake kuwakandamiza wanawake wenzao ni mengi sana na hususan maofisini ambapo maboss wanawake (baadhi yao) pia wamekuwa wakiwanyanyasa wanawake wenzao na hili limekuwa linanikera sana sana.
Naomba kuuliza swali, kwa nini BAADHI ya wanawake wanakuwa wakatili dihidi ya wanawake wenzao kwa mfano wa hapo juu?
Alipojaribu kumreport kituoni (maana mazingira yanaonyesha unyanyasaji na rushwa ya ngono) alikutana na polisi (mwanamke) na huyo polisi badala ya kumsaidia yule mama (asinyanyaswe kwa kutoa rushwa ya ngono kupata haki yake) alimnyang'anya simu na kuzifuta zile meseji kuondoa ushahidi (na hii inaonyesha rushwa toka kwa yule boss.)
Matukio kama haya ya wanawake kuwakandamiza wanawake wenzao ni mengi sana na hususan maofisini ambapo maboss wanawake (baadhi yao) pia wamekuwa wakiwanyanyasa wanawake wenzao na hili limekuwa linanikera sana sana.
Naomba kuuliza swali, kwa nini BAADHI ya wanawake wanakuwa wakatili dihidi ya wanawake wenzao kwa mfano wa hapo juu?