Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,530
- 217,789
Kiukweli nimeshangazwa sana na kitendo cha Rais wa Zanzibar kushiriki uzinduzi wa kilichoitwa Studio za Wasafi FM huko Zanzibar.
Zanzibar inayojitambulisha kama nchi, inao mawaziri walioteuliwa na Rais huyo huyo, miongoni mwao yumo Waziri wa Habari, huyu ndiye alipaswa kushiriki huu uzinduzi wa Studio kama hizi.
Rais wa nchi yenye changamoto nyingi kama Zanzibar, kuacha kuhangaika na Matatizo ya Wananchi na kushobokea uzinduzi wa Wasafi FM, ni Ishara kwamba majukumu ya Urais ni mepesi sana, kwamba kwenye uzinduzi huo angehudhuria Waziri tu ama hata DC kungepungua kitu gani?
Kiongozi unaacha kuhangaika na Uchumi wa Bluu uliotuaminisha kwamba utaondoa umasikini wetu, unaanza kuhangaika na Studio za Wasela! Mbona hujitokezi kuokoa ZBC inayopumulia mashine? Viongozi wetu mbona mnatuchukulia poa sana aisee?
Zanzibar inayojitambulisha kama nchi, inao mawaziri walioteuliwa na Rais huyo huyo, miongoni mwao yumo Waziri wa Habari, huyu ndiye alipaswa kushiriki huu uzinduzi wa Studio kama hizi.
Rais wa nchi yenye changamoto nyingi kama Zanzibar, kuacha kuhangaika na Matatizo ya Wananchi na kushobokea uzinduzi wa Wasafi FM, ni Ishara kwamba majukumu ya Urais ni mepesi sana, kwamba kwenye uzinduzi huo angehudhuria Waziri tu ama hata DC kungepungua kitu gani?
Kiongozi unaacha kuhangaika na Uchumi wa Bluu uliotuaminisha kwamba utaondoa umasikini wetu, unaanza kuhangaika na Studio za Wasela! Mbona hujitokezi kuokoa ZBC inayopumulia mashine? Viongozi wetu mbona mnatuchukulia poa sana aisee?