Hivi kwa nini tunaendekeza sana imani za kishirikina?

...ha ha ha... haki ya mungu hata mie chakula cha jirani kilikuwa kinanitoa mate kila siku ...sijui ilikuwa ni utoto? lakini hata wazungu wana msemo "the grass looks greener on the other side!"

...tukirudi kwenye sayansi ya mwafrika; ...na ile ya wale watoto wanaovimba vitumbo halafu unaambiwa "kalambishwa", au "kabemendwa" nayo imekaaje?

QM na Mbu mmenichekesha sana!
Unajua watoto huwa wana kawaida ya kukataa chakula kwao na kupenda kula kwa jirani...hasa wale wakorofi wa kula..na hii hutia aibu maana inaweza kutafsirika kuwa kwao hamna chakula!..Nadhani kama Mbu alivyosema the grass looks greener across the fence.

Kuhusu Kubemendwa ..huu ni msemo niliusikia kwa mara ya kwanza kwenye one of bongo flava songs...na baadae nikasoma kwenye makala.Sijui kama ni ushirikina as such au ni imani potofu kwamba mtoto hudhurika pale mama anapokuwa na mahusiano na mtu tofauti ( mbali na baba ya mtoto).Kama tukichambua kisayansi huwezi kuona co-relation..ila ukiangalia kisayansi..labda kama mama ni mzururaji na hajali usafi binafsi au kuangalia mwanae kwa karibu ni kweli mtoto anaweza kudhurika.Hii itatokea hata pale mama atakapokuwa mzembe kiusafi au vinginevyo hata kama hana mahusiano nje ya ndoa/mbali na baba ya mtoto.
 
Eh WOS! Si unajua wakati mwingine inabidi ku-compare menu ya 'home' na ya 'jirani.' Sasa unakuta maharage ya home yapoyapo tu, yameungwa kwa vitunguu na mafuta basi. Lakini maharage ya kwa jirani yananukia nazi, iliki, na pilipili mbuzi. Sasa hebu niambie, mtoto akipiga ana-ana-do lazima mkono uangukie kwa jirani. LOL




Next time ukialikwa kwenye harusi, nenda na khanga, halafu jaribu kwenda kumvisha bibi harusi (wakati wa kutoa zawadi). Wallahi hautaweza kumfikia bibi harusi. Utaona jinsi utakavyopigwa bonge la stop na 'shangazi-mpenda-shari.' Na ukifanikiwa kumvalisha, hiyo khanga itavulia in a blink of an eye. hautajua hata nani kaivua, kwa jinsi itavyovuliwa haraka.

Kwa nini usijaribu?...halafu uje utupe feedback



Hivi jicho baya nayo ni sehemu ya imani za kishirikina? Na kuna ile ya 'mdomo mbaya' pia.

QM,
Hunitakii mema naona!Kisa cha kuitwa mchawi kwenye harusi za watu?? kisa nije kuwapa ushuhuda hapa JF!
Utanisamehe maana mtihani huo wala sijaribu.
 
...Je Limbwata?

hujawahi kuona mume anafanyiwa kila kisa na mkewe yeye yupo yupo tu?

Nitakupa mfano mwingine; nilipokuwa Boarding school, na wenzangu tulikuwa tunatoroka kwenda uswahilini kula kwa mama ntilie... cha ajabu umati wa watu ulikuwa unang'ang'ania kula kwa kina mama fulani fulani tu, hata kama ni makoko,... wale mama ntilie wengine aaahh... masufuria yao hayaguswi japo wali tele, bei moja, portion sawa, ladha ya wali wa nazi na maharagwe ya nazi bomba...

mpaka leo najiuliza imekaaje ile!
 
hapo kweli umenenea kwasababu hili swala la imani za kishirikina linazidi kushamiriri sana na watu wanashindwa kuamini muumba wao, na hili jambo linazidi kudidimiza watu sana. mimi naona elimu itolewe watu wahamasishe wamuamini mungu.
 
Back
Top Bottom